Sh. Bilioni 700 si Haba na Wanaobeza Vibaba

Sh. Bilioni 700 si Haba na Wanaobeza Vibaba

Wamepunguziwa deni la kodi kwa zaidi ya 99% (maana wanayotulipa haifiki hata 1% ya kodi ya 425T tuliyokuwa tunadai). Basi kama hicho ni cha kupongezwa, tuombe na wafanya biashara wetu pale kariakoo wanao-struggle kulipa kodi wapunguziwe kodi kwa 99%.
Nilichogundua Ni kwamba watanzania wengi hasa wapinzani hawana shukrani.
 
TUKIACHANA NA KUVUTIA KILA MMOJA UPANDE WAKE ,MTU ANAPOTHUBUTU KUFANYA JAMBO JEMA TOKA KWENYE UBAYA NI USTARAABU KUPONGEZA NA SI KUPONDA HATA KAMA IMPACT YA JAMBO HILO HALIKUFIKIA MALENGO KWA 100% ILHALI TU NIA ILIKUWA NJEMA..NI KUMTIA MOYO MTU HUYO.
 
Kutoka trilioni 400 mpaka bilioni 600? Unasema sio haba? Kwanza pesa yenyewe sio ya kulipa deni ni wametupa tu hili tufunge mdomo.
.
Ndiyo, hiyo pesa ni cha juu lakini usisahau kuwa watatatoa ajira ya kudumu (kodi itapatikana), wataleta maendeleo (barabara, nyumba, maji, shule, kiwanda cha kuchakachua). Hayo yote yataongeza kukuwa kwa uchumi, kwasababu kama sehemu ina miundombinu biashara itaongezeka na ajira itaongezea zaidi, wenyewe wanaita 'snowball effect'.

Utakuta ile 400Tsh yote itakuwa imelipwa baada ya muda fulani, sasa nyinyi mlikuwa mnataka kututishia nyau na kama tungewasikiliza, sio tuu tungekosa maendeleo bali tungezidi kuibiwa.

Kuna kitu kingine ambacho wengi mnakisahau na hiki ni ile nguvu ya ushawishi wa nchi, leo Tanzania imerudi kwenye mstari kama ilivyokuwa kipindi cha nyerere. Nchi inaonekana makini, siyo shamba la bibi kama zamani. Leo hii watu hawawezi kuja kutuchezea kama zamani, inabidi wajipange, wajiulize mara mbili mbili, wawekezaji wa maana watataka kuja kwa kuwa wanajua watanzania ni watu makini.
 
.
Ndiyo, hiyo pesa ni cha juu lakini usisahau kuwa watatatoa ajira ya kudumu (kodi itapatikana), wataleta maendeleo (barabara, nyumba, maji, shule, kiwanda cha kuchakachua). Hayo yote yataongeza kukuwa kwa uchumi, kwasababu kama sehemu ina miundombinu biashara itaongezeka na ajira itaongezea zaidi, wenyewe wanaita 'snowball effect'.

Utakuta ile 400Tsh yote itakuwa imelipwa baada ya muda fulani, sasa nyinyi mlikuwa mnataka kututishia nyau na kama tungewasikiliza, sio tuu tungekosa maendeleo bali tungezidi kuibiwa.

Kuna kitu kingine ambacho wengi mnakisahau na hiki ni ile nguvu ya ushawishi wa nchi, leo Tanzania imerudi kwenye mstari kama ilivyokuwa kipindi cha nyerere. Nchi inaonekana makini, siyo shamba la bibi kama zamani. Leo hii watu hawawezi kuja kutuchezea kama zamani, inabidi wajipange, wajiulize mara mbili mbili, wawekezaji wa maana watataka kuja kwa kuwa wanajua watanzania ni watu makini.

Hizi ni habari za kufikirika, wamekaa pale miaka zaidi ya 20 wamefanya jambo gani la maana? Usitegemee Mzungu akuletee maendeleo kwako.
 
Hizi ni habari za kufikirika, wamekaa pale miaka zaidi ya 20 wamefanya jambo gani la maana? Usitegemee Mzungu akuletee maendeleo kwako.
.
Hata mwanzoni mlisema tutapelekwa mahakama ya kimataifa lakini sasa hivi stori imebadilika. Na siyo kuwa wanatuletea maendeleo bali wanashurutishwa kisheria, hapo mwanzo sheria haikuwabana kufanya hivyo.
 
.
Hata mwanzoni mlisema tutapelekwa mahakama ya kimataifa lakini sasa hivi stori imebadilika. Na siyo kuwa wanatuletea maendeleo bali wanashurutishwa kisheria, hapo mwanzo sheria haikuwabana kufanya hivyo.

Mimi na nani? Unaweza kuniambia ni lini nilisema hivyo?
 
Mie sijaona cha kushangaa hapo ikiwa Chinga ukiuliza bei ya kiatu atakuanzia 30,000 bahada ya majadiliano na kushushana bei, unakinunua kwa 6,000. hapo ajabu nini?
 
Mie sijaona cha kushangaa hapo ikiwa Chinga ukiuliza bei ya kiatu atakuanzia 30,000 bahada ya majadiliano na kushushana bei, unakinunua kwa 6,000. hapo ajabu nini?
Wangeruhusu basi na sisi tunaobanbikiziwa kodi huku kwenye viduka vya mtaani tujadiliane, ili mtu ukipewa kodi ya milioni tatu uweze kulipa laki sita, vingevyo hizo ni double standards.
 
Bln 700 ni mishahara ya watumishi wa umma ya mwezi mmoja tu

Ova
 
haya twende hivi.
toa gharama za vikao
posho kwa waendesha vikao hivyo
gharama za kamati zote mbili
zimebaki kiasi gani?


ambacho naweza kukubaliana na wewe ni hapo ulipo sema
kilicho kubaliwa ni zaidi ya fedha ijumaa njema wadau.
vipi kuhusu 50/50?
 
Wamepunguziwa deni la kodi kwa zaidi ya 99% (maana wanayotulipa haifiki hata 1% ya kodi ya 425T tuliyokuwa tunadai). Basi kama hicho ni cha kupongezwa, tuombe na wafanya biashara wetu pale kariakoo wanao-struggle kulipa kodi wapunguziwe kodi kwa 99%.
Hayo ya kupunguziwa kodi umeambiwa na na nan?
 
Mwanakijiji kwa mara ya kwanza nimeona ameandika makala ndefu lakini iliyokosa logic. Unaposema billion 670 si haba, siyo haba ukilinganisha na nini. Kwa vurugu tulizofanya, tumepoteza kiasi gani kwa kulinganisha na hiyo billion 670? Uzalishaji umesimama, tumepoteza kiasi gani cha kodi kama uzalishaji ungeendelea? wafanyakazi wamepoteza ajira, makampuni ya utafiti yote yamesimama na mengine kuondoka, wafanyakazi kwenye makampuni ya utafiti wote wamepoteza ajira, serikali imekosa kodi kutoka kwenye makampuni ya utafiti na kutoka kwa wafanyakzi wao, mifuko ya hifadhi ya jamii imepoteza mapato. Makampuni yote yaliyowekeza kwenye share markets yamepoteza kati ya 30 - 60% kwa sababu yalionekana yamewekeza kwenye eneo hatari. Sustainability ya mining industry ipo mashakani maana huwezi kuwa na sustainability kama hakuna utafiti.

Swali la kujiuliza, hivi hakukuwa na uwezekano wa kupata hizo billion 670 bila kusababisha taharuki kubwa na kuufanya uchumi wetu kuwa mashakani? Mbona Kikwete aliweza kubadilisha sheria ya madini bila ya kuleta matokeo hasi kama haya? Kikwete alibadilisha mrabaha kutoka 3% mpaka 4%, free carried shares alibadilisha kutoka 0% mpaka 10%. Aliweka sharti la minimum local procurement ya 45%, akaweka sharti la kila mgodi kuwa na succession plan iliyosababisha watanzania wengi kushika nafasi za juu kwenye migodi, aliweka kiwango cha chini cha mshahara kwenye migodi kuwa cha juu kuliko sekta zote. Alifanya mengi lakini bila kelele. Safari hii yamefanyika madogo na machqche sana kwa kelele nyingi na kusababisha hasara kubwa za kiuchumi na kijamii.

Hata kama dhamira ilikuwa njema, mbinu ilikuwa mbaya sana.
 
Yaani hii dunia kuna watu wameumbwa kubisha na kupinga kila jambo hata lingekuwa zuri kiasi gani watalijengea mazingira lionekane baya,na wao waonekane sahihi na wote walio nyuma yao hufuata misimamo hiyo hiyo bila hata chembe ya kuhoji, amini nawaambieni hawataubadili uhalisia wa jambo zuri kuwa baya kwa maneno.
 
vipi kuhusu 50/50?
50/50 si chochote. Haimaanishi chochote. Hiyo 50/50 siyo ownership bali ni mgao baada ya kutoa production costs, kodi zote na dividents. Bulyanhulu haijawahi kupata faida kwa zaidi ya miaka 10 (na ni jambo la kawaida sana kwenye migodi. Wastani wa Dunia ni kuwa katika kila migodi 7 ni 4 tu ndiyo hutengeneza faida kupitia uzalishaji). Unafahamu kuwa Mwadui tunamiliki 50% lakini kwa miaka 50 hatujawahi kupata kitu? Wanaojua uchumi wa madini, hata nikiambiwa serikali ichukue 60% ya faida, ningekubali maana najua watakachopata ni fahari ya macho.
 
Subiri kwanza bwana Thornton apeleke haya mapendekezo kwa share holders na board ya wakurugenzi wa ACCACIA ndo utoke kifua mbele maana yawezekana kabisa wakayatupa kapuni.
Halafu hiyo 700B kwa tafasiri ya haraka ni tutaiitaje vile? kuzibwa mdomo au ni wazungu wameamua kujisafisha tu mbele ya uso wa dunia ya kibiashara?
Hamchoki kuhamisha magoli. Nyinyi si ndio mliosema kwamba huyo Thornton hawezi kuja kuongea na serikali?.

Amekuja na amefikia makubaliano, mnasema tusubiri akaongee na wakurugenzi!!, akiongea na wakurugenzi na wakafikia makubaliano mtasema subiri tuone kama fedha zimeingia hazina!!.

By the way, lini tunakwenda kushtakiwa MIGA?.
 
Tujadiliane kwa tija badala ya uelekeo huu wa sasa kupingana tu....nchi bila upinzani makini ni hasara kwa taifa, ni wakati tujiulize tunataka upinzani wa aina gani ....tunapingana tu hadi kwenye vitu vilivyo wazi kabisa ...base ya malalamiko wakati JPM amezuia Makinikia imegeuzwa ....hawataki kukubali walikosea ....Nyerere alikiri kukosea, hata CCM yenyewe wanakubali walichemka kwenye mikataba ...kwanini wapinzani wasikubali kukosea na kujenga hoja mpya ....hoja hapa ingekuwa utekelezaji wa haya makubaliano ....lakini kwa hili serikali inastahili pongezi ...
 
Back
Top Bottom