Serikali za awamu zilizopita ziligubikwa na kashfa za ufisadi, waliwezaje kuendesha nchi

Agama_Agama

Senior Member
Sep 13, 2016
141
135
Nimekuwa nikijiuliza swali hili bila mafanikio ya kupata jibu. Serikali za awamu mbili zilizopita ziligubikwa na kashfa nyingi za ufisadi uliohusisha mabilioni ya shilingi.
Awamu hii ilikuja na kutuaminisha kuwa itapambana na ufisadi na kubana matumizi ya serikali. Haya yalianza kutekelezwa mara tu serikali hii ilipoingia madarakani.

Safari za nje kwa watumishi zikapigwa stop mpaka kipatikane kibali cha mkulu, likaja zoezi la kupunguza matumizi ya vikao, wakasakwa watumishi hewa, ukaja uhakiki wa watumishi (kitu ambacho sijaona tija yake kabisa zaidi ya kuharibu mifumo - creating instability), kuhimiza ukusanywaji wa kodi (tunaambiwa makusanyo yameongezeka) na mengine mengi yaliyolenga kubana matumizi na kuongeza pato la taifa.

Kimtazamo hali hii ilitakiwa kufanya maisha yawe bora zaidi maana mianya ya wapigaji imezibwa. Cha kunishangaza ni kuwa hali imekuwa tofauti katika kipindi cha takriban miaka miwili. Huduma zitolewazo na serikali zimezorota mfano mzuri ukiwa hospitali za serikali. Katika vipindi viwili vilivyopita hakukuwahi kuwa na upungufu wa dawa hospitalini kama tuliouona katika kipindi hiki.

Watumishi wa serikali wamekuwa wakipata nyongeza kwenye mishahara kila mwaka ili kujaribu kufidia ongezeko la gharama za maisha, kitu hicho kimekuwa ni ndoto huku gharama za maisha zikizidi kupanda.

Yapo mengi nayoyafikiria mpaka kujiuliza hili swali, serikali zilizotangulia ziliwezaje kuepuka hii hali ya sasa ikiwa kulikuwa na wapigaji kila sehemu, wafanyakazi hewa, wakwepa kodi na madudu mengine yote?
 
Nimekuwa nikijiuliza swali hili bila mafanikio ya kupata jibu. Serikali za awamu mbili zilizopita ziligubikwa na kashfa nyingi za ufisadi uliohusisha mabilioni ya shilingi.
Awamu hii ilikuja na kutuaminisha kuwa itapambana na ufisadi na kubana matumizi ya serikali. Haya yalianza kutekelezwa mara tu serikali hii ilipoingia madarakani.

Safari za nje kwa watumishi zikapigwa stop mpaka kipatikane kibali cha mkulu, likaja zoezi la kupunguza matumizi ya vikao, wakasakwa watumishi hewa, ukaja uhakiki wa watumishi (kitu ambacho sijaona tija yake kabisa zaidi ya kuharibu mifumo - creating instability), kuhimiza ukusanywaji wa kodi (tunaambiwa makusanyo yameongezeka) na mengine mengi yaliyolenga kubana matumizi na kuongeza pato la taifa.

Kimtazamo hali hii ilitakiwa kufanya maisha yawe bora zaidi maana mianya ya wapigaji imezibwa. Cha kunishangaza ni kuwa hali imekuwa tofauti katika kipindi cha takriban miaka miwili. Huduma zitolewazo na serikali zimezorota mfano mzuri ukiwa hospitali za serikali. Katika vipindi viwili vilivyopita hakukuwahi kuwa na upungufu wa dawa hospitalini kama tuliouona katika kipindi hiki.

Watumishi wa serikali wamekuwa wakipata nyongeza kwenye mishahara kila mwaka ili kujaribu kufidia ongezeko la gharama za maisha, kitu hicho kimekuwa ni ndoto huku gharama za maisha zikizidi kupanda.

Yapo mengi nayoyafikiria mpaka kujiuliza hili swali, serikali zilizotangulia ziliwezaje kuepuka hii hali ya sasa ikiwa kulikuwa na wapigaji kila sehemu, wafanyakazi hewa, wakwepa kodi na madudu mengine yote?


cc Akina MM & Pasco
 
Hakuna cha kujibu hapo, nchi hii ni masikini tanfu kuanzishwa kwake, na tangu nizaliwe sijawahi kusikia Watanzania wakisema wanapata huduma nzuri Hospitalini au wana Mishahara mizuri kazini, hivyo ni stupi post!
Unajua unapoambiwa wewe ni mrefu lazima wamekupima na mtu mwingine
 
Hakuna cha kujibu hapo, nchi hii ni masikini tanfu kuanzishwa kwake, na tangu nizaliwe sijawahi kusikia Watanzania wakisema wanapata huduma nzuri Hospitalini au wana Mishahara mizuri kazini, hivyo ni stupi post!
Tunaweza kuwa maskini lakini hali ya maisha katika huu huu umaskini ikatofautiana baina ya awamu moja na nyingine hilo ndilo analohoji..
Mkuu hivi sisi ni maskini wa nini wakati tuna kila kitu madini, mbuga, bahari na vyote vinavyoambatana nayo.
Huoni tatizo ni wasimamizi?
 
Another stupid chadema fan, kwa hiyo TZ ilikuwa rich country kabla?
Acha upuuzi weka uchama pemben na utumie akili badala ya kicheo kufikiria. Alichoongea n Kwel kkabisa hi ni awamu ya sifa pesa zinatumika kumsifia Mangu na kujenga chato na chama kwa kununua na kuuwa upinzani....kila kona hali n mbaya zimebaki blabla na ahadi za kutafuta sifa kwenye majukwaa kila uchwao, huku hakuna linalofanyika la maana. Ww unayeshabikia awamu hii bora usingelizaliwa ni hasara huna mchango wwte zaidi ya kutujazia vyooo.. Tukutane 26/4
 
Acha upuuzi weka uchama pemben na utumie akili badala ya kicheo kufikiria. Alichoongea n Kwel kkabisa hi ni awamu ya sifa pesa zinatumika kumsifia Mangu na kujenga chato na chama kwa kununua na kuuwa upinzani....kila kona hali n mbaya zimebaki blabla na ahadi za kutafuta sifa kwenye majukwaa kila uchwao, huku hakuna linalofanyika la maana. Ww unayeshabikia awamu hii bora usingelizaliwa ni hasara huna mchango wwte zaidi ya kutujazia vyooo.. Tukutane 26/4
Kuna wakati huwa naona umuhimu wa kutumia condom
 
Waliweza kwa sababu wakati huo angalao ccm ilifuata misingi ya kuanzishwa kwake, ilikuwa huwezi kusikia lugha kama hizi kwa mfano, waliokula hela hizi watazitoa kupitia kwenye matundu yaliyopo kwenye miili yao, n.k.
 
Makarai yamebanwa kila kona awamu hii, ngosha endelea kukaza mpaka yanyooke sawasawa!
 
Kila zama nayake,kupanga ni kuchagua, mtoa mada swali kwako,umri wako please tuuujue ili tukupe ulinganifu
 
Back
Top Bottom