Shairi: Nyege ni kunyegezana by Andanenga

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,800
Peni yangu Andanenga, uwino unapotona,
Mantiki huzilenga, na balagha na bayana,
Hufaidika malenga, huvurugika akina,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Msemo wa Kiswahili, nyege ni kunyegezana,
Maana yaki kamili, “wema ni kutendeana’,
Wasiojua fasili, hunamba nimetukana,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Ni msemo maarufu, ambao shaka hauna,
Kwenye kamusi sanifu, funueni mtaona,
Niwezeje kukashifu, nami mwana muungwana!
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Ninataja ukurasa, wazi hapa naunena,
Soma mbili moja tisa, soma bila ya fitina,
Msemo siyo wa sasa, si juzi licha wa jana,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Ushairi kubwa fani, mithili yake haina,
Kujua zake bayani, yataka kikubwa kina
Muoneni mwafulani, hata kuku wamguna,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Ulipotamkwa mlo, kaja akitunatuna,
Akakabwa koromelo, akabaki kugunaguna,
Kabakia lolololo, uzamani umechina,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Alhaji Jitukali, pokea pongezi tena,
Kikubwa chako kilili, hapandi yule mtwana,
Atuache tule wali, yeye ugali wa dona,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Kaditama wa Busara, na Mbwezi heko kijana,
Pongezi ndugu Kagera, Yobu has ante sana,
Ndimi Mshairi Bora, kipofu ninaeona,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.
(Mshairi Bora)

Amiri A. S. Andanenga (Sauti ya Kiza)
SLP 4775,
Kinondoni Shamba
Dar es salaam.
 
HUKU NA KULE

Peni yangu Andanenga, uwino unapotona,
Mantiki huzilenga, na balagha na bayana,
Hufaidika malenga, huvurugika akina,
Nyege
ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Msemo wa Kiswahili, nyege ni kunyegezana,
Maana yaki kamili, "wema ni kutendeana',
Wasiojua fasili, hunamba nimetukana,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Ni msemo maarufu, ambao shaka hauna,
Kwenye kamusi sanifu, funueni mtaona,
Niwezeje kukashifu, nami mwana muungwana!
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Ninataja ukurasa, wazi hapa naunena,
Soma mbili moja tisa, soma bila ya fitina,
Msemo siyo wa sasa, si juzi licha wa jana,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Ushairi kubwa fani, mithili yake haina,
Kujua zake bayani, yataka kikubwa kina
Muoneni mwafulani, hata kuku wamguna,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Ulipotamkwa mlo, kaja akitunatuna,
Akakabwa koromelo, akabaki kugunaguna,
Kabakia lolololo, uzamani umechina,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Alhaji Jitukali, pokea pongezi tena,
Kikubwa chako kilili, hapandi yule mtwana,
Atuache tule wali, yeye ugali wa dona,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Kaditama wa Busara, na Mbwezi heko kijana,
Pongezi ndugu Kagera, Yobu has ante sana,
Ndimi Mshairi Bora, kipofu ninaeona,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.
(Mshairi Bora)

Amiri A. S. Andanenga (Sauti ya Kiza)
SLP 4775,
Kinondoni Shamba
Dar es salaam.

Matusi, sitaki!
 
Hakuna matusi hapo Mkuu. Kiswahili kina utamu wake...

Kuna maneno/matendo katika mila na desturi za watu duniani hayasemwi/hayafanywi hadharani .Mfano, huwezi kusimama mbele za watu ukajikuna sehemu za siri. Watu watakushangaa. Si unajua Nyege ni neno la ngono, na ngono ni taboo in african customs. Au wamasemaje Mkuu?
 
Andanenga amenena lililo mwake moyoni
mwasema ametukana kwenu lipi lilo geni
nani hapa alo mwana mnalaumu kwanini
kiswahili lugha pana utamu wake lahajani

Tusi katukana nani alosema lipi baya
kipi ni tusi jamani tukisute bila haya
nijuze nipate amani kipi kimeleta haya
kiswahili lugha pana utamu wake lahajani
 
Kuna maneno/matendo katika mila na desturi za watu duniani hayasemwi/hayafanywi hadharani .Mfano, huwezi kusimama mbele za watu ukajikuna sehemu za siri. Watu watakushangaa. Si unajua Nyege ni neno la ngono, na ngono ni taboo in african customs. Au wamasemaje Mkuu?

unakijua kitu kinaitwa leseni ya kisanaa?
 
Andanenga amenena lililo mwake moyoni
mwasema ametukana kwenu lipi lilo geni
nani hapa alo mwana mnalaumu kwanini
kiswahili lugha pana utamu wake lahajani

Tusi katukana nani alosema lipi baya
kipi ni tusi jamani tukisute bila haya
nijuze nipate amani kipi kimeleta haya
kiswahili lugha pana utamu wake lahajani


It looks good as wewe sio mwandishi try to make it more serious, big up "YES YOU CAN"
 
Samahani kwa kukwazika, binafsi nakipenda sana kiswahili kwani kiingereza nimeanza kusoma kidato cha kwanza.....Nashukuru kwa kunikumbusha

wala sijakwazika,mi ni mwalimu wa lugha zote mbili kwa hiyo nakitendea haki kiswahili pale kinapostahili na nakitendea haki kiingereza pale inapostahili,huwa naumia sana mtu akitumia hizo lugha kwa wakati mmoja halafu nihisi amejichanganya au alichokusudia kusema hakijakaa sawa!uwe na amani!
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom