Mniko The Poet
Member
- Aug 4, 2017
- 49
- 34
1. wapenzi wengi wamekosa umahiri, umahiri wa kutunza siri,
lakini wewe u mzuri, umenitunzia siri,
nimekukosea mengi lakini umeyafanya mazuri,
u mzuri wewe uliye msiri.
2. tulipokula mbatata kwa ugali, haya yote ulisitiri,
haujawahi kuropoka, nakiri, yanayotuhusu wawili,
unayatunza yanayojiri, ndani ya chumba chetu cha siri,
u mzuri wewe uliye msiri.
3. wapenzi wengi ni machachali, wanaropoka bila siri,
ukiwakanya ni wakali, kama wamelamba shubiri,
jinsi unavyonisitiri, sijawahi choka kukujali,
u mzuri wewe uliye msiri.
4. wapenzi wengi ni wazuri, lakini hawana siri,
wakinunua binzari, hutangaza hadi mtaa wa pili,
hongera kwa kunisitiri, na kunifanya niwe rijali,
u mzuri wewe uliye msiri.
5. wapenzi wengi ni wakali, zaidi ya ladha ya pilipili,
lakini wewe unajali, mpole kama kivuli,
maneno yao kama shubiri, maneno yako matamu kama kidali,
u mzuri wewe uliye msiri.
2017, shairi hili limeandikwa na Mniko The Poet.
lakini wewe u mzuri, umenitunzia siri,
nimekukosea mengi lakini umeyafanya mazuri,
u mzuri wewe uliye msiri.
2. tulipokula mbatata kwa ugali, haya yote ulisitiri,
haujawahi kuropoka, nakiri, yanayotuhusu wawili,
unayatunza yanayojiri, ndani ya chumba chetu cha siri,
u mzuri wewe uliye msiri.
3. wapenzi wengi ni machachali, wanaropoka bila siri,
ukiwakanya ni wakali, kama wamelamba shubiri,
jinsi unavyonisitiri, sijawahi choka kukujali,
u mzuri wewe uliye msiri.
4. wapenzi wengi ni wazuri, lakini hawana siri,
wakinunua binzari, hutangaza hadi mtaa wa pili,
hongera kwa kunisitiri, na kunifanya niwe rijali,
u mzuri wewe uliye msiri.
5. wapenzi wengi ni wakali, zaidi ya ladha ya pilipili,
lakini wewe unajali, mpole kama kivuli,
maneno yao kama shubiri, maneno yako matamu kama kidali,
u mzuri wewe uliye msiri.
2017, shairi hili limeandikwa na Mniko The Poet.