Serikali yatoa trilioni moja za kununua dawa

Serikali hii kwa uongo. Hivi wana ccm mnaijua trillion??
Mmejiuliza bajet ilikua sh ngap ya wizara ya afya? Nakataa mpaka nakufa hakuna uwezekano wa serikali hii kutoa trillion moja tena kwa wakati mmoja kununulia dawa ni uongo!! Subirin mtajua haya!!
 
Zilongwa mbali zitendwa mbali

Sasa kama hela ya dawa imepelekwa leo vipi wagonjwa wa juzi je walipaswa kuvumilia ugonjwa hadi hii leo ambapo serikali itanunua hizo dawa au zilitakiwa zipewe kipaumbele kwa kununuliwa kabla hata ya vitu vingine?
Nyumbu ni nyumbu
 
Chanjo tuu ya yellow fever pamoja na kuwa sisi wananchi tunanunua sh15,000 inashindikana sembuse hizo dawa za bure
 
Tatizo ni kuongea bila kutenda....

Hivi mngenunua dawa kimya kimya watu wakazikuta hospital si wangekuja hapa kuwasifia wenyewe bila kujitangaza.......

Masikini majaliwa naye kaambukizwa kuongea sana bila kutenda......
Tatizo lako unaongea kwa kukurupuka. Utakua una matatizo kichwani. Be careful! Utakuja toa bomu la mwaka ambalo litakupeleka lupango very soon
 
Najua kuna kikundi fulani kitakuja na kukejeli hatua hii. Mungu ibariki serikali hii ya awamu ya tano kwani ni wewe ee Mwenyezi ulie iweka madalakani kama njia za kuikomboa Tanzania.
Sasa yale madeni yao pale MSD wamelipa ? Kumbuka hiyo ni hela imetolewa , sasa ukiambiwa 85% imelipa deni usirushe ngumi .
 
Serikali hii kwa uongo. Hivi wana ccm mnaijua trillion??
Mmejiuliza bajet ilikua sh ngap ya wizara ya afya? Nakataa mpaka nakufa hakuna uwezekano wa serikali hii kutoa trillion moja tena kwa wakati mmoja kununulia dawa ni uongo!! Subirin mtajua haya!!
Labda na za Kagera zimeunganishwa humo!
 


AHADI ya serikali ya kuanza kusambaza dawa katika hospitali zote nchini kutokana na madai ya kuwepo kwa uhaba wa dawa za aina mbalimbali, imeanza kutekelezwa.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa ziarani mkoani Arusha amesema Serikali imetoa Sh trilioni moja kwa ajili ya ununuzi wa dawa na kuhakikisha pia madaktari 8,000 wanasambazwa kwenye hospitali mbalimbali za mikoa na wilaya ili kutatua changamoto za afya na utoaji wa huduma bora kwa wananchi.
Katika hatua nyingine, Majaliwa amewataka watendaji wa Idara ya Uhamiaji kufanya misako kwenye nyumba za wageni na kudhibiti wageni wanaoingia kwenye mipaka mbalimbali nchini kutokana na kushamiri kwa wahamiaji haramu.
Aliyasema hayo jana wakati alipokuwa akizungumza na watumishi wa idara na taasisi mbalimbali za serikali ikiwemo watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha na Wilaya ya Arusha.
Ukosefu wa dawa.
Akizungumzia upatikanaji wa dawa, Majaliwa alisema serikali imetoa Sh trilioni moja kwa ajili ya ununuzi wa dawa za aina mbalimbali ili kuondoa upungufu wa dawa kwenye hospitali nchini.
Akieleza namna serikali ilivyo na nia ya dhati ya kumaliza tatizo la dawa nchini, Majaliwa alisema; “Awali tulitoa Sh bilioni 40 kwa ajili ya dawa na sasa tumeongeza fedha hadi kufikia shilingi trilioni moja.
“Tunataka kero ya upungufu wa dawa hospitalini iishe. Naagiza kila hospitali kuhakikisha inakuwa na dirisha la huduma za bure kwa wazee pamoja na duka la dawa,” alisema.


Chanzo: ITV
Safi sana Mh. waziri mkuu...pigeni kazi hatimaye wenye maneno watakosa cha kuongea watakapo ongea vyote vikaisha
 
Zilongwa mbali zitendwa mbali

Sasa kama hela ya dawa imepelekwa leo vipi wagonjwa wa juzi je walipaswa kuvumilia ugonjwa hadi hii leo ambapo serikali itanunua hizo dawa au zilitakiwa zipewe kipaumbele kwa kununuliwa kabla hata ya vitu vingine?
Hivi kulalamika siku hizi imekuwa sifa?
 
Haya mambo ya kuja hadharani kusifia kuwa sirikali imenunua madawa ni sawa na baba kwenda barabarani nakujisifia kuwa amewanunulia watoto wake chakula!
 
Bunge lilipitisha hayo matumizi???? Yako kwenye Bajeti ya Wizara ya Afya 2016-2017?????
 
Kweli ninaamini ukiwa nyumbu ni ngumu kujitambua, ndiomaana maMvi hakurudi kwao kuchunga ng'ombe ameamua kuchunga nyumbu. Yaani ili la serikali kununua dawa mnapiga?
 
hizi sound tu

Kati ya wizara hali mbaya ni hiyo ya afya. Hakuna fedha kabisa zinazotoka serikali kuu. Mahospitali yanayotegemea fedha za serikali kuu hali mbaya.
ofisi za watendaji hali mbaya, OC zinapelekwa chini ya asilimia 10. watendaji hawapewi vitendea kazi. Pesa zinazokusanywa si vibaya kuziita fedha hewa. Maana hakuna zinakoonekana Zaidi ya kwenye matamko ya TRA.
 
Bajeti Wizara ya Afya 2016/17 ni kizungumkuti

Bajet ya afya ni billion 800 , msiwe wenda wazimu. Mnataka kuniambia serikali safari hii imevuka lengo??

Tunadanganywa wadanganyika kwa mara nyingine tena

Tunadanganywa mchana kweupe. Wizara ya afya fedha zilizotolewa toka kipindi cha bajeti hata asilimia 20 inaweza isifike. na hapo walishakata fedha zilizokuwa zina-bajetiwa kipindi cha nyuma.

hakuna cha trilioni wala mjomba wake trilioni, labda trilioni ya zimbabwe
 
Back
Top Bottom