shairi: U mzuri wewe uliye msiri.

shairi: U mzuri wewe uliye msiri.

Joined
Aug 4, 2017
Posts
49
Reaction score
34
1. wapenzi wengi wamekosa umahiri, umahiri wa kutunza siri,

lakini wewe u mzuri, umenitunzia siri,

nimekukosea mengi lakini umeyafanya mazuri,

u mzuri wewe uliye msiri.


2. tulipokula mbatata kwa ugali, haya yote ulisitiri,

haujawahi kuropoka, nakiri, yanayotuhusu wawili,

unayatunza yanayojiri, ndani ya chumba chetu cha siri,

u mzuri wewe uliye msiri.


3. wapenzi wengi ni machachali, wanaropoka bila siri,

ukiwakanya ni wakali, kama wamelamba shubiri,

jinsi unavyonisitiri, sijawahi choka kukujali,

u mzuri wewe uliye msiri.


4. wapenzi wengi ni wazuri, lakini hawana siri,

wakinunua binzari, hutangaza hadi mtaa wa pili,

hongera kwa kunisitiri, na kunifanya niwe rijali,

u mzuri wewe uliye msiri.


5. wapenzi wengi ni wakali, zaidi ya ladha ya pilipili,

lakini wewe unajali, mpole kama kivuli,

maneno yao kama shubiri, maneno yako matamu kama kidali,

u mzuri wewe uliye msiri.


2017, shairi hili limeandikwa na Mniko The Poet.
 
kumbe unaemsifia ni msiri ila wewe si msiri!
"Tulipokula mbatata kwa ugali,haya yote ulisitri" kumbe mlikuwa mnakula mbatata na ugali ha ha ha! we si msiri nafikiri moja ya dhamira hapo ni kutokuwa msiri! akili yangu naijua mwenyewe
 
kumbe unaemsifia ni msiri ila wewe si msiri!
"Tulipokula mbatata kwa ugali,haya yote ulisitri" kumbe mlikuwa mnakula mbatata na ugali ha ha ha! we si msiri nafikiri moja ya dhamira hapo ni kutokuwa msiri! akili yangu naijua mwenyewe
teh teh "Tulipokula mbatata kwa ugali, haya yote ulisitiri" naongezea pia kuwa kuna dhamira ya Umaskini au uhitaji kwenye shairi hili.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom