Serikali yakwaa kisiki Hospitali binafsi!

Naombea hii iwe kweli na kama private ni wazalendo wa kweli aoutomatically lazima wamejibu hivyo. Unajua huyu jamaa baada ya kuitwa dhaifu mara kibao chinichini mpaka waziwazi akafikiri kutokuwa dhaifu ni kutishia wanyonge na kuwapiga (kama alivyofanya kwa Dk Uli) akili ya kuku.
 
Wakurugenzi wa hospitali binafsi wamegoma kubeba mzigo wa serikali wa kuchukua wagonjwa kutoka hospitali za Public zilizoathiriwa na mgomo.

Serikali yapata jibu la kejeli... "Kama mnaweza kuwalipia wagonjwa private kwanini fedha hizo msitumie kuwalipa madaktari?"

Umeipata kutoka wapi hii habari? Walifanya mkutano au waliandikiana barua? Substantiate plz!
 
Wakurugenzi wa hospitali binafsi wamegoma kubeba mzigo wa serikali wa kuchukua wagonjwa kutoka hospitali za Public zilizoathiriwa na mgomo.

Serikali yapata jibu la kejeli... "Kama mnaweza kuwalipia wagonjwa private kwanini fedha hizo msitumie kuwalipa madaktari?"

Baba Mwanaasha dhaifu sana hata wa fikra! Bravo Drs
 
Jeuri, dharau, unafiki na uroho wa viongozi wa Tanzania ndiyo itakayoliangamiza Taifa letu. Haiingii akilini watu wanadai kuboreshwa kwa mazingira ya utoaji wa huduma muhimu kama afya na elimu; wanatokea viongozi wachache tena kwa kiburi na jeuri wanasema hakuna fedha ama liwalo na liwe lakini wanakuwa na jeuri ya kusema wanaodai waondoke kwani wana fedha za kutosha kuagiza madaktari wa nje ama kuingia ubia na hospitali binafsi. Hivi kwa uelewa wao finyu wanafikiri hospitali binafsi wanapata wapi madaktari kwa ajili ya shughuli zao.

Nafikiri imefika wakati Watanzania tuoneshe umoja wa hali ya juu kwani kiburi cha hawa viongozi ni matokeo ya kugawanyika kwetu na uhuru walioachiwa katika kukomba rasilimali za Taifa letu. Leo hii tunaambiwa kuwa kuna viongozi wanamiliki mabilioni na matrilioni ya shilingi kwenye akaunti za nje lakini watanzania wanakufa kwa kukosa madawa ama huduma nyingine za msingi kama elimu na maji.

Rais wa nchi anasafiri kiholela na msafara wa watu zaidi ya hamsini pasipo kufikiri hali ya wananchi wake; rais kama huyo atakuwa na huruma kwa wananchi wake kweli?? Gharama kwa safari moja ya rais ingeweza kuboresha huduma ya zahanati ngapi hapa Tanzania.

Hata pale wanapougua wao huwahishwa India na kwingineko kwa ajili ya kupata huduma ya daraja la kwa tena kwa gharama ya fedha za walipa kodi, mtanzania mnyonge atapata wapi huduma kama hiyo kama sio kuishia kwenye miti shamba na kwenye vikombe kama ilivyotokea Samunge huko Loliondo.
 
Habari za kuunda hizi, private wanataka hela tu wao, siasa wamewaachia hao wa muhimbili.

Kweli mkuu hii habari niyakutoka kwenye mawazo ya mtu haina ukweli kabisa'imekuja hapa kufurahisha watu na ipate comment basi'private hospt zimefunguliwa kwa ajili ya pesa leo wakatae wagonjwa?haingii akilini kbs'
 
Si kweli kwamba serikali haina uwezo wa kuboresha mazingira ya utoaji huduma za afya. Shida ni kasumba ya kufanya siasa za kibabe, siasa za ki-mungu mtu. Wangejishusha na kuwa kama binadamu wa kawaida (no one is perfect) na kusiliza kwa dhati maoni ya walio chini yao tungeepuka hii kadhia.

Mkuu FJM soma hapa:

Mbatia ambaye pia ni mbunge mteule alisema kuwa tangu Julai mwaka jana mpaka Februari mwaka huu Serikali imepoteza zaidi ya Sh1.04 trilioni za misamaha ya kodi, fedha ambazo zingeweza kuongezwa katika fungu la fedha za maendeleo ambazo ni kidogo katika bajeti ya mwaka wa fedha wa 2012/2013.

Mbatia: Sera ya misamaha ya kodi itizamwe upya
 
Hiyo habari ya kweli mkuu? Yaani private hospitals zikatae kufanya biashara?????. Labda hizo hospitali hazipo TZ ninayoifahamu!!.

Kiazi sana wewe! Hakuna kufanya kjazi kwa mkopo, serikali imeshindwa lipa Drs wake itaweza lipa huduma za private? Hebu vaa chupi wewe
 
Umeipata kutoka wapi hii habari? Walifanya mkutano au waliandikiana barua? Substantiate plz!

[h=6] hospitali X .....Kama selikali Inaweza kulipia wagonjwa huku private kwanini wasitumie pesa hizo kulipa Madaktari? :
hospitali Y ......andiken contract vinginevyo NO, hospitali hizi zinajiendesha kibiashara.
hospitali Z........haijatoa jibu
[/h]
 
Wakurugenzi wa hospitali binafsi wamegoma kubeba mzigo wa serikali wa kuchukua wagonjwa kutoka hospitali za Public zilizoathiriwa na mgomo.

Serikali yapata jibu la kejeli... "Kama mnaweza kuwalipia wagonjwa private kwanini fedha hizo msitumie kuwalipa madaktari?"

Kimsingi,serikali ya rais jakaya kikwete haifai na haiwapendi wananchi wake,kwanini Rais kikwete anakubali kudanganyika?Mimi namshauri akae chini na atafakali kwamba kwani nchi hii anaiongoza yeye mwenyewe?
 
Habari za kuunda hizi, private wanataka hela tu wao, siasa wamewaachia hao wa muhimbili.

Lakini inakubidi utambue ya kuwa, hao waliopo private ndiyo walewale wa serikalini. Wengi katika muda wao binafsi huwa wanapractiz huko private. Na walio private jumla ndiyo kina Dr.Ulimboka. Sasa wameamua kubana kotekote.
 
Habari za kuunda hizi, private wanataka hela tu wao, siasa wamewaachia hao wa muhimbili.

Kwani wagojwa wanaopelekwa na serikali wanabeba cash? Au ni mambo ya tiba malipo baadae! jambo ambalo malipo huchukua muda sana kulipwa ambapo mwisho wa siku huduma katika hospitali za binafsi zitashuka kutokana nakuelemewa na mzigo wa madeni ambayo hayalipwi.
Sidhani kama watalikubali hilo. Kuikopesha serikali ni shughuli pevu kwenye malipo
 
Habari za kuunda hizi, private wanataka hela tu wao, siasa wamewaachia hao wa muhimbili.
Nani asiyejua kuwa ukitaka shirika lako lifilisike unaingia mkataba na serikali? serikali inaongoza kwa kudaiwa katika almost mashirika yote; Shirika la nyumba, Tanesco, Dawasa, n.k. Private hospital wanalijua hilo ndo maana hawawezi kuingia mkataba na serikali kwasababu wanajua watakuwa wanatumiwa tu na hawatapata pesa kama unavyofikiri.
 
hospitali X .....Kama selikali Inaweza kulipia wagonjwa huku private kwanini wasitumie pesa hizo kulipa Madaktari? :
hospitali Y ......andiken contract vinginevyo NO, hospitali hizi zinajiendesha kibiashara.
hospitali Z........haijatoa jibu
jk angekaa nao magogoni halafu later on awapeleke apollo huko wanakotibiwa wao! pathetic kwa kweli
 
Safi, kwa nini wabebe mzigo wa serikali?
Kwani wastaafu hawatoshi?
 
Sidhani kama madaktari walisimamia 3.5Ml kama mshahara wa kuanzia. Walikuwa wanahitaji kufikia muafaka lakini pia ni pamoja na vifaa muhimu vya hospitali ili kuongeza ufanisi wa huduma yenyewe.
 
Sasa hii kali kwa kuwa dada yangu kapokelewa regency bila tatizo hio wamegoma kuwapokea imetoka wapi.....mtakufa na roho mbaya zenu na kuwaunga mkono hao vibaraka wa ibilisi wanaojiita madaktari kumbe wanasaidia kuuwa watu
 
Back
Top Bottom