Mkuu hii vita nini hasa aim yake maana wame patanishwa na dunia still wanekaza fuvu, halafu kuna habari ilikuwa A journal kuwa huko Doha congo ilikuwa inatuma unauthorised people kwenye mazungumzo kwa nini hao waasi au hata Qatar ilikuwa inawapokea? Then yule mmarekani anasema watasaini mkataba? This time around tutaona mengi ila marais wengi wa Afrika wana moto wao wa peke yao.
Kumbuka DRC inasemekana kuwa ndo nchi tajiri wa madini duniani kote.
Na madini yote yanayohitajika, yapo pale pale, hasa mashariki mwa nchi hiyo.
Ukweli utabaki kuwa pale pale, Afrika mashariki imeshakuwa na Israel yake. Na baba ni yule yule. Na yupo kimasrahi zaidi.
Sasa hivi, inasemekana tena maraisi watatu,walihusika kupewa madaraka kwa Big pale DRC. Hili nalo limeibuka, na linaibua mengi. Yumo wa Kenya, wa Egypt na wa South Africa. Wote hawa, kuna mikataba ilisainiwa, na ndo inaenda kuumbuka.
Mi nasemaga, DRC ilishajikaanga yenyewe, siku iliyokubali kusign mikataba.
Kwa sasa, ya DRC ni sawa na ya Russia na Ukraine kwa upande mwingine. Wa Congoman wanaozungumza Kinyarwanda, huwezi watofautisha. Ni kama masai wa Kenya, useme umtofautishe na wa Tanzania. Hivyo, hata kwenye siasa na jeshi, ni ngumu lile eneo kukaa sawa. Rais wa DRC hana nguvu ya kupambana na wanajeshi.
Dunia hii, inaendeshwa kinafiki kupita maelezo. Ukraine washikaji walishapata contracts zao, na yenyewe inazidi kuteketea.
Na huku, usitegemee US italeta jeshi la kucover nchi yote. Penye masrahi yake, mwenye uhakika wa usalama, ndo watadeal nae. Full stop.
Kuna issue ya FDLR, kwamba inatakiwa kwanza inyanganywe silaha.
FDLR, kwenye wazalendo, serikalini, jeshini, imo. Si kazi ndogo kuiangamiza. Miaka 31, walishaenea nchi nzima. Mpaka uhakika wa wameisha upatikane, si kesho wala keshokutwa.
Mpaka Rwanda inatangaza yote yale, inajua inachokiongelea, na wapi walipo. Kwa sasa, baada ya pale, walio wengi walianza kuhamia Burundi. Kumbuka, na Burundi haina mahusiano mazuri na Rwanda.
Sasa basi, unadhani wa kuihifadhi na akawa na amani ni nani?