Sheikh Ponda anaendelea kushikiliwa Polisi. Inasemekana yupo Kituo cha Magomeni

Leo nao wanatoa wa kwao, unaohusu mustakbali wa nchi na maslahi yao then serikali inamtia ndani msomaji tu wa Taarifa ya maimamu, kama hii siyo double standard ni kitu gani?
Bahati ya mwenzio usiilalie mlango wazi.

Kwahiyo unataka kuhalalisha makosa ya Ponda kwa kutumia makosa ya maaskofu?
Acha sheria ifuate mkondo wake.
 
Fair treatment kwa makundi yote ya jamii lazima iwepo.

Askofu wa Rulenge, Niwemugizi alitoa kauli ya kupinga kuwaachia watu kwenda kusali kwenye mijumuiko ya wengi kipindi cha korona alikamatwa?

TEC wametoa nyaraka za kutaka haki za watu na demokrasia viwepo nchini, umewahi kusikia wanawekwa ndani?

Walutheri nao walitoa waraka wao, kuna askofu alikamatwa?

Askofu Bagonza naye huwa anatoa misimamo kuhusu haki za raia umewahi kusikia anaitwa hata Central?

Gwajima anatoa kauli kuwa Wasukuma waungane wamsaidie msukuma mwenzao, umewahi kusikia akiwekwa ndani hata siku moja kwa uchochezi?

Waislamu siku zote hizo wako kimya, hawajatoa waraka hata mmoja

Leo nao wanatoa wa kwao, unaohusu mustakbali wa nchi na maslahi yao then serikali inamtia ndani msomaji tu wa Taarifa ya maimamu, kama hii siyo double standard ni kitu gani?

Serikali lazima iheshimu makundi yote ya kijamii siyo kundi moja inaheshimu viongozi wake na kundi jingine inakamata na kuweka ndani viongozi wake!

Leo hii kuna Masheikh kibao wako jela, hawajatibitika kuwa na kosa lolote mbele ya sheria lakini wako wanaozea jela!

Serikali hii imesamehe hadi wabakaji waliofungwa kifungo cha maisha lakini haiachii huru masheikh ambao imeshindwa kuthibitisha makosa yao mbele ya mkono wa sheria.

Acha maneno yako wewe, fikiria sana ksbla ya kucomment mitandaoni.

Waislamu hawapendi treatments za nsmna hii!
Ponda anaonewa. Ponda ana haki ya kunena dhidi ya yale anayoyaona hayaendi sawa.

Kuna mahali Waislam wanakosea. Wamegawanywa nao wakakubali kugawanyika. Hakuna namna yoyote ambaye viongozi wa dini ya kiislam watajihakikishia haki zaidi ya kuwa wamoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waislamu siyo waoga hata kidogo

Ni Waislamu waliomface Mkoloni kuanzia vita vya majimaji na hata kwenye harakati za kudai uhuru wao walikuwa msitari wa mbele.

Waislamu ni majasiri wa kumueleza mtawala ukweli, isipokuwa wana uungwana sana na subira sana.

Nakuhakikishia kundi pekee nchini ambalo likisema kuwa linaingia barabarani kudai haki yao katika nchi hii ni waislamu ndo wenye ujasiri huo. Na serikali inalijua hilo ndiyo maana siku zote imejitahidi kuwaweka masheikh wenye ushawishi kwenye "payroll" yake. Na BAKWATA ilianzishwa specifically ili kuwa "watchdog" wa waislamu, kwa sababu inawajua kuwa waislamu wakiamua lao huwezi kuwazuia.

Isipokuwa sasa serikali lazima iwatendee haki, isiabuse ukimya wao, hawa wana subira sana, lakini ikivuka mipaka, inakuwa inatengeneza bomu linalosubiri kupasuka!

Tusitengeneze Mwembechai nyingine!
Kuliko kuwa na mwembechai nyingine ni bora huyo Ponda arudishwe kwao unajua hawa majirani zetu watu wao wanatuletea matatizo sana angalia huyu ndugu yake wa ACT wazalendo matusi kejeli na kutishia watu kuwaroga
 
Mandela naye wajinga walimdharau hivihivi,kama huna uchungu na yanayoendele Tanzania utakuwa upande wa selikali,naamini wanaume wa kweli kwa karne hii ni Shekhe ponda na Tundu lissu,hawana uoga wala kuramba viatu vya mtu
 
Wacha amalize mwaka akitoka atakuwa amejifunza shughuli za kueneza dini na sio siasa.

‘Siasa bila dini ni uendawazimu’

Na Lilian Nyenza

Kanisa halitaacha kutoa mwongozo kwa watu wake hata kwa mambo ya kisiasa ukiwamo uchaguzi kwa kuwa, siasa bila dini ni sawa na uendawazimu.

Aidha, imedaiwa kuwa tabia ya kuwalaghai vijana kuwa ni taifa la kesho, ndiyo inayowadumaza kiakili na kuwafanya watumiwe na wanasiasa kufanya fujo, badala ya kujitokeza kuongoza kwa kufuata taratibu za nchi.

Mkurugenzi wa chama cha kifamilia cha Undugu Association Tanzania, Padri Baptiste Mapunda, alitoa kauli hiyo katika sherehe za kuuaga mwaka 2004 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2005, zilizofanyika katika ukumbi wa Parokia ya Mt. Yosefu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.

 
....Ponda ni mtu hatari kwa Taifa hili!


Huyu mtu wa usalama kwa taifa?? Unaweza kutuambia kesi yake ilienda vipi ??


PADRI AKAMATWA KWA UJANGILI HUKU BUNDUKI 48, RISASI 764 ZIKIKAMATWA





Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda, akionyesha bunduki aina ya AK47 kati ya silaha zilizokamatwa katika msako maalum wa ujangili.
Na Daniel Mbega, Namanyere

PADRI wa Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga (jina linahifadhiwa) ni miongoni mwa watu 50 waliokamatwa kwa ujangili na Kikosi Kazi cha Taifa katika Pori la Akiba la Lwafi wilayani Nkasi katika Mkoa wa Rukwa.
Padri aliyekamatwa ni wa Parokia ya Kirando katika mwambao wa Ziwa Tanganyika, ambaye bunduki yake aina ya Rifle yenye darubini inadaiwa kutumika katika ujangili ndani pori hilo la Lwafi wilayani humo.

Taarifa za kipolisi zimeeleza kwamba, mbali ya kukamatwa kwa watu hao, pia jeshi hilo limekamata bunduki 48 za aina mbalimbali ikiwemo ya Padri huyo anayoimiliki kihalali, pamoja na risasi 764 na maganda ya risasi 101.

Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Jacob Mwaruanda amesema kuwa baadhi ya waliokamatwa silaha zao wanazimiliki kihalali lakini zinatumika kinyume na utaratibu wa kumilikishwa kwao.

"Watu hawa bado wanahojiwa na upelelezi utakapokamilika watafikishwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake," alisema Kamanda Mwaruanda.
Kamanda Mwaruanda alisema kati ya bunduki 48 imo moja ya kivita aina ya AK47, bunduki 8 aina ya Rifle na risasi zake 83, Shortgun 19 na risasi zake 138, bastola 5 na risasi zake 133, magobore 15, magazine nne za bunduki aina ya Sub-Machine Gun, maganda matano ya bunduki aina ya Rifle, maganda 96 ya risasi za bunduki ya shortgun pamoja na vifaa vya kutengenezea bunduki za kienyeji na mitutu sita.

Watuhumiwa hao walikamatwa pia na nyara za serikali ambazo ni mikia sita ya tembo, nyama ya nyati kilo 20, miba ya nungunungu, ngozi moja ya paka-pori na pembe ya Nshya.



Kamanda Mwaruanda akifafanua jambo huku nyuma yake wanaonekana maofisa wa Kikosi Kazi cha Taifa pamoja na askari wa wanyamapori.

Kama Mwaruanda alitoa muda wa mwezi mmoja kuanzia sasa kwamba watu wanaomiliki silaha kinyume cha sheria kuzisalimisha mara moja kwenye vituo vya polisi au ofisi za serikali za vijiji kabla operesheni kabambe ya kuwatafuta watu hao haijaanza.

Rukwa na Katavi ni miongoni mwa maeneo ambayo ujangili kuua tembo umeshamiri sana hasa katika mapori ya akiba ya Lwafi na Hifadhi ya Taifa ya Katavi kutokana meno ya tembo kuonekana kuwa na soko katika mikoa mingine nchini na nchi jirani.


Kamanda Mwaruanda akionyesha kigudulia ambacho hutumiwa na majangili kubebea risasi.
Ofisa Mkuu wa Idara ya Ulinzi katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi, Davies Mushi alinukuliwa hivi karibuni kuwa kuwepo kwa soko zuri la biashara haramu ya nyara za Serikali hususan meno ya tembo ni moja ya sababu zinazochangia ongezeko la ujangili katika hifadhi hizo.

"Soko zuri la meno ya tembo lililopo katika mji wa Mpanda (Katavi), Sumbawanga (Rukwa), Tabora na maeneo mengine ya nchi linachangia sana kushamiri kwa ujangili ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Katavi, lakini tunajitahidi kufanya doria ndani ya hifadhi na kukabiliana na kasi hii iliyopo ya kuua tembo inayofanywa na majangili ambao wengi wao ni kutoka nje ya nchi," alisema Mushi.
 
Waislamu siyo waoga hata kidogo

Ni Waislamu waliomface Mkoloni kuanzia vita vya majimaji na hata kwenye harakati za kudai uhuru wao walikuwa msitari wa mbele.

Waislamu ni majasiri wa kumueleza mtawala ukweli, isipokuwa wana uungwana sana na subira sana.

Nakuhakikishia kundi pekee nchini ambalo likisema kuwa linaingia barabarani kudai haki yao katika nchi hii ni waislamu ndo wenye ujasiri huo. Na serikali inalijua hilo ndiyo maana siku zote imejitahidi kuwaweka masheikh wenye ushawishi kwenye "payroll" yake. Na BAKWATA ilianzishwa specifically ili kuwa "watchdog" wa waislamu, kwa sababu inawajua kuwa waislamu wakiamua lao huwezi kuwazuia.

Isipokuwa sasa serikali lazima iwatendee haki, isiabuse ukimya wao, hawa wana subira sana, lakini ikivuka mipaka, inakuwa inatengeneza bomu linalosubiri kupasuka!

Tusitengeneze Mwembechai nyingine!
Mkuu unazungumzia Waislamu WA Nchi gani?.. Tanzania hii ? Ni waoga KULIKO wanafanyiwa mangapi wameufyata?.. Wazee WA uamsho walipigwa kimya wafuasi wapo kimya hawajali wala nn!.. na How viongozi wao Hawaishi kugonha chears na vigogo.. zungumza Waislamu wa Palestina huko na Somalia Hao ndo Vidume,,Takbiriiiiii
 
Back
Top Bottom