sheikh Yahya Hussein, anajenga heshima yake au anajidhalilisha?

Sumbalawinyo

JF-Expert Member
Sep 22, 2009
1,282
247
Namna ambavyo sheikh anavyotumia vyombo mbalimbali vya habari na mawasiliano kunadi unajimu wake, ni kama yuko kwenye promosheni ya biashara yake.
Kweli wasikilizaji wa unajimu wake wameongezeka sana, wengine wakimpuuza na wengine wakimsifu.
Je tukiliangalia kwa undani, heshima ya huyu mtabiri imeongezeka au imeporoka katika kipindi cha miaka hii mitano 2005-2010?
 
WAMTUMAINIO Bwana ni kama MLIMA SAYUNI Hawatatikisika milele yote.
SHEIKH YAHYA HAMTUMAINI BWANA, BADALA YAKE MAJINI NA MASHETANI NDIO TUMAINI LAKE,
THATS WHY HESHIMA YAKE KWENYE JAMII INAPOROMOKA KILA KUKICHA.
 
once a man and twice a child, ktk maisha ukizeeka unarudia utoto, naona sasa huyu mzee sasa anarudia utoto
 
Jamani kama kawaida yangu muono wangu ni tofauti .
ingawa mimi siamini mambo ya unajimu lakini ninaheshimu taaluma na wataalam. Kuhusu huyu mzee kuporomoka au kutoporoma ni nadharia ambayo kwa 'wanatafakuri' haipendezi sana ila cha msingi "'prove him wrong' na namna ya kuthibitisha aliyoyasema kuhusu uchaguzi mkuu ujao [nadhani hili limekera wengi] basi ni busara kungoja hadi uchaguzi upite na hapo ndipo tunapoweza kujadili kwa kina yale yote aliyoyasema na ndipo tutakapokuwa na haki ya kumbeza au kumsifu
 
Pia alitabiri kikwete atashinda ushindi wa kishindo, sijui atashindaje bila uchaguzi?
Tena alisema kuwa atakaye mpinga kikwete kwenye uchaguzi atakufa... Sijui ni uchaguzi upi?
Huyu jamaa anajichanganya sana yeye na kauli zake.
 
Kama kweli yeye ni mtabiri mbona hajawahi kutabiri lini yeye atakufa?

Kazi kuiombea mabaya nchi na watu wasiokuwa na hatia.

ATUAMBIE YEYE ANAKUFA LINI?
 
Kwani alishawahi kuwa na heshima?

Kwa mujibu wa vyanzo mbalmbali vya habari:

=Aliwahi kutabiri vita dhidi ya Nduli Iddi Amini, ikatokea
=Aliwahi kutabiri moto kuwaka juu ya maji ikatokea kule Goma DRC
=Aliwahi kutabiri Mwanamuziki mwenye upara kufariki ghafla akiwa ******, utabiri huo ukamuangukia Brenda Fasi wa kule Afrika ya Kusini
=Aliwahi kutabiri Mwanmuziki maarufu kutoka nchi jirani aliyefungwa kuachiwa huru, wengi walidhani angekuwa ni Babu Seya, lakini utabiri huo ukamuangukia Papa Wemba wa kule DRC aliyefungwa kule nchini Ufaransa kutokana na kuingiza wahamiaji haramu kupitia Bendi yake.
=Aliwahi kutabiri Rais wa awamu ya tatu Mheshimiwa Benjamini Mkapa kuongezewa muda wa kuongoza nchi hata bada ya muda wake kuisha, wengi wakapiga kelele, lakini mwishowe ikatokea bada ya kifo cha mgombea mwenza wa chama kama sikosei TLP au Chadema na uchaguzi ukasogezwa na hivyo Rais wa wakati huo Mheshimiwa Mkapa akajikuta akiendelea kuongoza kwa muda zaidi ya kipindi chake, utabiri huo ulitimia.
=Alitabiri kifo cha Makamu wa Rais Hayati Dr. Omari Ali Juma na utabiri huo ulitimia.

Kwa kifupi zipo tabiri nyingi ambazo zilithibitishwa kutokea na hizi ni miongoni mwa tabiri hizo.
Kwa kifupi utabiri ni utaratibu wa kudadavua kitu ambacho aidha kinaweza kutokea au kisitokee kulinga na mazingira.
Taaluma hiyo ni ya kujifunza na mtu yeyote anaweza kujifunza akipenda.

Lakini hata hivyo umri nao unaweza kuchangia kiwango cha ufanisi kupungua na ndio sababu ya Sheikh Yahya kupoteza umaarufu, na ndio maana hata serikali kuweka umri wa waajiri wetu kustaafu, kutokana na kuchoka kiakili na kimwili. Hata hivyo hilo limeshindikana kutokana na watu wengi waliostaafu kutoka serikalini kukimbilia kwenye siasa. Inashangaza kidogo kwa kuwa kama mtu ameshindwa kwenye utumishi wa umma atawezaje uleta tija kwenye siasa.

Naona sasa ninachanganya mada, ngoja niishie hapa.

 
Kwa mujibu wa vyanzo mbalmbali vya habari:

=Aliwahi kutabiri vita dhidi ya Nduli Iddi Amini, ikatokea
=Aliwahi kutabiri moto kuwaka juu ya maji ikatokea kule Goma DRC
=Aliwahi kutabiri Mwanamuziki mwenye upara kufariki ghafla akiwa ******, utabiri huo ukamuangukia Brenda Fasi wa kule Afrika ya Kusini
=Aliwahi kutabiri Mwanmuziki maarufu kutoka nchi jirani aliyefungwa kuachiwa huru, wengi walidhani angekuwa ni Babu Seya, lakini utabiri huo ukamuangukia Papa Wemba wa kule DRC aliyefungwa kule nchini Ufaransa kutokana na kuingiza wahamiaji haramu kupitia Bendi yake.
=Aliwahi kutabiri Rais wa awamu ya tatu Mheshimiwa Benjamini Mkapa kuongezewa muda wa kuongoza nchi hata bada ya muda wake kuisha, wengi wakapiga kelele, lakini mwishowe ikatokea bada ya kifo cha mgombea mwenza wa chama kama sikosei TLP au Chadema na uchaguzi ukasogezwa na hivyo Rais wa wakati huo Mheshimiwa Mkapa akajikuta akiendelea kuongoza kwa muda zaidi ya kipindi chake, utabiri huo ulitimia.
=Alitabiri kifo cha Makamu wa Rais Hayati Dr. Omari Ali Juma na utabiri huo ulitimia.

Kwa kifupi zipo tabiri nyingi ambazo zilithibitishwa kutokea na hizi ni miongoni mwa tabiri hizo.
Kwa kifupi utabiri ni utaratibu wa kudadavua kitu ambacho aidha kinaweza kutokea au kisitokee kulinga na mazingira.
Taaluma hiyo ni ya kujifunza na mtu yeyote anaweza kujifunza akipenda.

Lakini hata hivyo umri nao unaweza kuchangia kiwango cha ufanisi kupungua na ndio sababu ya Sheikh Yahya kupoteza umaarufu, na ndio maana hata serikali kuweka umri wa waajiri wetu kustaafu, kutokana na kuchoka kiakili na kimwili. Hata hivyo hilo limeshindikana kutokana na watu wengi waliostaafu kutoka serikalini kukimbilia kwenye siasa. Inashangaza kidogo kwa kuwa kama mtu ameshindwa kwenye utumishi wa umma atawezaje uleta tija kwenye siasa.

Naona sasa ninachanganya mada, ngoja niishie hapa.

 
kwa mujibu wa vyanzo mbalmbali vya habari:

=aliwahi kutabiri vita dhidi ya nduli iddi amini, ikatokea
=aliwahi kutabiri moto kuwaka juu ya maji ikatokea kule goma drc
=aliwahi kutabiri mwanamuziki mwenye upara kufariki ghafla akiwa ******, utabiri huo ukamuangukia brenda fasi wa kule afrika ya kusini
=aliwahi kutabiri mwanmuziki maarufu kutoka nchi jirani aliyefungwa kuachiwa huru, wengi walidhani angekuwa ni babu seya, lakini utabiri huo ukamuangukia papa wemba wa kule drc aliyefungwa kule nchini ufaransa kutokana na kuingiza wahamiaji haramu kupitia bendi yake.
=aliwahi kutabiri rais wa awamu ya tatu mheshimiwa benjamini mkapa kuongezewa muda wa kuongoza nchi hata bada ya muda wake kuisha, wengi wakapiga kelele, lakini mwishowe ikatokea bada ya kifo cha mgombea mwenza wa chama kama sikosei tlp au chadema na uchaguzi ukasogezwa na hivyo rais wa wakati huo mheshimiwa mkapa akajikuta akiendelea kuongoza kwa muda zaidi ya kipindi chake, utabiri huo ulitimia.
=alitabiri kifo cha makamu wa rais hayati dr. Omari ali juma na utabiri huo ulitimia.

kwa kifupi zipo tabiri nyingi ambazo zilithibitishwa kutokea na hizi ni miongoni mwa tabiri hizo.
kwa kifupi utabiri ni utaratibu wa kudadavua kitu ambacho aidha kinaweza kutokea au kisitokee kulinga na mazingira.
taaluma hiyo ni ya kujifunza na mtu yeyote anaweza kujifunza akipenda.

lakini hata hivyo umri nao unaweza kuchangia kiwango cha ufanisi kupungua na ndio sababu ya sheikh yahya kupoteza umaarufu, na ndio maana hata serikali kuweka umri wa waajiri wetu kustaafu, kutokana na kuchoka kiakili na kimwili. Hata hivyo hilo limeshindikana kutokana na watu wengi waliostaafu kutoka serikalini kukimbilia kwenye siasa. Inashangaza kidogo kwa kuwa kama mtu ameshindwa kwenye utumishi wa umma atawezaje uleta tija kwenye siasa.

naona sasa ninachanganya mada, ngoja niishie hapa.


so what?
 
Suala ni je ana hitajika katika jamii? Utabiri unasaidia nini hasa ? Kufa mtu ni wajibu na sote tutakufa...nchi badala ya kusikiliza planners and other experts juu ya future wanamsikiliza huyu....mbona hjawahi kutabiri Dar kuwa na foleni mbaya?
 
Back
Top Bottom