Sex After CS ?

I really dont have a straight answer for that but....nadhani wanawake wengi huwa wanaexaggerate ile hali ya kujifungua kwa CS, nimeshaona wanawake wengi tu mwaka mmoja au zaidi baada ya CS bado analalamika 'mshono'...kaka yangu anadekewa mshono mpaka sasa wakati CS ilifanyika miaka mi4 iliyopita (mke hataki kwenda uchagani eti kuna baridi, akienda mshono unauma!).

Ukweli ni kwamba, kovu liniloogopwa baada ya CS ni lile kovu la ndani kwenye kizazi, na tataizo la kovu ili ni iwapo mama aliyejifungua kwa CS atapata ujauzito tena. Kizazi kinapopanuka kutokana na ukuaji wa mtoto, basi na kovu linapata hatari ya kuchanika, na anapoanza uchungu hatari hiyo inakuwa kubwa sana kiasi cha kuhitaji uangalizi wa karibu sana wa daktari..au kufanyiwa tena CS.

Lakini baada ya kujifungua na kidonda kupona kabisa, kitu mabacho hakichukui zaidi ya mwezi mmoja tangu CS, hakuna madhara yeyote yaliyokuwa documented ambayo wake/wachumba/dada/rafiki zetu wanayalalamikia ie..mshono kuuma wakati wa tendo la ndoa, mshono kuuma wakati wa baridi, mshono kuuma kama akifanya mazoezi (mfano ya kurudisha tumbo, ndio maana wanawake wengi waliojifungua kwa CS matumbo yao hayarudi kwa kudeka), mshono kuuma akifanya kazi, etc...Baada ya CS na vidonda kupona, masiha yanaendelea kama kawaida sawa na mwanamke aliyejifungua kwa njia ya kawaida ya uzazi!

Kwa hiyo...muda wa kusubiri kufanya tendo la ndoa kwa mwanamke aliyejifungua kwa CS au kwa kawaida ni ule ule tu, japo hii process inategemea na utayari wa kisaikolojia wa wote wawili (mume na mke) ili muweze kuenjoy tendo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom