Serikali yajibu Hoja za Kivuko cha MV Dar es Salaam na Uuzwaji wa Nyumba Zake

MV Dar Es Salaam maarufu kama Meli Chakavu, ilinunuliwa na Waziri wa Ujenzi wa kipindi hicho, Mh. Magufuli, kwa fedha za wapiga kura na Walipa kodi wa Tanzania, kiasi cha Tsh bilioni 7.9, Pamoja na kununuliwa kwa kiasi hicho cha fedha, meli hiyo ni mbovu hivyo kushindwa kufanya kazi kwa viwango vilivyokusudiwa. Inaelea Elea kwenye Bahari ya Hindi bila kurudisha gharama za Fedha za wapiga kura na Walipakodi wa Tanzania.

Uuzwaji wa nyumba za Umma kwa bei chee, nao ulifanywa na Mh. Magufuli. Nyumba hizo ni mali za wapiga kura na walipakodi wa Tanzania.

Kwa sababu yeye sasa ni raia namba moja, Basi atumbuliwe kwa Ufisadi huu.
Mmh kwakweli
 
atumbukizwe kisimani fisadi wa mv hoihoi na muuzaji wa masinagogi kwa dotto na mussa, huyu ni mpiga dili mkuu huko jamaicani..
 
Watu mkishavunja vibubu vyenu vya mwaka mnakuwa huru sana kwenye kutoa maoni yenu.
Ni matumaini yangu mnayo ile ada ya uchochezi.
Usilete vitisho kwani havisadii. Kutumia nguvu za polisi ni mbinu zilizotumika na wakoloni. Tulishatoka huko. Kwani nyie ni malaika hamsemwi? Mbona wengine mnawasema hampelekwi mahakamani? Tusiposema sisi hata nawe yatasema. Kishfa ni sawa na pembe LA ng'ombe halifichiki
 
Usilete vitisho kwani havisadii. Kutumia nguvu za polisi ni mbinu zilizotumika na wakoloni. Tulishatoka huko. Kwani nyie ni malaika hamsemwi? Mbona wengine mnawasema hampelekwi mahakamani? Tusiposema sisi hata nawe yatasema. Kishfa ni sawa na pembe LA ng'ombe halifichiki
Nitake radhi kwa kunichanganya nao.
 
“Ni kweli kivuko kina mapungufu ikiwamo kasi ndogo, lakini hakuna ukiukwaji wowote wa taratibu wakati wa ununuzi. Temesa ilitangaza zabuni na baada ya maombi kupitiwa, kampuni ya MS Jones Gram Hansen ilishinda zabuni hiyo kwa kuwa na bei nafuu,” alisema Profesa Mbarawa.
Hapa ndipo kwenye shida hiyo inaitwa"Kanyaboya au Mkenge" na watoto wa mujini!Kitu kilichonunuliwa hakikidhi thamani halisi.
 
Watanzania tumezoea kusikia maneno mengi, wapo waliosema ndege ni mitumba tena watu wenye heshima kwenye chama Fulani. Ninawasiwasi kama kweli kivuko hicho ni mtumba maana serikali makini hainunui mitumba hata kidogo.
 
Hahahahaha.....sio khikhi mkuu ila kuna ukweli kwamba propagandists na strategies zenu against Magu zimekuwa zina zero effect kwenye community tofauti na hapo nyuma...labda mkibadili mwenyekiti wenu.
Nahisi una pepo upelekwe kwa lusekelo
 
The guilty are always afraid. Kwa kuwa hawana namna sahihi ya kujibu huja hukimbilia policcmmmm ili wawasaidie. Jibuni hoja
 
Mmh kwakweli


Serikali imejibu hoja za upinzani kuhusu uuzwaji wa nyumba za Serikali na kutetea ununuzi wa kivuko cha MV Dar es Salaam ambacho kilitakiwa kufanya safari zake kati ya Dar na Bagamoyo.

Hoja hizo ziliibuliwa katika hotuba ya Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani kwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, James Mbatia akitaka kutekelezwa kwa azimio la Bunge la urejeshwaji wa nyumba hizo serikalini lililotolewa Aprili 2008.

Pia, ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ilibainisha upungufu katika kivuko cha MV Dar es Salaam ambao ni kutolipiwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), kutokuwa na kasi kadri ya mkataba na kutokuwapo hati ya makabidhiano.

Hoja hizo za upinzani zilijibiwa juzi jioni na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa ambaye alisema hakuna taratibu zozote zilizokiukwa wakati wa ununuzi wa kivuko hicho ambacho kwa zaidi ya mwaka hakijaanza kazi.

Alisema wizara ilipata taarifa ya CAG ambayo ilibainisha upungufu kadhaa ikiwa ni pamoja na kivuko hicho kununuliwa kwa Dola za Marekani 4.9 milioni (Sh7.9 bilioni) bila kulipiwa VAT, lakini akasisitiza kwamba hakukuwa na ukiukwaji wowote wa taratibu za ununuzi.

“Ni kweli kivuko kina mapungufu ikiwamo kasi ndogo, lakini hakuna ukiukwaji wowote wa taratibu wakati wa ununuzi. Temesa ilitangaza zabuni na baada ya maombi kupitiwa, kampuni ya MS Jones Gram Hansen ilishinda zabuni hiyo kwa kuwa na bei nafuu,” alisema Profesa Mbarawa.

Alisema baada ya kivuko kuletwa nchini Desemba 2014, kilifanyiwa majaribio na kubainika kwamba hakikuwa na kasi ya kuridhisha. Alisema makubaliano yalikuwa ni kujenga kivuko chenye kasi ya nots20, lakini hicho kilikuwa na kasi ya nots 15.7.

Kutokana na hali hiyo, alisema Serikali ilimtaka mkandarasi kurekebisha kasoro hiyo kwa gharama zake na kuwa ameshawasilisha andiko juu ya namna atakavyoifanya kazi hiyo.

“Mpaka sasa mzabuni huyo hajalipwa asilimia 10 ya malipo yaliyokubaliwa mpaka pale atakapokamilisha kazi hiyo. Kwa hiyo, taratibu zote zilifanyika kwa mujibu wa sheria,” alisema.

Kuhusu nyumba, Profesa Mbarawa alisema Serikali iliidhinisha mpango huo Aprili 24, 2008 baada ya kupata ridhaa ya Bunge ilipopeleka suala hilo kujadiliwa.

“Suala la uuzwaji wa nyumba za Serikali, pia taratibu zilifuatwa. Serikali ilileta mpango huo bungeni na kupata ridhaa ya wabunge wote. Kwa hiyo, niwaambie tu wabunge kwamba suala hili lilipata baraka zao,” alisema waziri huyo.

Uuzwaji wa nyumba za Serikali na ununuzi wa kivuko cha Mv Dar es Salaam vilifanyika wakati Rais John Magufuli akiwa waziri wa ujenzi kwa nyakati tofauti.

Kambi ya upinzani imekuwa ikisisitiza kwamba kuna ukiukwaji wa sheria uliofanyika wakati wa uuzaji wa nyumba na ununuzi wa kivuko hicho. Hata hivyo, Serikali imeshikilia msimamo wake kwamba sheria zilifuatwa.
Hiii inanikumbusha neno la mtukufu malaika "wapiga dili" wakati yeye ndiye mpiga dili maarufu kwa kununua mkangafu wenye speed ndogo kuliko baiskeli ya miti. Tukisema kala cha juu tunaitiwa polisi watukamate
 
Mwalimu aliwahi kusema ile ofisi ni mahali patakatifu ambapo hapafai mtu kama una kasoro hata kidogo kupakimbilia. Aibu zako zote zitajulikana waziwazi
 
Kama mlivyomsamehe fisadi Lowasa na kumuuzia chadema hata sisi watanzania wenye akili tulishamsamehe Magufuli na tutamchagua kuwa rais Milele ili aendelee kuwatumbua hapo ufipa maana mmejimilikisha mashamba na hamlipi kodi za wananchi
Kweli watu mnajisahau sasa hivi mnataka raising wa milele hujui kuwa kuna katiba
 
Mh Mbarawa ni makini na shupavu bt ktk hil umemezeshwa majbu ya mawaziri waliopita hakuna hapo ulichokijbu wew naamin ivo,majibu mepesi mpaka yanatia hasira,nakushaur kwa residents zaina hzi uwe wakausha usilishwe majbu unajitoa thamani.
 
Back
Top Bottom