Trust None
JF-Expert Member
- Feb 12, 2018
- 1,260
- 4,421
Huu ni ushindi kwa mabeberu waliokatalia baadhi ya misaada,
wakishinikiza sheria ibadilishwe.
BUNGE limefuta kifungu cha 37(4) cha Sheria ya Takwimu kinachotoa adhabu kwa mtu anayetoa taarifa za takwimu bila kupata kibali cha Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).
Katika kifungu hicho cha 37 (4) kabla ya kupendekezwa kufutwa katika marekebisho yaliyopelekwa bungeni na kisha kupitishwa, adhabu kwa makosa ya jinai katika Sheria ya Takwimu ilikuwa ni miezi sita jela au kulipa faini isiyopungua Sh. milioni mbili au vyote viwili.
Makosa kwa mtu yeyote kutoa taarifa zilizopatikana isivyo halali, adhabu yake ni kifungo kisichopungua miezi 12 au faini isiyopungua Sh. milioni tano au vyote viwili.
Katika marekebisho ya Sheria ya Takwimu (Sura ya 351) iliyosomwa Bungeni na Prof. Kilangi, yanaeleza kuwa marekebisho ya jumla yanayopendekezwa katika sheria hiyo yanalenga kubainisha dhahiri haki ya kuchapisha au kutoa taarifa za takwimu kwa umma.
Kwa maelezo ya Mwanasheria Mkuu huyo wa serikali, mapendekezo hayo yanakusudia kuanzisha Kamati ya Kitaalamu (Technical Committee) ambayo jukumu lake litakuwa kupokea kujadili malalamiko yanayotokana na wadau kuhusu usahihi wa takwimu zilizotolewa kwa umma.
"Katika jedwali la marekebisho, inapendekezwa kufuta vifungu vya 24A na 24B na kuviandika upya, pia kuongeza vifungu vipya vya 24C, 24D, 24E na 24F kwa lengo la kuweka utaratibu wa kutoa matokeo ya takwimu zinazotofautiana na takwimu rasmi zilizotolewa na serikali," alisema Kilangi.
Kwa mujibu wa Mwanasheria Mkuu, marekebisho hayo yanatoa fursa kwa mtu yeyote kutoa takwimu zinazotofautiana na zilizotolewa na serikali, iwapo atakuwa amezingatia misingi ya kitakwimu iliyowekwa katika miongozo mbalimbali ya kitaifa na kimataifa inayosimamia utoaji wa takwimu.
Lakini, sambamba na marekebisho hayo sheria hiyo inapendekeza kufutwa kwa kifungu cha 37 (4) kinachotoa adhabu kwa mtu anayetoa taarifa za takwimu bila kupata kibali cha Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).
Rejea https://www.ippmedia.com/sw/habari/bunge-lafuta-adhabu-sheria-ya-takwimu
---------
"Don't start what you can't finish!"
anyway, poleni Taifa Stars, pole mh. Makonda na poleni Watanzania wote.
wakishinikiza sheria ibadilishwe.
BUNGE limefuta kifungu cha 37(4) cha Sheria ya Takwimu kinachotoa adhabu kwa mtu anayetoa taarifa za takwimu bila kupata kibali cha Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).
Katika kifungu hicho cha 37 (4) kabla ya kupendekezwa kufutwa katika marekebisho yaliyopelekwa bungeni na kisha kupitishwa, adhabu kwa makosa ya jinai katika Sheria ya Takwimu ilikuwa ni miezi sita jela au kulipa faini isiyopungua Sh. milioni mbili au vyote viwili.
Makosa kwa mtu yeyote kutoa taarifa zilizopatikana isivyo halali, adhabu yake ni kifungo kisichopungua miezi 12 au faini isiyopungua Sh. milioni tano au vyote viwili.
Katika marekebisho ya Sheria ya Takwimu (Sura ya 351) iliyosomwa Bungeni na Prof. Kilangi, yanaeleza kuwa marekebisho ya jumla yanayopendekezwa katika sheria hiyo yanalenga kubainisha dhahiri haki ya kuchapisha au kutoa taarifa za takwimu kwa umma.
Kwa maelezo ya Mwanasheria Mkuu huyo wa serikali, mapendekezo hayo yanakusudia kuanzisha Kamati ya Kitaalamu (Technical Committee) ambayo jukumu lake litakuwa kupokea kujadili malalamiko yanayotokana na wadau kuhusu usahihi wa takwimu zilizotolewa kwa umma.
"Katika jedwali la marekebisho, inapendekezwa kufuta vifungu vya 24A na 24B na kuviandika upya, pia kuongeza vifungu vipya vya 24C, 24D, 24E na 24F kwa lengo la kuweka utaratibu wa kutoa matokeo ya takwimu zinazotofautiana na takwimu rasmi zilizotolewa na serikali," alisema Kilangi.
Kwa mujibu wa Mwanasheria Mkuu, marekebisho hayo yanatoa fursa kwa mtu yeyote kutoa takwimu zinazotofautiana na zilizotolewa na serikali, iwapo atakuwa amezingatia misingi ya kitakwimu iliyowekwa katika miongozo mbalimbali ya kitaifa na kimataifa inayosimamia utoaji wa takwimu.
Lakini, sambamba na marekebisho hayo sheria hiyo inapendekeza kufutwa kwa kifungu cha 37 (4) kinachotoa adhabu kwa mtu anayetoa taarifa za takwimu bila kupata kibali cha Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).
Rejea https://www.ippmedia.com/sw/habari/bunge-lafuta-adhabu-sheria-ya-takwimu
---------
"Don't start what you can't finish!"
anyway, poleni Taifa Stars, pole mh. Makonda na poleni Watanzania wote.