SEHEMU YA NUKUU ZA HOTUBA YA KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA ITIKADI NA UENEZI SHAKA HAMDU SHAKA KATIKA SHEREHE YA MAULID MADRASAT NURUU TEMEKE MWISHO DSM
"Nitoe wito kwa viongozi wa dini nchini kuwa mstari wa mbele katika kuelekeza jamii mambo mema, ikiwepo kupinga na kukemea vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa kujenga uelewa kwa waumini wao" - Shaka Mwenezi Taifa
"Viongozi wa dini wamekuwa wakisaidi katika kuhamasisha umoja, amani na mshikamano wa taifa jambo ambalo limefanikiwa sana" - Shaka Mwenezi Taifa
"Niwaombe viongozi wa dini kuendelea kusukuma ajenda ya kutokomeza ukatili wa kijinsia nchini ili Taifa letu likawe mfano duniani kote kwa kuamini kuwa imani zote zinapingana na vitendo hivyo ambavyo kwa namna moja ama nyingine vinadhalilisha utu wa mtu'' - Shaka Mwenezi Taifa
"Viongozi wa dini ni kundi muhimu katika mapambano dhidi ya kutokomeza ukatili wa kijinsia hususani kwa wanawake na wasichana kwani wao ni kimbilio la jamii kwakuwa wanaaminika, hivyo ni lazima kutumia uaminifu huo kusaidia mema na si kuwa miongoni mwa wanaoshiriki kufanya ukatili wa kijinsia" - Shaka Mwenezi Taifa
"Matukio ya wanawake na wasichana kubakwa, kupigwa, kudhalilishwa, kunyanyaswa, kunyimwa haki ya kumiliki mali na mengine yo ni mambo ambayo sote kwa umoja wetu tunapaswa kuyapiga vita kwa nguvu zetu zote bila kujali itikadi zetu kwa namna yoyote" - Shaka Mwenezi Taifa
"Ni dhambi na fedheha jamii kushiriki vitendo vya ukatili wa kijinsia katika dunia ya leo inayohimiza maendeleo jumuishi, yenye usawa na endelevu ambapo hata maandiko matakatifu yanapinga kadhia hiyo" - Shaka Mwenezi Taifa
"Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa akitoa wito Mara kwa jamii kuchukua wajibu wa kuwa mstari wa mbele kupinga na kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia ili kuwapa wanawake na wasichana mazingira huru, yenye usalama, usawa, amani na furaha kwao kushiriki katika maendeleo" -Shaka Mwenezi Taifa
"Nitoe wito kwa viongozi wa dini nchini kuwa mstari wa mbele katika kuelekeza jamii mambo mema, ikiwepo kupinga na kukemea vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa kujenga uelewa kwa waumini wao" - Shaka Mwenezi Taifa
"Viongozi wa dini wamekuwa wakisaidi katika kuhamasisha umoja, amani na mshikamano wa taifa jambo ambalo limefanikiwa sana" - Shaka Mwenezi Taifa
"Niwaombe viongozi wa dini kuendelea kusukuma ajenda ya kutokomeza ukatili wa kijinsia nchini ili Taifa letu likawe mfano duniani kote kwa kuamini kuwa imani zote zinapingana na vitendo hivyo ambavyo kwa namna moja ama nyingine vinadhalilisha utu wa mtu'' - Shaka Mwenezi Taifa
"Viongozi wa dini ni kundi muhimu katika mapambano dhidi ya kutokomeza ukatili wa kijinsia hususani kwa wanawake na wasichana kwani wao ni kimbilio la jamii kwakuwa wanaaminika, hivyo ni lazima kutumia uaminifu huo kusaidia mema na si kuwa miongoni mwa wanaoshiriki kufanya ukatili wa kijinsia" - Shaka Mwenezi Taifa
"Matukio ya wanawake na wasichana kubakwa, kupigwa, kudhalilishwa, kunyanyaswa, kunyimwa haki ya kumiliki mali na mengine yo ni mambo ambayo sote kwa umoja wetu tunapaswa kuyapiga vita kwa nguvu zetu zote bila kujali itikadi zetu kwa namna yoyote" - Shaka Mwenezi Taifa
"Ni dhambi na fedheha jamii kushiriki vitendo vya ukatili wa kijinsia katika dunia ya leo inayohimiza maendeleo jumuishi, yenye usawa na endelevu ambapo hata maandiko matakatifu yanapinga kadhia hiyo" - Shaka Mwenezi Taifa
"Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa akitoa wito Mara kwa jamii kuchukua wajibu wa kuwa mstari wa mbele kupinga na kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia ili kuwapa wanawake na wasichana mazingira huru, yenye usalama, usawa, amani na furaha kwao kushiriki katika maendeleo" -Shaka Mwenezi Taifa