Shamba-dimbwi linauzwa

Shamba-dimbwi linauzwa

Malila

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2007
Posts
5,395
Reaction score
5,211
Habari,

Katika kijiji cha Buyuni, kata ya Vigwaza kuna madimbwi makubwa mawili, dimbwi moja lina ukubwa wa eka 12.5, na dimbwi la pili ni kubwa sana, ni eka 39.0 (hapa tulipima nusu ya dimbwi). Madimbwi yote yana maji yenye samaki jamii ya perege, kitoga na kambale. Nimewaona hao samaki wakati nayapima haya madimbwi.

Maeneo yanayozunguka haya madimbwi yanauzwa Tsh 350,000/ kwa eka moja. Hili dimbwi kubwa linakaa na maji mpaka msimu mwingine wa mvua kama hakuna ukame, linafaa kwa wanaotaka kufuga kwa scale kubwa, maana maji yapo ya kutosha. Hili dimbwi dogo pia lafaa kwa ufugaji,ila maji yake kina ni kifupi, ila ardhi yake ina rutuba sana. Buyuni kuna wakulima na wafugaji, kijiji kimetenga maeneo ya wafugaji.

Ni km 9 toka barabara kuu pale Vigwaza, na kutoka kijijini center mpaka dimbwi kubwa lilipo ni km 3. Nchi ina uoto wa asili mzuri, ni kijani sehemu kubwa ya mwaka.

Kwa anayehitaji shamba-dimbwi kwa ufugaji na kilimo cha nafaka, basi tuwasiliane.
 
bei gani hayo madimbwi

Dimbwi hili dogo lenye ujumla wa eka 12.5pamoja na nchi kavu wanauza Tsh 350,000/ kw eka. Hili kubwa pia bei ni hiyo hiyo ila inabidi ununue na nchi kavu ili upate pa kujenga. Ukinunua dimbwi lote eka 39, makazi utajenga wapi?
 
mkuu nitakupm maana unaongeaga vitu vya maana na umenisaidiaga sana wakati Fulani hivi nilikuwa nahitaji mbuzi.Ok by the way madimbwi si huwa mali ya umma maana kuna sehemu wanaita Mawamba mawili hapo mbezi kuna mabwawa ya asili limeandikwa hii ni sehemu ya umma.
 
mkuu nitakupm maana unaongeaga vitu vya maana na umenisaidiaga sana wakati Fulani hivi nilikuwa nahitaji mbuzi.Ok by the way madimbwi si huwa mali ya umma maana kuna sehemu wanaita Mawamba mawili hapo mbezi kuna mabwawa ya asili limeandikwa hii ni sehemu ya umma.

Hili dogo linakuwa ndani ya shamba lako, hili kubwa unatakiwa kununua kando ili ulifanye beach.

Mkuu, tumekosa hela tu, lile dimbwi kubwa kama una mkwanja,unaliandikia paper ya Ukweli ili upate kibali cha kulitunza,ndani ya mwaka mmoja unatoka.
 
Hili dogo linakuwa ndani ya shamba lako, hili kubwa unatakiwa kununua kando ili ulifanye beach.

Mkuu, tumekosa hela tu, lile dimbwi kubwa kama una mkwanja,unaliandikia paper ya Ukweli ili upate kibali cha kulitunza,ndani ya mwaka mmoja unatoka.

mkuu nimekupata itakucheki kwenye simu jioni mkuu shukrani sana na Ubarikiwe mkuu
 
Back
Top Bottom