Serikali yafuta ongezeko la kodi mbalimbali

Serikali yafuta ongezeko la kodi mbalimbali

Mpaka Kieleweke

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2007
Posts
4,132
Reaction score
1,580
Mgimwa anasema baada ya kubanwa sana jana serikali imeamua kuondoa ongezeko la kodi iliyokuwa imependekezwa kwenye mafuta .

mtakumbuka michango ya wabunge makini Mdee, Mnyika , Lissu jana , imewafanya kuondoa ongezeko hilo.
 
Lete taarifa kamili bana, tuanza kukokotoa inakuwaje man!
 
Mgimwa anasema baada ya kubanwa sana jana serikali imeamua kuondoa ongezeko la kodi iliyokuwa imependekezwa kwenye mafuta .

mtakumbuka michango ya wabunge makini Mdee, Mnyika , Lissu jana , imewafanya kuondoa ongezeko hilo.

Kwenye mini bajeti atairudisha akidai anafukia mashimo bila ya kutuelezea ni nani kayachimba.

Kodi za magari chakavu bado ni kero hasa kwa mitambo mikubwa ambayo na huu umasikini wetu hatuna jinsi. pia ongezeko la vehicle licence ni wizi wa mchana kweupe kabisa. Yawaje gari lilelile lilundikiwe kodi kibao? Double taxation is unconstitutional.............and sinful! Nifahamuvyo siyo cdm tu waliolia na kibanio cha kodi. By the way are u sympathetic na hawa magwanda hadi ukawavika vilemba vya ukoka?
 
Ni kuwa zile kodi mpya za mafuta , isipokuwa ile ya fuel levy ambayo ni shilingi 50 per litre haikuondolewa ila zile nyingine za mafuta zimeondolewa ktk mswada wa sheria ya fedha, hiyo ya fuel levy ni kwa ajili ya kupeleka nishati vijijini kupitia REA , sheria ya fedha imepitishwa muda huu.
 
Na kuanzia July mosi huo mziki wa bima za magari haufai! Eti lori la canter au kitipa cha mchanga nilichokuwa nalipia 80,000 third party sasa natakiwa kiulipia 750,000! kwa mwaka! Hapa serikali ya CCM imegusa watu wa kati ambao ndio wengi tunaoibeba!
 
Na kuanzia July mosi huo mziki wa bima za magari haufai! Eti lori la canter au kitipa cha mchanga nilichokuwa nalipia 80,000 third party sasa natakiwa kiulipia 750,000! kwa mwaka! Hapa serikali ya CCM imegusa watu wa kati ambao ndio wengi tunaoibeba!
Bora mguswe ili muugulie maumivu labda mtaelewa nini maana ya kuwa na viongozi Mafisadi...
 
Ushindi kwa CDM si ktk box la kura tu, hata CCM wanapoiba kura na kuonekana washindi, huja kushidwa ktk hoja za maendeleo na kiuchumi.Kila mbunge aliukubali muswada wa fedha wa CDM
 
Mgimwa anasema baada ya kubanwa sana jana serikali imeamua kuondoa ongezeko la kodi iliyokuwa imependekezwa kwenye mafuta .

mtakumbuka michango ya wabunge makini Mdee, Mnyika , Lissu jana , imewafanya kuondoa ongezeko hilo.

umewaona hao wabunge watatu pekee au ndo kuzimikia watu.
 
jamani vipi kuhusu vehicle license? hasa kwa vyombo vya moto vyenye cc less than 500? mtoa mada ulitakiwa kufunguka vyakutosha.
 
Wanafanya hivyo sababu hawana misaada ya ulaya ule mpango wa GBS kufikia 2015 utakuwa umefungwa, kwa sasa wanamalizia tu,Tanzania sijajua kama tulipima sawasawa kuwashiti wazungu na kuelekeza nguvu kwa mchina wakati tunajua sustainability in term of income ni questionable.wachina hawahusiki na social responsibility wao ni biashara.Kama unataka budget support yeye haimhusu, sasa leo eti wazungu tunawaona hawafai zaidi ya mchina.

Miradi mingi ni ndoto kukamilika EU hawatoi tena pesa kwa wakati kwani wamegundua they are no longer honey to Tzania.
 
Ni kuwa zile kodi mpya za mafuta , isipokuwa ile ya fuel levy ambayo ni shilingi 50 per litre haikuondolewa ila zile nyingine za mafuta zimeondolewa ktk mswada wa sheria ya fedha, hiyo ya fuel levy ni kwa ajili ya kupeleka nishati vijijini kupitia REA , sheria ya fedha imepitishwa muda huu.

Vipi kuhusu kodi ya SIM card (1000/-) kila mwezi nayo imepita?. Halafu vipi kuhusu ushuru wa magari ambayo serikali inayaita chakavu, ile 25% badala ya 20% ya mwanzo kwa magari yenye umri wa zaidi ya miaka 10 tangu kutengenezwa nayo imepita?. Je kuhusu kodi ya kuhamisha fedha, Mpesa, tigo pesa n.k nazo zimepita?. Ama kweli CCM WAMACHOKA HADI KUFIKIRI. Sasa watanzania ndo akili itawaingia na kujua kuwa nchi imeshauzwa.
Naomba nisaidie kujua haya machache tafadhari.
 
vp cm maana hapo kwny kutuma hela kwa cm itakuwa balaa na wanaoathirika zaidi wale wanotuma elfu kumi au kumi na tano wa laki saba milion moja wala hawaumii si wanazo hata akikatwa elfu tano haoni uchungu.
 
Kwenye mini bajeti atairudisha akidai anafukia mashimo bila ya kutuelezea ni nani kayachimba. Kodi za magari chakavu bado ni kero hasa kwa mitambo mikubwa ambayo na huu umasikini wetu hatuna jinsi. pia ongezeko la vehicle licence ni wizi wa mchana kweupe kabisa. Yawaje gari lilelile lilundikiwe kodi kibao? Double taxation is unconstitutional.............and sinful! Nifahamuvyo siyo cdm tu waliolia na kibanio cha kodi. By the way are u sympathetic na hawa magwanda hadi ukawavika vilemba vya ukoka?
Yaani ukweli unaujuwa umeusikia na kuuona lkn you cant appreciate? Ndio tatizo la magamba mnaunga mkono hoja kama kilaza mmoja toka kwa magamba wenzako jana anasema naunga mkono asilimia mia 200 halafu malalamiko kibao, hata hapa unalaumu mambo ya msingi na unasema ni unconstitutional lkn moyo uko huko huko kwa magamba hata aibu huna.
 
Vipi kuhusu kodi ya SIM card (1000/-) kila mwezi nayo imepita?. Halafu vipi kuhusu ushuru wa magari ambayo serikali inayaita chakavu, ile 25% badala ya 20% ya mwanzo kwa magari yenye umri wa zaidi ya miaka 10 tangu kutengenezwa nayo imepita?. Je kuhusu kodi ya kuhamisha fedha, Mpesa, tigo pesa n.k nazo zimepita?. Ama kweli CCM WAMACHOKA HADI KUFIKIRI. Sasa watanzania ndo akili itawaingia na kujua kuwa nchi imeshauzwa.
Naomba nisaidie kujua haya machache tafadhari.
mimi nataka kujua kuhusu pombe nayo imepita??
 
Back
Top Bottom