Serikali yahumiwa, wazuia malipo yote

Serikali yahumiwa, wazuia malipo yote

Calipso

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2009
Posts
284
Reaction score
15
Leo nimeingia kwenye ofisi moja kudai malipo,na nilikuwa nishataarifiwa kuwa malipo yapo tayari baada ya wiki niende,ile wiki imetimia leo,nikatia timu saa tatu asubuhi ya leo hii, majibu niliyoyapata ni haya,kwa kuwa jamaa nafahamiana nae akanipa ukweli.. nanukuu.. Mkuu wangu kweli nilikupa taarifa uje baada ya wiki lkn hali imebadilika hafla,angalia huu waraka wa serikali unatwambia tusifanye malipo ya aina yoyote,na pesa yote irudi kwa ajili ya shughuli maalum. mwisho wa kunukuu. jamaa akanipa kidogo za ndani akaniambia ccm hawakutegemea hali kama itakuwa ngumu hivi,sasa wameamua kuchukua nguvu za ziada kwani hawana tena uhakika wa kushinda kama walivotegemea. jamani pesa zetu hizoooooooooo
 
Kama kuna mtu wa kuweza kutuwekea copy ya waraka huo pls.
 
Hata mimi nimesikia kuwa kwenye mawizara huko mambo hayaendi pesa zimekuwa directed kwenye uchaguzi. Ufisadiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii. Slaa ingilia kati hii nchi inafia mikononi mwa wezi.
 
Hata mimi nimesikia kuwa kwenye mawizara huko mambo hayaendi pesa zimekuwa directed kwenye uchaguzi. Ufisadiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii. Slaa ingilia kati hii nchi inafia mikononi mwa wezi.
mwe pesa zetu hizooo! Slaa akiiingia hakuna kitu!
 
mwe pesa zetu hizooo! Slaa akiiingia hakuna kitu!

NCHI HII INAPESA NYINGI MNO, NA HAO WEZI WANA PESA NYINGI WAMEZIWEKA KWENYE MABENKI YAO, WATAITWA MMOJAMMOJA NA KESI NDANI YA WIKI IMEISHA NA WATANZANIA TUNACHUKUA CHETu
 
Hawana uhakika wanaanza kugawana Dr.SLAA atakuta hamna hazina pesa imegawanwa.inabidi tupate evidence tuiweke wazi watanzania wasikie
 
Mimi sina uhakika na hili,inawezekana huu ni uzushi!tuseme mambo ya kweli washikaji!hii nahakika si kweli!
 
Mimi sina uhakika na hili,inawezekana huu ni uzushi!tuseme mambo ya kweli washikaji!hii nahakika si kweli!

Mkuu hii ni kweli. Mtu wangu wa karibu yuko wizara fulani anasema hali ni mbaya, hakuna pesa hata safari za muhimu hakuna labda za Pinda kumwakilisha Kikwete tu ndo zinapataikana. CCM wanatumia pesa zetu kwenye kampeni zao, sijui baada ya EPA hii itaitwaje. Ngoja tusubiri.
 
Sioni la ajabu CCM ilishatamka sio mara moja mara nyingi tu na viongozi mbali bali kuwa watatafuta ushindi kwa hali yoyote na gharama zozote hivyo ikiwa plan A inashindikana watakwenda plan B nayo ikishindikana wataingia plan C ya Mzee Mugabe kubakia madarakani kwa hali yoyote.Sahau mambo ya fair play .
 
WANDUGU,

MBONA HIZI NYEWS ZINAENDANA KABISA NA UKWELI UNAZIDI KUPASUKA....CHEKINI HII THREAD WA AWALI ILIYOPO CHINI...THEN CONNECT THE DOTS, YOU GET WHAT IS HAPPENING INSIDE THE GOVT...NAONA KUNAWAKA MOTO!

"Quote Originally Posted by Kimweri View Post - JAMIIFORUMS

Kwa wale mlio Tanzania mnafahamu kuwa kwa miezi miwili sasa,wafanyakazi wa serikali wamekuwa wanakatwa mishahara yao,na fedha zinadaiwa kupelekwa kwenye kampeni.majibu ya serikali ni kuwa kuna tatizo kwenye system ya ulipaji wa mishahara(c'mon!).
Wafanyabiashara wakubwa na wakati wamelazimishwa kuchangia si chini ya 50M kugharamia kampeni za CCM(CCM kanusheni hili).wengi ninaowafahamu wamekiri na ahadi yao ni kurudisha gharama zao baada ya uchaguzi(watazirudishaje?)
Wakuu wa idara zote za serikali wame-amriwa kurudisha OC serikalini,pamoja na mafungu yote ya serikali kwenda kwenye idara za serikali yamezuiwa kwa miezi mi-2 sasa.kwa kifupi idara za resikali ziko ICU kugharamikia uchaguzi.
wakuu wa vitengo serikalini wameamriwa kuchangia 2M kwenda kwenye kampeni za CCM,kama kuna mkuu wa kitengo hapa athibitishe hilo.
Safari/warsha/semina/posho za aina zozote zile zimezuiliwa huko serikalini,wafanyakazi wa serikali ni mashahidi wa hili,wachache sana wanaopata fedha hizo, hadi zithibitishwe na makatibu wakuu wa wizara kwa amri maalum toka Ikulu.(je walikuwa wapi kudhibiti matumizi ya fedha za serikali miaka mi 4 iliyopita?kwa nini wazuie hadi matumizi ya msingi?).
Ni ukweli ulio wazi kabisa kuwa sehemu pekee inayotumia fedha za serikali sasa ni IKULU.hivi uchaguzi si ulitengewa bajeti yake?kwa nini nchi nzima iichangie IKULU/HAZINA kufanikisha uchaguzi?
Je?

1. wafanyakazi wa Tanzania wana sababu gani kuipigia kura serikali isiyowajali kwa kiasi hiki?
2. Ndugu na jamaa wanaowategemea wafanyakazi hawa kwa maisha yao ya kila siku wana sababu gani ya kuendelea kuikumbatia CCM?
3. CHADEMA,CUF,TLP,kwa nini msitumie mwanya huu mkubwa kabisa kujenga hoja ya matumizi mabovu ya fedha za UMMA kwenye uchaguzi huu yanayofanywa na CCM?



nionavyo mimi wafanyakazi kadhaa nilioongea nao,si chini ya kumi,wamekata tamaa ya maendeleo chini ya CCM,wengi wanataka mabadiliko,wako tayari kumpigia slaa kura hata kama hawampendi/hawamkubali ili mradi mabadiliko yatokee(CHADEMA mnalijua hili?)

makada wa chadema,fanyeni hima kusambaza hizi taarifa kuwa wafanyakazi wanakatwa mishahara kufidia gharama za CCM

PIA MUWAULIZE CCM/KIKWETE sababu za kutumuia fedha karibu zote za serikali kugharamia UCHAGUZI tu!kuna sababu gani mpiga kura akanunuliwa kwa fedha nyingi kiasi hicho? "
 
Leo nimeingia kwenye ofisi moja kudai malipo,na nilikuwa nishataarifiwa kuwa malipo yapo tayari baada ya wiki niende,ile wiki imetimia leo,nikatia timu saa tatu asubuhi ya leo hii, majibu niliyoyapata ni haya,kwa kuwa jamaa nafahamiana nae akanipa ukweli.. nanukuu.. Mkuu wangu kweli nilikupa taarifa uje baada ya wiki lkn hali imebadilika hafla,angalia huu waraka wa serikali unatwambia tusifanye malipo ya aina yoyote,na pesa yote irudi kwa ajili ya shughuli maalum. mwisho wa kunukuu. jamaa akanipa kidogo za ndani akaniambia ccm hawakutegemea hali kama itakuwa ngumu hivi,sasa wameamua kuchukua nguvu za ziada kwani hawana tena uhakika wa kushinda kama walivotegemea. jamani pesa zetu hizoooooooooo

Mkuu asante sana lkn tafadhali rudi kwa huyo jamaa, mwombe akupe copy ya waraka huo ili uwekwe jamvini. Waraka huu utamsaidia DR SLAA ktk kampeni
 
Labda mimi nna bahati,, sijakatwa chochote,angalieni isije kuwa mlikua na madeni.
 
Tusaidieni jamani mlioko serikalini... kama kuna nakala ziwekeni kiaina jamvini ili tuzidadavue
 
Safari/warsha/semina/posho za aina zozote zile zimezuiliwa huko serikalini,wafanyakazi wa serikali ni mashahidi wa hili.....

Bla bla tupu na uongo mwiiingi. Mbona wengine wanasafiri vizuri tu na mishahara wanapata kwa wakati?

Tusiwe waoga na kukumbatia kila uvumi. Nov haiko mbali, JF itagundua kuwa imekuwa ikijidanganya saaana kwa mambo ya kufikirika. Watanzania wataamua na itakuwa ni final.
 
Asilimia 85 ya miradi ya serikali imesimama unless contractor atumie hela yake kisha baadae aje kulipwa. Ila si dalili nzuri kwa serikali iliyo madarakani kwani ni dhahiri maslahi yao wameweka mbele kuliko maendeleo ya Taifa ndiyo maana hela zote za maendeleo wamepeleka kwenye uchaguzi huku pia wafadhili kama kawaida wametoa fedha kwa ajiri ya uchaguzi (sijui wame-fund kiasi gani). januari lazima kutakuwa na
mini-budget ili shughuli ziendelee, TOO BAD TO OUR POOR NATION HOW ARE WE GOING TO DEVELOP
 
Back
Top Bottom