Sh 64 bilioni zatumika sherehe za Uhuru!

Sh 64 bilioni zatumika sherehe za Uhuru!

hivi kuna mtu anamzidi mwanakijiji umbeya kweli??? khaaa

hahahahaha
Naomba nisijibu hili mkuu....
Huyo ni poti wangu sana......
Ila mzazi pia una swagga za kimbeya kweli kama Sugu!

 

We ni Daudi mtata, sio Mchambuzi.....
Hata JK akiiona atalia!
Unajua tatizo la watawala wetu hawana watu wa kuwakumbusha haya, wamezungukwa na mahayawani ambayo kila siku ni nkumsifia na kumwambia kuwa bongo kama ulaya na uchumi unakuwa sana.
 
We ni Daudi mtata, sio Mchambuzi.....
Hata JK akiiona atalia!
Unajua tatizo la watawala wetu hawana watu wa kuwakumbusha haya, wamezungukwa na mahayawani ambayo kila siku ni nkumsifia na kumwambia kuwa bongo kama ulaya na uchumi unakuwa sana.


Mkuu wao wenyewe ni mahayawani pia.
 
hivi ni sherehe gani hasa imegharimu kiasi hicho kikubwa cha fedha bilioni 64,hayo maonyesho uchwara ya wizara, hilo gwaride uwanja wa taifa, au hiyo sherehe ya nishani ikulu???hapa bongo kila kitu ni deal tu, kuna watu hata kwenye mazishi ya binadamu mwenzao kwao ni deal ya kutengeneza fedha,hizi fedha zimekua inflated tu lakini zimeishia mifukoni kwa watu. Kama mwananchi wa kawaida ningependa kujua budget ya matumizi ya fedha hizi imetoka kwenye kasma gani na je imeidhinishwa na bunge??nchi maskini kama hii itatumiaje fedha zote hizi kwa sherehe tu ya kawaida wakati kuna lundo la matatizo yanayo wakabili wananchi wake,ni wajibu wetu kama watanzania kuhoji mwenendo huu mbovu wa matumizi ya kodi za wanainchi.
 
Kama zimelipwa mifukoni mwa watz wenzetu sio mbaya sana maana zitaongeza mzunguko wa fedha, na at the end of the day nyingine zitarudi kwene kapu la hazina Kama kodi, zengine zitatrickle down mpaka huku Uswazi kwa wauza maandazi. Dili za hovyo ni zile za kuwalipa maponjoro au mafisi wengine halafu wanazitoroshea Dubai..hili ndio la kupinga kwa nguvu zote.
 
hahahahaha
Naomba nisijibu hili mkuu....
Huyo ni poti wangu sana......
Ila mzazi pia una swagga za kimbeya kweli kama Sugu!

LOL.... mie mndundu kuliko sugu, mbishi kuliko dagaa na maneno kuliko mbwiga
 
Hazikutumika kwenye sherehe bali wamegawana wakubwa kwa kupeana tenda uchwara za mapambo, vinywaji, kukirimu wageni, ulinzi, ushenzi, matangazo, vyombo vya habari, umbea uongo na upuuzi mwingine. Hiyo ndiyo namna mafisadi wapumbavu waibiavyo wanuka njaa.
 
Celebrations are for Achievements. WHAT has the current regime ACHIEVED? WHAT is there to be PROUD of for making TANZANIA the 3rd leading AID recipient country in the world? IS that an ACHIEVEMENT? Be FREE from the colonizers in order for the nation to become a welfare state. The per diems says it all. ALL your money went mostly to per diems for civil servants. SHOCKING! A nation that cannot even feed its citizens squandering money like its an English monarchy.
 
wivu wa kike huo bil 64 ndogo sana kulinganisha na umuhimu wa sherehe husika hivi hata baba mwenye binti au kijana anayeoa si atafanya kila awezalo kufanikisha sherehe hata awe masikini vipi nyie wa zamani kweli!!

Hatusemi hapakuwa na umuhimu wa kusherekea bali tunapinga gharama kubwa iliyotumika. Hizo pa diem sijui zililipwa kwa lengo gani wakati kila watu waliombwa kusherekea mahali walipo! Pia ikumbukwe kwa watumishi kama askari, wakuu wa wilaya na hata mawaziri kwenda uwanjani kuadhimisha shughuli kama hiyo ni moja ya majukumu yao ya kila siku na wanalipwa mishahara kwa hilo, hivyo haikuwepo sababu ya kulipana posho.
 
Mi mara nyingi huwa nawashangaa mnaojiita Great thinker,kwani kuna tofauti gani mchaga kutumia milion kumi akisherekea xmas rombo na ndgu zake ambao hat secondary hawajagusa na nchi yenye watu zaidi ya 40mil?,nyie wenyewe kila mwaka mnafanya birthday zenu za zaidi ya 70 elfu na hili khari bado hamja timiza mahitaji yenu yote ya kifamilia iweje gvt isisherekee 50yrs kwa Bs?ok anaway this is a demothinking ground.

Wewe nae!
Kwani huyo mchagga anakuwa na majukumu gani au mangapi mpaka kufikia kufanya hiyo sherehe au una uhakika gani kama anakuwa hajatimiza majukumu yake yote!
Hapa naona unataka we ndo uonekane great thinker etiiiii eeeeeeh si ndio??
Mchagga gani alienda kusherehekea na kutumia 10m wakati wanae au mkewe au mzazi wake yuko mahututi hospitali au ni mchagga gani alietumia 10m kwenye starehe alafu akashindwa kuwapeleka wanae secondary au hata chuo???
Ni upofu wa fikra kujustify ubadhirifu wa rasilimali za umma kwa kutumia mifano ya watu binafsi wanaotumia mali zao katika starehe. Hebu kaone mataifa ya magharibi watu wanavyofanya starehe alafu uje unambie kama bongo kuna starehe alafu angalia mipango ya matumizi ya nchi hizo na ujaribu kuoosha mambo labda itakusaidia kidogo! "great thinker"
 
Wanafunzi wangapi wameshindwa kuripoti chuo kisa ada?. Shule ngapi za kata hazna madawati, vitabu, laboratory n.k! Vijiji vingapi havina maji! Waalimu wangapi wanadai makato yao!.. Vijiji vingapi havna magari ya kubebea wagonjwa!

Matatizo ni mengi sana. Inakuaje watumie 64bln/day?. Hawawatendei haki watanzania.
Haya sio mawazo yako, labda uniambie Nape amekutosa!
 
Fedha hizi ni nyingi sana kwa nchi maskini kama yetu. Mtu maskini kule kijijini amefaodika na nini ma matumizi haya yote ni heri tungenunua madawati, kujenga zahanati. Jamani naomba uchunguzi wa haraka ufanyike na watu wachukuliwe hatua uganda iliwezekana na hata hapa inawezekana
 
Ukisikia Kenya wanaisifia TZ basi ujue wanasifia huu upupu ili wazidi kuwa juu!
 
duuh, mihela iliyotumika ni mingi! ndio maana kila kitu kimepanda bei sababu kumbe walikuwa wanaandaa sherehee!!!!!!!
 
bilioni 64 kwa sherehe wakati umeme nchini ni mgogoro,shule za kata walimu mgogoro, hospitali za govt panadol ni issue,maji vijijini na mjini ni issue,madawati primary school ni mgogoro, wakati huo huo tanzania ina aibika kama taifa namba tatu kwa kuombaomba duniani??????
 
Back
Top Bottom