Serikali: Watumishi 4,160 walioondolewa kwa vyeti feki warudishwa

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Naibu Waziri – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe Dkt. Mary Mwanjelwa amesema watumishi wa umma 4,160 kati 15,189 walioondolewa kazini kwa kuwa na vyeti vya kughushi wamerudishwa.

Dkt. Mwanjelwa amesema Serikali imechukua hatua hiyo baada ya kubainika kuwa Watumishi hao waliondolewa kimakosa.

====

NAIBU Waziri wa Nchi, Ofi si ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Dk Mary Mwanjelwa amesema watumishi 4,160 walioondolewa katika mchakato wa kuwaondoa wenye vyeti feki wamebainika kuondolewa kimakosa au kwa uonevu na wamerejeshwa kazini.

Dk Mwanjelwa aliyasema hayo bungeni jana wakati wa kujibu swali la Mbunge wa Musoma Mjini, Vedastus Manyinyi (CCM) na kuongeza kuwa kati ya watumishi waliorejeshwa kazini, watumishi 3,057 ni watendaji wa vijiji, mtaa na kata.

Katika swali lake, Manyinyi alisema serikali katika kuhakikisha inapata watumishi bora wenye sifa, iliamua kuwaondoa watumishi wasio na sifa pamoja na wenye vyeti feki, hivyo alitaka kujua ni kwanini serikali isiunde timu maalumu ili ipitie kila halmashauri kupitia taarifa juu ya zoezi hilo ili haki itendeke hasa kwa wale ambao hawana uwezo wa kwenda wizarani.

Pia alitaka kujua kama serikali haioni kuwa watumishi waliojiendeleza kielimu zaidi ya darasa la saba na wameondolewa kwa kosa la udanganyifu kuwa ni bora kuliko ambao hawajajiendeleza. Akijibu maswali hayo, Dk Mwanjelwa alisema katika zoezi hilo watumishi 15,189 walibainika kuwa na vyeti vya kughushi na kuondolewa kwenye orodha ya malipo ya mshahara.

Alisema baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa watumishi na vyanzo vingine kuhusu watumishi kuondolewa kimakosa au kwa uonevu katika orodha ya mishahara, serikali imekuwa ikifanya ufuatiliaji wa karibu ikiwa ni pamoja na kuunda timu za ufuatiliaji wa utekelezaji wa zoezi hilo.

PIA, SOMA:
-
Orodha ya Watumishi wenye vyeti vya Kughushi
 
Hata wenye vyeti mishahara ipo vile vile.

Madaraja kupanda halmashauri in mtihani mzito. Kuna baadhi ya kada eti mpaka madiwani wakae. Sasa muda umefika bajeti imetangazwa kinasubiriwa kikao cha madiwani.

Nchi yetu nzuri sana Tanzania.
 
Naibu Waziri – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe Dkt. Mary Mwanjelwa amesema watumishi wa umma 4,160 kati 15,189 walioondolewa kazini kwa kuwa na vyeti vya kughushi wamerudishwa.

Dkt. Mwanjelwa amesema Serikali imechukua hatua hiyo baada ya kubainika kuwa Watumishi hao waliondolewa kimakosa.

Weka orodha ya waliorudishwa ili kujiridhisha kama sio kupendelea hawa na kuwaumiza wale.
 
Umakini katika serikali na idara zake umeshuka sana katika awamu hii.

Nn tatizo?
 
Hao utakuta ni makada wa CCM wanarudishwa kuja kuiba kura ili CCM ishinde tena. Kwa hali hiyo wanaotii bila shuriti ndio hawa
 
Naibu Waziri – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe Dkt. Mary Mwanjelwa amesema watumishi wa umma 4,160 kati 15,189 walioondolewa kazini kwa kuwa na vyeti vya kughushi wamerudishwa

Dkt. Mwanjelwa amesema Serikali imechukua hatua hiyo baada ya kubainika kuwa Watumishi hao waliondolewa kimakosa
Tatizo la nguvu z kiume lemeltwa na serikali kwa kuwapunguza watu kazini ikachangia mawazo mpaka mdudu hanyanyuki
 
Naibu Waziri – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe Dkt. Mary Mwanjelwa amesema watumishi wa umma 4,160 kati 15,189 walioondolewa kazini kwa kuwa na vyeti vya kughushi wamerudishwa

Dkt. Mwanjelwa amesema Serikali imechukua hatua hiyo baada ya kubainika kuwa Watumishi hao waliondolewa kimakosa
Mimi namfahamu mmoja wizara ya elimu imepitisha kuwa vyeti vyake ni halali lakini shirika lake la umma limekataa kumpokea; maana yake ni kwamba wengine waliondolewa kwa hila kwa kutumia mgongo wa vyeti feki.
 
Back
Top Bottom