Kwanza pongezi kwa kumkubali mtoto. Kinachonishangaza lakini ni kuwa tangu mtoto amezaliwa na kufikia umri huo hamkuwahi kushirikiana naye katika tendo la ndoa. Ulitunza mtoto, lakini uliishi kivyako naye kivyake. Sasa leo unataka kufunga ndoa kwa nini awe mbogo wakati uhusiano wa mapenzi ulishavunjia zaidi ya miaka 3? Ni ajabu hii! Au unatufunga kamba uliendelea kufaidi!?Huyu binti ni 'mchaga'
Huyu binti,alijifungua mtoto a kike,mtoto sasa ni mkubwa kwa 3yrs,sasa imefika mahala nahitaji kuendelea na maisha yangu AMEKUWA MBOGO
Sikuwahi kuishi nae,na wala kushirikiana nae baada ya ile mimba.Na sikuwahi kutoa ahadi za ndoa pale,lakini AMEKUWA MKALI nilipomwambia sasa ninaendelea na maisha yangu nina mchumba na ninahitaji kuoa.
Amenitishia kuniletea vurugu ofisini,sasa mimi inanisumbua kichwa.ilifika mahala nilitamani nihame dar.
TAFADHALI
Kama unayoyasema ni kweli, basi ujue hata kama mzazi mwenzako anang'aka si kwa sababu anakupenda kwani mlishaachana siku nyingi. Ana wivu wa kimaslahi - anataka pesa/mali yako, uendelee kumhudumia yeye na mtoto wenu. Ukioa anaona mali yote atakumbatia mkeo.
Sasa ufanyeje? NENDA kafunge ndoa yako na umpendaye kwa moyo wa dhati. Hata akileta fujo hatafanikiwa kukuzuia kufunga ndoa kwani ni haki yako msingi. Sheria inakulinda.
Ila mtoto usimtelekeze. Endelea kumtunza kama mwanzo. Hapo unawajibika. Vinginevyo utachukuliwa hatua.