Sheikh Jongo bado ana mengi ya kujifunza

Sheikh Jongo bado ana mengi ya kujifunza

Status
Not open for further replies.
Kuna haja ya Sheikh Mohamed Said kuturithisha na kutufunza historia hii ya Tanzania Kabla na mpaka uhuru,binafsi nimeanza kufanya utafiti wangu wapi nitampata mwalimu huyu.bahati iliyoje nimeelekezwa mpaka kwake nikajaribu kuulizia majirani zake pale kariakoo nikaambiwa ni mtu mkarimu sana(wala simpambi) ndio ukweli niliokutana nao.Nikaja kujua kumbe aliwahi kuwa mfanyakazi wa Bandari pia,kwa Dar Es Salaam na Tanga.Sheikh Mohamed Said Allah akujaalie kheri nyingi duniani na kesho akhera.

David Webb,
Nakushukuru kwa maneno mazuri lakini kuna hadith sijui kama nitapata vizuri
inayosema kuwa endapo mmoja wenu atasifiwa kwa wema basi aseme dua hii
kuwa Allah nijaalie haya mabaya yangu uyaondoshe ambayo huyu ndugu yangu
hayajui.

Ahsante kwa dua nami naitika, ''Amin kwa sote.''
 
Mohamed Said
Hivi leo sheikh Jongo amekuwa sio sheikh kwasababu amekwenda kinyume na mitazamo yako??? Nadhani wewe sheikh una nafasi kubwa sana ya kumuona sheikh Jongo na kumuelimisha; nina uhakika sheikh Jongo haingii JF sasa huoni hili darsa litakuwa limepotea bure?? siku zote Bakwata imekuwa ndio taka la lawana lakini inashangaza sana kuona hadi leo mmeshindwa kuunda taasisi yenye nguvu ambayo itasimamia haki za waislamu; sheikh siku zinakwenda kilio hiki umekianza miaka mingi sana sasa nadhani huu ni wakti mauafaka wa kupata majibu ya kilio chako; maana hata ikija Chadema madarakani (Mungu aupushe mbali balaa hilo) yatakuwa ni yaleyale maana zamani tulikuwa tunasikia tunaonewa kwasababu hatuna raisi muislamu sasa mmebadili maneno tu lakini mdundo ni uleule. Nakutakia afya njema Mola aendelee kukupa wingi hakima na bausara na pale penye mapungufu ayaondoe. Amen

Chama,
Kuna baadhi ya mambo umepatia na mengine kwa uoni wangu umekosea.

Sijapatapo kusema Jongo kaacha kuwa sheikh.

Kuhusu kumuelimisha Sheikh Jongo ndiyo huku nimeeleza historia ya masheikh
waliojipendekeza na nini ulikuwa mwisho wao na hao niliowataja ni baadhi tu.

Haya yote niliyoandika yashamfikia wala usiwe na wasiwasi kuhusu hilo.

Ama kuhusu ''kilio'' hakuna anaelia.

Nimeandika historia ya Waislam katika Tanganyika na leo wale waliokuwa na
fikra kuwa hii ni nchi ya Kikristo wamebadili fikra zao.

Nadhani unalikumbuka sakata na sensa na kwa nini Waislam waligoma kushiriki

Wanachojua ni kuwa Tanganyika si nchi ya Kikristo ila Wakristo wamehodhi
fursa kwa wingi takriban fursa zote.

Haya ndiyo majibu ya juhudi zangu.
Namshukuru sana Allah kwa haya.

Hilo la kuunda taasisi yenye ''nguvu'' sijui una maana gani unaposema ''nguvu.''

Waislam tunazo taasisi nyingi zilizodhahiri na zisizo dhahiri na ndiyo maana hadi
leo unashuhudia Uislam una nguvu nchini kila kukicha umma unasonga mbele juu
ya vikwazo tulivyowekewa.

Wala hujasikia Waislam wanatoka kwenye dini yao kwa ajili ya shida.

Hilo la rais Muislam na sisi kubadili ''mdundo''sijui umelitoa wapi.

Nakushukuru kwa dua.
Amin kwa sote.
 
Mohamed Said
Hivi leo sheikh Jongo amekuwa sio sheikh kwasababu amekwenda kinyume na mitazamo yako??? Nadhani wewe sheikh una nafasi kubwa sana ya kumuona sheikh Jongo na kumuelimisha; nina uhakika sheikh Jongo haingii JF sasa huoni hili darsa litakuwa limepotea bure?? siku zote Bakwata imekuwa ndio taka la lawana lakini inashangaza sana kuona hadi leo mmeshindwa kuunda taasisi yenye nguvu ambayo itasimamia haki za waislamu; sheikh siku zinakwenda kilio hiki umekianza miaka mingi sana sasa nadhani huu ni wakti mauafaka wa kupata majibu ya kilio chako; maana hata ikija Chadema madarakani (Mungu aupushe mbali balaa hilo) yatakuwa ni yaleyale maana zamani tulikuwa tunasikia tunaonewa kwasababu hatuna raisi muislamu sasa mmebadili maneno tu lakini mdundo ni uleule. Nakutakia afya njema Mola aendelee kukupa wingi hakima na bausara na pale penye mapungufu ayaondoe. Amen


Chama nimekusoma hata namimi.

Ila tatizo la watu kama Jongo ni unafiki na kuendekeza njaaa

Ukweli wanaujua ila wanauuza for the sake of matumbo yao.
 
Mwalimu Wangu Moh Said nitaomba hiki kisa unitumie kwenye mail yangu najua unayo nitaiprint andiko hili na kusambaza kwa wamakonde wenzangu wapate kuujua uhalisia...

Ili haki na batili vipate kufahamika ma kujitenga.

Shukran sana.
 
hakuwa tu anampandisha Nyerere kwenye daraja isiyoweza kufikiwa na kiumbe chochote, lakini lililo baya zaidi, alikuwa akitoa kauli hiyo kwa Mkristo...
... na huo 'ubaya' ndio hasa msingi wa thread yako hii. Hivi wastani wa umri wa maisha ya mtanzania ni miaka mingapi jamani ili tupishane kidogo?
 
Al akh mzee mohammad nimefaidika mengi sana sababu mmoja wa wahanga ni babu yangu nae alujipendekeza mpaka kutoa na nyumba mtaa wa mkunguni na skuma yaliompata 1967 yalimtoa roho yake

Alifilisiwa tena kwa kutajwa jina
 
soga, simulizi, porojo za barabarani kibao!!

Ungezijuwa?

Mwache Al Alama Mohamed Said atiririke tupo wengi yanatugusa sana haya anayoyaandika.

Hivi wewe huoni anatajwa Augustine Mrema hapo? hivi hukumsikia William Lukuvi alivyoenda kujitetea BMK alimsifia sana Mrema mpaka akamwambia sasa atahakikisha mafao yake yanashugulikiwa? Hivi unafikiri ule ujumbe wa William Lukuvi ulikuwa kwa Mrema pekee? Jiulize, mafao ya Mrema na Katiba mpya yana uhusiano upi?

Mwenye masikio haambiwi sikia.
 
Last edited by a moderator:
David Webb,
Nakushukuru kwa maneno mazuri lakini kuna hadith sijui kama nitapata vizuri
inayosema kuwa endapo mmoja wenu atasifiwa kwa wema basi aseme dua hii
kuwa Allah nijaalie haya mabaya yangu uyaondoshe ambayo huyu ndugu yangu
hayajui.

Ahsante kwa dua nami naitika, ''Amin kwa sote.''

No offense or disrespect intended, ila katika simulizi zako zote sijapata kuona solution dhidi ya matatizo tuliyo nayo collectively kama nchi, achilia mbali hisia za malalamiko ya waislamu kutengwa. Sijapata kuona ukiongelea Tanzania kama nchi tunawezaje kufanya mabadiliko ya status quo ili kuboresha maisha yetu, unless uniambie huko interested na collective well being ya watanzania wote.
 
No offense or disrespect intended, ila katika simulizi zako zote sijapata kuona solution dhidi ya matatizo tuliyo nayo collectively kama nchi, achilia mbali hisia za malalamiko ya waislamu kutengwa. Sijapata kuona ukiongelea Tanzania kama nchi tunawezaje kufanya mabadiliko ya status quo ili kuboresha maisha yetu, unless uniambie huko interested na collective well being ya watanzania wote.

Ibambasi,
Waliokuwa madarakani hawakubali kama kuna ubaguzi.

Inabidi kwanza walikubali tatizo ndipo kisha tunaweza kupanda ngazi ya pili.
Soma historia zote za mapambano ya karibu soma historia ya Mandela na ANC.

You cant jump the gun.
 
soga, simulizi, porojo za barabarani kibao!!

Mwamikili,
Hapana sio soga hayo yote niloandika yalitendeka.

Labda kwa kuwa wazee wako walikuwa nje ya harakati hizi ndiyo maana
zinakuchoma moyo.

Mimi na wenzangu wengi sana tunatembea kifua mbele kwa historia hii.
 
Duuh...ndio maana naamini Nyerere was ahead of his time....mpaka leo ndio mjanja wetu hata kama hatupendi. Ukiona bado tunasumbuka naye hata baada ya kufa miaka 14 iliyopita definitely he was a revered figure....Habari ndio hiyo

Na kila jambo likitaka kukwama, tutatumia jina lake kujaribu kurekebisha mambo! Iwe kwa nia njema au ovu! Huyo ndio Nyerere, kiongozi wa kweli wa Tanzania hii.
 
Ya kina jongo na simba ndio kama haya ....waso haya
 

Attachments

  • 1398934868942.jpg
    1398934868942.jpg
    17.2 KB · Views: 2,724
Al akh mzee mohammad nimefaidika mengi sana sababu mmoja wa wahanga ni babu yangu nae alujipendekeza mpaka kutoa na nyumba mtaa wa mkunguni na skuma yaliompata 1967 yalimtoa roho yake

Alifilisiwa tena kwa kutajwa jina

Salmar,
Mkunguni na Sukuma.

Pale kulikuwa na chuo cha Shariff Abdulrahman kisha mbele kidogo kulia
kama unaelekea Mtaa wa Mafia ilikuwa club ya Young Africans..

Chuo cha Shariff Abdulrahman kilikuwa kinatazamana na nyumba ya akina
Kaka Said Hamza na Dada Tatu Hamza, Jaffari Hamza, Ghalib ''Guy''
Hamza, Hamidu Hamza
na Mwashamba Hamza wengi katika ndugu hawa
wametangulia mbele ya haki...

Nyumba yenu pale ni ipi?
 
Duuh...ndio maana naamini Nyerere was ahead of his time....mpaka leo ndio mjanja wetu hata kama hatupendi. Ukiona bado tunasumbuka naye hata baada ya kufa miaka 14 iliyopita definitely he was a revered figure....Habari ndio hiyo

Na kila jambo likitaka kukwama, tutatumia jina lake kujaribu kurekebisha mambo! Iwe kwa nia njema au ovu! Huyo ndio Nyerere, kiongozi wa kweli wa Tanzania hii.

Ndahani,
Naamini unajua nani anatajwa kila wanapoikumbuka Auschwitz.

Vipi na huyo umemtia katika orodha yako?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom