She is having my baby, I can't get married to her!

Teamo

JF-Expert Member
Jan 9, 2009
12,272
1,034
Huyu binti ni 'mchaga'

Huyu binti katika ujana ujana ule ilitokea akaconceive

Huyu binti alitaka kutoa mimba nikamsihi sana asifane hiyo dhambi,nilimwahidi kwamba nitamlea mtoto,HILO TU!

Huyu binti,alijifungua mtoto a kike,mtoto sasa ni mkubwa kwa 3yrs,sasa imefika mahala nahitaji kuendelea na maisha yangu AMEKUWA MBOGO

Sikuwahi kuishi nae,na wala kushirikiana nae baada ya ile mimba.Na sikuwahi kutoa ahadi za ndoa pale,lakini AMEKUWA MKALI nilipomwambia sasa ninaendelea na maisha yangu nina mchumba na ninahitaji kuoa.

Amenitishia kuniletea vurugu ofisini,sasa mimi inanisumbua kichwa.ilifika mahala nilitamani nihame dar.

Najua nilikosea,lakini pia sio rahisi kulazimisha kuishi na mtu ambae humpendi,kwa sababu sitakuwa mwaminifu kwake,na hata akilazimisha tutakaa nusu mwaka tu then tutaachana.

waungwana mnisaidie nimweleweshe vipi huyu mzazi mwenzangu kwamba mapenzi hayalazimishwi?

TAFADHALI
 
sasa wewe unamharibia maisha huyu mdada na kumwacha tu hivi hivi? Wewe unadhani sasa nani atamwoa huyu dada wakati ni wewe umemzalisha?

Isitoshe tayari ameshakuzalia mtoto mzuri!

Basi mfungulie mradi mkubwa au mpe pesa ya kutosha atulie!
Kikubwa mbembeleze kwa akili..na taratibu!

Zamani ukimbebesha binti mimba ni lazima unamwoa..hata kama hampendi..mtapendana mbele kwa mbele!
 
Basi mfungulie mradi mkubwa au mpe pesa ya kutosha atulie!
Kikubwa mbembeleze kwa akili..na taratibu!!
HILI NAWEZA KULIFANYA!na tulikubaliana hivyo,lakini sasa naona amenibadilikia

Zamani ukimbebesha binti mimba ni lazima unamwoa..hata kama hampendi..mtapendana mbele kwa mbele!
sasa hili kaka ni gumu,na zamani walitumia huo ubabe kwasababu mtu alikuwa anaweza kuoa wake hata kumi akitaka.sasa hivi kuna UKIMWI
 
Huyu binti ni 'mchaga'

Najua nilikosea,lakini pia sio rahisi kulazimisha kuishi na mtu ambae humpendi,kwa sababu sitakuwa mwaminifu kwake,na hata akilazimisha tutakaa nusu mwaka tu then tutaachana.

waungwana mnisaidie nimweleweshe vipi huyu mzazi mwenzangu kwamba mapenzi hayalazimishwi?

TAFADHALI

Kulazimwisha kivipi kwani hiyo mimba ilitunga vipi kama mlikuwa hampendani?? Ikiwa kama ulikuwa humpendi basi wewe ni mbakaji maana hadi mimba itunge ni kwamba ulikuwa unampenda kwa dhati na hukujali kutumia condom, sasa kwanini sasa useme humpendi???

Unajua wewe ni mtu mzima unajua jinsi ya kujikinga sio tu na mimba hata magonjwa ya zinaa sasa kanini ufanye bila kondom.
Huyu binti anahaki kabisa ya kuolewa na wewe mlipendana now unamwona si mali kitu unataka kumtosa. Kwanza unatakiwa umshukuru na kumweshimu maana bila yeye usingeonekana ni rijali na unauzazi ,kwa maoni yangu kumwoa na kuishi nae ni wajibu wako.
Nyie ndio mnao ongeza idadi ya watoto wa mitaani duniani,jambo jingine geuza upande wapili ungekuwa ww umefanyiwa hivyo ungejisikia vipi. tatu angekuw mwanao ama dada yako kafanyiwa hivyo unefurahia!

Ukipata majibu ya maswali nilio kuuliza utajua uchungu alionao huyo dada.
NENDA KAMUOWE ACHA KUONGEZA IDADI YA WATOTO MITAANI NA WSIO NA MALEZI YA PANDE MBILI.
 
huyu ni mchaga wa rombo-tarakea
lol sasa mkuu wakati unailowesha mule ndani ulijua hawezi kuwa mkeo? una test zali kavu kavu?
kwa sasa huwezi kumuoa kwanini? kawa mbaya kitabia,kisura au vipi?
 
mchaga wa wapi? ili nikupe njia ya kudeal nae

Sio mchaga tu hata angekuwa mjaluo ana haki kwanini umzalishe alafu umtelekeze??
Ushauri unatakiwa kumpa ni kujenga familia yake alio ianza maana mpaka wanapeana mimba wameanzia mbali hao wanapendana wasituzinguwe!
 
naweza kusema mtu unaweza kutembea na mtu na ujampenda, ile onja onja ndio imemfikisha kijana huku, ishu ni kwamba kwanini hukutumia zana na ulijua huna future nae? kuoa/kuolewa bila mtu kuridhia nayo ina cost sana mana utaona nyumba kama gereza, kaa nae chini mweleweshe mambo vizuri na kama mmoja alivyokuambia mfungulie mradi wa yeye kujikimu na maisha yake, na mtoto ndio umtunze wewe...
 
Wewe ndugu kama ulithubutu kulala naye bila ya kutumia Condom katika kipindi hiki cha hatari ya gonjwa la ukimwi pamoja na magonjwa mengine ya zinaa, basi ulikuwa unampenda sana. Mimi namwuunga mkono huyo dada wa kichaga kwa kukung'ang'ani na nakushauri ufanye haraka mpango wa kuoana naye ili mlee tunda la penzi lenu, yaani mtoto wenu
 
Huwezi kulazimisha ndoa. Thats simple. NA NADHANI NI KUKOSA uelewa kusema kwamba jamaa kamuharibia maisha binti. Does it mean bila huyu jamaa kumuoa huyu dada maisha yake ndo yamefika mwisho? c`on people tuwe serious. Binti bado anaweza kuendelea na maisha yake. Otherwise mi hii naiona issue kama ya kumdhalilisha mwanamke..kwamba hawezi kujisimamia na maisha yake mpaka jamaa amuoe.

Cha kufanya muite mdada mueleweshe kwamba utatake responsibility ya mwanao fully! vinginevyo..hata ukimuoa hiyo itakuwa ni karaha tupu..mwanamke ataishi kwa machungu...na naamini hata wewe utakuwa na nyumba ndogo..which is worse than her doing her own things..

It takes two to play the game..sasa sioni kwanini ionekane kwamba jamaa kamharibia maisha msichana...she can as well be a single mama and happy! Furaha si lazima uoelwe au uoe..Every persona has the right to be happy..and if happiness means living with a different person..so be it.
 
Pole aaaa lakini nakupa pole ya nini? usimfanyie mwenzako mambo usiyotaka kufanyiwa,hivi ingekuwa ni wewe ungejisikiaje kufanyiwa hayo unayotaka kumfanyia?Yawezekana ulimwambia utamwoa na ameshajua kuwa huna mpango nae na ndo maana amekomalia hilo,hata ingekuwa ni mimi nisingekubali,unizalishe halafu ukaoe kwingine inaingia kweli akilini hiyo?Hivi kwa nini mnapenda sana kututenda? Kaa tafakari kwa kina kwamba ni haki na ni sawa hayo unayotaka kuyafanya?
 
pole kwa mkasa mkuu
kwa ujasiri ulionyesha kwa binti huyo moja kusababisha ujauzito na kumshauri asichomoe lo!na sita kukueleza ukweli.sijaona sababu ya msingi kwanini usimuoe.
 
Jamani ndoa hailazimishwi, kumbukeni ndoa ni kitanzi cha maisha hasa kwa wakristo. Pengine ni kweli alikuwa anampenda hadi akafikia hatua ya kumpa ujauzito na sasa kuna babygirl lakini jamani huyu kaka ana akili timamu pengine ktk kuendel;ea na huo uhusiano ameona kuna kasoro ambazo kama kweli atamuoa huyo dada atakuwa ameingia kwenye shida.

Nakushauri mwite huyo dada zungumza nae kwa upole kabisa kwamba umeshindwa kumuoa kwa sababu zipi. Pia umahakikishie kuwa utakuwa full responsible ktk matunzo ya mtoto na yeye usimwache hivihivi mfungulie hata biashara ili ajiingizie kipato.

Hata hivyo wachaga wa Rombo ni wakorofi sana, kila la heri bro!
 
Kwa nini ulilala naye bila kinga kama ulijua hutaweza kumuoa,
Nadhani hata huyo dada siyo anakung'ang'ania kwa sababu anakupenda, ni kwa sababu ya mtoto, hataki mtoto wake alelewe na mama wa kambo na wala baba wa kambo, hata kama utamtunza mtoto, bado anahitaji mapenzi ya wazazi wake aishi nao wote.
Hata ukimfungulia biashara haisaidii nia yake ni muishi pamoja mlee mtot wenu, hata wewe una makosa na sidhani kama kipindi cha uhusiano wenu ulikuwa unampenda kweli? au ulikuwa unapitapita tu, halafu unajua hii tabia inarithi sasa utakuja kuona hata huyo binti yako mdogo na yeye akikua atazalishwa na ataachwa, halafu kama mzazi uone utakavyosikia.
tayari una maamuzi yako moyoni hata tukikuambia huwezi kubadilika, lakini mrombo lazima ulijue jiji.
 
Mtu unapoanzisha thread ukiulizwa maswali jibu ili uweze kushauriwa kirahisi naona umejibu maswali ya mwanzo tu,mengine umechuna.
Kaka Geoff,kuna post kibao zina maswali yako plz hebu yajibu.
 
nashukuru kwa ushauri jamani
nitaanza kujibu maswali sasa
 
jamani mnanishutumu kwa kutotumia zana!?

inawezekana ni udhaifu wangu,au niseme ndio kosa kubwa la kwangu!

Sasa mimi kuishi nae kwakweli ni kunilazimisha!because I DON'T LOVE HER FROM MY HEART,ilikuwa ni katika kukata kiu hapa na pale
 
Huyu binti ni 'mchaga'

Huyu binti katika ujana ujana ule ilitokea akaconceive

Huyu binti alitaka kutoa mimba nikamsihi sana asifane hiyo dhambi,nilimwahidi kwamba nitamlea mtoto,HILO TU!

Huyu binti,alijifungua mtoto a kike,mtoto sasa ni mkubwa kwa 3yrs,sasa imefika mahala nahitaji kuendelea na maisha yangu AMEKUWA MBOGO

Sikuwahi kuishi nae,na wala kushirikiana nae baada ya ile mimba.Na sikuwahi kutoa ahadi za ndoa pale,lakini AMEKUWA MKALI nilipomwambia sasa ninaendelea na maisha yangu nina mchumba na ninahitaji kuoa.

Amenitishia kuniletea vurugu ofisini,sasa mimi inanisumbua kichwa.ilifika mahala nilitamani nihame dar.

Najua nilikosea,lakini pia sio rahisi kulazimisha kuishi na mtu ambae humpendi,kwa sababu sitakuwa mwaminifu kwake,na hata akilazimisha tutakaa nusu mwaka tu then tutaachana.

waungwana mnisaidie nimweleweshe vipi huyu mzazi mwenzangu kwamba mapenzi hayalazimishwi?

TAFADHALI

Inawezekana ulimuahidi future yenu together wakati mpo hot in love halafu sasa anaona umebadilika unamuacha azeeke mwenyewe. Kama kweli hukuwa na nia nae zaidi ya kuwa wazazi wenza tu, sidhani kama angekusumbua hivyo mpaka leo hii. Lakini kwa nini unamuacha mama wa mtoto wako solemba? Je unamjalije kama mzazi mwenzio?
Tatizo kubwa mzazi mwenzio alikuwa au amekuweka plan A wakati wewe umemuona yeye ni plan B. Nadhani baada ya nyie kubarikiwa mtoto (hata kama hamkupanga), alijua ndo tayari mtakuwa familia yaani umuoe.
 
Yaani katika kitu ambacho sipendagi kukisikia ni kitu kama hiki cha kwako Geoff. Hebu imagine huyo dada angekuwa dada ako au mdogo wako wa kike ungejiskiaje. Huyo dada anakupenda ndio maana amekuwekea ngumu mpaka kichwa kinakuuma. Nampa huyo mchumba wako tahadhari manake nae akishika mimba yako (maana inaelekea condom kwako ni proverb) utamfanyia hivo hivo. Muone huyo mchaga nakuhakikishia you will not regret.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom