Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,896
Uchunguzi wa Mauaji
Katika hatua nyingine, Werema amekiri bungeni kwamba Serikali imekuwa dhaifu kwa kutochunguza vifo vya raia ambavyo vimekuwa vikitokea katika mazingira yenye utata na kuahidi kwamba taratibu zinafanywa ili uchunguzi ufanyike.
"Nakiri kwamba tulilegalega kidogo kwa kutofanya uchunguzi wa mauaji yaliyotokea bila kujua sababu zake, lakini tumejiandaa shughuli hiyo itaanza karibuni".
Alisema uchunguzi wa vifo hivyo utafanywa na Mahakama za Korona (Coronerยs Court) ambazo zilikwishaundwa tangu mwaka 2004 kwa Tangazo kwenye Gazeti la Serikali namba 252 la Julai 16, 2004.
"Jaji Kiongozi kwa kushirikiana na Jaji Mkuu waliwateua mahakimu wote wakazi kuwa makorona (viongozi wa Mahakama za Korona), hivyo watu wa kufanya kazi hii (ya uchunguzi) wapo. Tutatumia taarifa hizi zilizotolewa, ipo ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora na yingine ili kujua nini hasa kilichotokea," alisema Jaji Werema.
Kwa muda mrefu Chadema kimekuwa kikishinikiza kufanywa uchunguzi wa mauaji kadhaa ambayo kinadai kuwa yalifanywa na polisi katika sehemu mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na Arusha, Tabora na eneo la Mgodi wa Nyamongo mkoani Mara.
Lema, akiwasilisha maoni ya kambi ya upinzani juzi, alihoji sababu za kutoundwa kwa mahakama za uchunguzi wa mauaji hayo.
Alisema uundwaji wa mahakama hizo ni utekelezaji wa matakwa ya Sheria ya Uchunguzi wa Vifo (The Inquest Act) Sura ya 24 na kwamba Waziri Mkuu wakati anahitimisha mjadala kuhusu Bajeti ya ofisi yake, alikubaliana na ushauri wa kambi ya upinzani kwamba Serikali itaanzisha mahakama ya kuchunguza mauaji hayo.
"Kambi rasmi ya Upinzani inachotaka sasa ni kuona utekelezaji. Je, ni lini waziri mwenye dhamana atatangaza uteuzi wa kuundwa kwa mahakama hiyo katika Gazeti la Serikali ili wauaji wahukumiwe? Tunataka uchunguzi ufanyike haraka ili haki itendeke mapema," alisema Lema.
Kwa mujibu wa Sheria ya Uchunguzi wa Vifo, Sura ya 24 ya Sheria za Tanzania, kifo chochote ambacho kimetokea katika mazingira ya shaka kinatakiwa kuchunguzwa. Uchunguzi huo ni pamoja ule wa kidaktari ili kubainisha sababu halisi ya kifo husika na hatua ya pili ni uchunguzi wa kimahakama kwa kutumia mahakama ya korona ili kujiridhisha kwamba kifo hicho hakijatokana na vitendo au sababu za kijinai.
Mwananchi
Katika hatua nyingine, Werema amekiri bungeni kwamba Serikali imekuwa dhaifu kwa kutochunguza vifo vya raia ambavyo vimekuwa vikitokea katika mazingira yenye utata na kuahidi kwamba taratibu zinafanywa ili uchunguzi ufanyike.
"Nakiri kwamba tulilegalega kidogo kwa kutofanya uchunguzi wa mauaji yaliyotokea bila kujua sababu zake, lakini tumejiandaa shughuli hiyo itaanza karibuni".
Alisema uchunguzi wa vifo hivyo utafanywa na Mahakama za Korona (Coronerยs Court) ambazo zilikwishaundwa tangu mwaka 2004 kwa Tangazo kwenye Gazeti la Serikali namba 252 la Julai 16, 2004.
"Jaji Kiongozi kwa kushirikiana na Jaji Mkuu waliwateua mahakimu wote wakazi kuwa makorona (viongozi wa Mahakama za Korona), hivyo watu wa kufanya kazi hii (ya uchunguzi) wapo. Tutatumia taarifa hizi zilizotolewa, ipo ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora na yingine ili kujua nini hasa kilichotokea," alisema Jaji Werema.
Kwa muda mrefu Chadema kimekuwa kikishinikiza kufanywa uchunguzi wa mauaji kadhaa ambayo kinadai kuwa yalifanywa na polisi katika sehemu mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na Arusha, Tabora na eneo la Mgodi wa Nyamongo mkoani Mara.
Lema, akiwasilisha maoni ya kambi ya upinzani juzi, alihoji sababu za kutoundwa kwa mahakama za uchunguzi wa mauaji hayo.
Alisema uundwaji wa mahakama hizo ni utekelezaji wa matakwa ya Sheria ya Uchunguzi wa Vifo (The Inquest Act) Sura ya 24 na kwamba Waziri Mkuu wakati anahitimisha mjadala kuhusu Bajeti ya ofisi yake, alikubaliana na ushauri wa kambi ya upinzani kwamba Serikali itaanzisha mahakama ya kuchunguza mauaji hayo.
"Kambi rasmi ya Upinzani inachotaka sasa ni kuona utekelezaji. Je, ni lini waziri mwenye dhamana atatangaza uteuzi wa kuundwa kwa mahakama hiyo katika Gazeti la Serikali ili wauaji wahukumiwe? Tunataka uchunguzi ufanyike haraka ili haki itendeke mapema," alisema Lema.
Kwa mujibu wa Sheria ya Uchunguzi wa Vifo, Sura ya 24 ya Sheria za Tanzania, kifo chochote ambacho kimetokea katika mazingira ya shaka kinatakiwa kuchunguzwa. Uchunguzi huo ni pamoja ule wa kidaktari ili kubainisha sababu halisi ya kifo husika na hatua ya pili ni uchunguzi wa kimahakama kwa kutumia mahakama ya korona ili kujiridhisha kwamba kifo hicho hakijatokana na vitendo au sababu za kijinai.
Mwananchi