Subhana Allah!!!!analia kisa na mkasa waasisi wametukwanwa???mtume wake ametukanwa mara ngapi??na je amewahi lia???Allah(SW) ametukanwa mara ngapi???amewahi lia???amepigigwa risasi shekh Ponda amewahi li???amefungwa Shekh Mselem Ally ameliaaa????angelia basi hata ilivyozama MV Spice kama kweli ana huruma na imani kiasi hiko....Amuogope Mungu ataumbuka bure
Sheikh Idriss,
Mashekh wa BAKWATA hakika wana mambo sana.
Kuna kitu kinaitwa ''theatrics,'' masheikh wa BAKWATA ni mabingwa na wana
medali za dhahabu.
Sheikh Mkuu wa BAKWATA Shaaban Simba aliwahi kutoa medali kumpa
Reginald Mengi kwa utumishi wake uliotukuka kwa Waislam.
Hakika umma ulipigwa na butwaa.
Umma ukajiuliza.
Sheikh Shaaban Simba hajapata kumsikia
Sheikh Hassan bin Amir bingwa
wa tafsir ya Qur'an na aliyeandika vitabu lukuki mpaka akapewa shahada ya
heshima na Al Azhar, Cairo mwaka 1964?
Ukiachia sifa yake ya kupigania uhuru wa Tanganyika nk. nk.
Sheikh Shaaban Simba hajamsikia
Sheikh Mohamed Ayub aliyesomesha
dini maisha yake yote na ana wanafunzi Afrika ya Mashariki nzima na hao
wote wanafunzi wake wana vyuo wanaisomesha Qur'an?
Sheikh Shaaban Simba hawa wote hakuwaona ila kamuona Reginald Mengi?
Sasa hili la kulia
Sheikh Jongo ni mlolongo tu wa hizo ''theatrics'' za masheikh
wa BAKWATA.
Sheikh Shaaban Simba hivi kweli hajapatapo hata siku moja kumsikia
Sheikh
Aboud Maalim aliyejenga misikiti chungu mzima kwa kuwahamasisha Waislam
matajiri na masikini wachangie ujenzi kila mtu kwa uwezo wake alojaaliwa na
Allah?
Sheikh Aboud Maalim akaweza kujenga Msikiti wa Manyema, Msikiti wa Ngazija,
Msikiti wa Maamur, Msikiti wa Mwinjuma Mwinyikambi na mingine tusiyoijua.
Achilia mbali kuanzisha scholarship kwa vijana wa Kiislam kusoma Udaktari na
Uhandisi Uturuki chini ya taasisi aliyoanzisha, Tanzania Muslim Trust Fund.
Kwa wasiowajua masheikh wa BAKWATA hakika wanapata tabu.
Kwa wanowajua masheikh wa BAKWATA hawashangazwi.
Wakati mwingine hakika huwa vioja na vichekesho khasa.
Kuna msemo wa Kiarabu unaosema,''Sababu ikijulikana ajabu huondoka.''
Naamini
Sheikh Jongo anaujua msemo huu.