Sijala kitu chochote kwa sababu hiyo nyumba haikaliwi na mtu lakini hata kama ningeletewa chakula nisingekula kwa sababu siwezi kuwaamini kula chakula chao kwa hivyo nilichokuwa nafanya nikienda chooni kujisaidia ndio nakunywa maji ya mferejini kwa wingi sana na Alhamdulillah (nashukuru Mungu) amenisaidia, aliongeza Sheikh huyo ambaye alikuwa amezongwa na umati mkubwa hapo nyumbani kwake. sikuwa naona kitu chochote kwa kuwa alikuwa amefunikwa uso wote,Kwa kweli nazungumza neno kutoweka lakini mimi sikutekwa bali nilichukuliwa na watu ambao ni polisi na wakaniingiza katika gari na kunipeleka sehemu moja ambayo mimi nilikuwa siijui wakanifunga kitambaa machoni na kunipeleka sehemu nisiyoifahamu na kuniingiza katika nyumba yenye geti nikiwa na kitambaa cheusi usoni,