Serikali Yatoa Onyo: Hakuna atakayevumiliwa kwa kuficha Mgonjwa wa Mpox, wakiwemo waganga wa kienyeji

Serikali Yatoa Onyo: Hakuna atakayevumiliwa kwa kuficha Mgonjwa wa Mpox, wakiwemo waganga wa kienyeji

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Mkoa wa Tabora umeanzisha oparesheni maalamu ya kukabiliana na ugonjwa wa mlipuko wa mpox kwa kuandaa vituo tengefu kwenye Hospitali za Wilaya zote za mkoa huo pamoja na vituo vya afya ili kuwahudumia kwa kina wagonjwa wa mlipuko huo endapo watabainika, huku wataalamu wa afya ngazi ya mkoa wakiendelea kutoa elimu kwa jamii na kufanya uchunguzi wa kubaini kama kuna mgonjwa yeyote mkoani hapo ili wachukue hatua stahiki.

Soma Pia: Wizara ya Afya yathibitisha uwepo wa wagonjwa wawili wa Mpox nchini

Katika hatua nyengine japo hakuna kisa chochote cha ugonjwa huo kwa Mkoa wa Tabora lakini Katibu Tawala wa Mkoa wa huo Daktari John Mboya amesema Serikali haitamvumilia mtu yeyote wakiwemo Mganga wa kienyeji atakayebainika kushiriki kumficha Mgonjwa wa Mpox kwa sababu za Imani za Kiahirikina
 
Back
Top Bottom