tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Sheikh wa Mkoa wa Singida, Sheikh Issa Nassoro, amewataka viongozi wa dini nchini kuwa waaminifu na kuacha kutumia nafasi zao kuchochea taharuki au migogoro ya kisiasa, akibainisha kuwa baadhi yao wamekuwa wakihusika katika matukio ya udanganyifu ikiwemo kujiteka wao wenyewe kwa maslahi binafsi.
Akizungumza leo Oktoba 25, 2025 jijini Dodoma, katika kongamano la viongozi wa dini wa Kanda ya Kati (Dodoma na Singida) kuliombea taifa amani na utulivu kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, Sheikh Nassoro alisema ni muhimu viongozi wa dini kujitathmini na kusema ukweli ili kulinda heshima ya taasisi za kidini.
Soma pia: Sheikh Mustafa: Maandamano yao ni batili
“Viongozi wa dini tumekuwa ni chachu ya kuchochea baadhi ya mambo ya kisiasa yanayolalamikiwa katika nchi hii, ikiwemo suala la utekwaji wa watu. Ukweli ni kwamba baadhi yetu tumekuwa tukitumia nafasi hizi kujiteka sisi wenyewe kwa maslahi binafsi. Ni lazima tuambizane ukweli, maana ukweli siku zote humweka mtu huru,” amesema Sheikh Nassoro.
Ameongeza kuwa vitendo hivyo vimekuwa vikisababisha taharuki katika jamii, huku waumini wakihisi viongozi wao wametekwa, kumbe baadhi yao wameamua kuishi maisha tofauti kwa hiari yao binafsi.
Akizungumza leo Oktoba 25, 2025 jijini Dodoma, katika kongamano la viongozi wa dini wa Kanda ya Kati (Dodoma na Singida) kuliombea taifa amani na utulivu kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, Sheikh Nassoro alisema ni muhimu viongozi wa dini kujitathmini na kusema ukweli ili kulinda heshima ya taasisi za kidini.
Soma pia: Sheikh Mustafa: Maandamano yao ni batili
“Viongozi wa dini tumekuwa ni chachu ya kuchochea baadhi ya mambo ya kisiasa yanayolalamikiwa katika nchi hii, ikiwemo suala la utekwaji wa watu. Ukweli ni kwamba baadhi yetu tumekuwa tukitumia nafasi hizi kujiteka sisi wenyewe kwa maslahi binafsi. Ni lazima tuambizane ukweli, maana ukweli siku zote humweka mtu huru,” amesema Sheikh Nassoro.
Ameongeza kuwa vitendo hivyo vimekuwa vikisababisha taharuki katika jamii, huku waumini wakihisi viongozi wao wametekwa, kumbe baadhi yao wameamua kuishi maisha tofauti kwa hiari yao binafsi.