kichunachangu
Member
- Oct 17, 2015
- 97
- 20
Ni wito wangu kuwa watanzania wote,tutapiga kura na kurudi majumbani mwetu na hatutakuwa tayari kushiriki vitendo vyovyote vya uvunjifu wa amani
Acha ujinga, tutapiga kura tutalinda kura zetu. Na tutatunza amani kwa mujibu wa sheria.
Unalindaje?
Haikuhusu.. wewe kalale...
Wakati Taifa likisubiri uamuzi wa kesi ya mita 200 iliyofunguliwa Mahakama Kuu ya Tanzania na Amy Patience Kibatala, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe, ambaye Wizara yake inasimamia jeshi la polisi ametoa tamko. Chikawe amesema kuwa zipo Sheria zinazoruhusu kuwapo kwa maandamano na mikusanyiko, zikiwataka wanaotaka kufanya hivyo kupata kibali cha polisi.
"Ikiwa kituo cha kupigia kura kipo nyumbani kwako huwezi kuhama nyumba, ila hupaswi kufanya sherehe. Piga kura na tii Sheria ya Uchaguzi. Kwa watakaotaka kukusanyika, waombe kibali cha Jeshi la Polisi kama Sheria inavyowataka. Tunachohitaji ni kuwepo kwa amani wakati na baada ya kumalizika uchaguzi mkuu" alisema
Chanzo: Mwananchi la leo, ukurasa wa 1 na 3
Swali langu binafsi: Polisi watatoa vibali hivyo?
Wakati Taifa likisubiri uamuzi wa kesi ya mita 200 iliyofunguliwa Mahakama Kuu ya Tanzania na Amy Patience Kibatala, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe, ambaye Wizara yake inasimamia jeshi la polisi ametoa tamko. Chikawe amesema kuwa zipo Sheria zinazoruhusu kuwapo kwa maandamano na mikusanyiko, zikiwataka wanaotaka kufanya hivyo kupata kibali cha polisi.
"Ikiwa kituo cha kupigia kura kipo nyumbani kwako huwezi kuhama nyumba, ila hupaswi kufanya sherehe. Piga kura na tii Sheria ya Uchaguzi. Kwa watakaotaka kukusanyika, waombe kibali cha Jeshi la Polisi kama Sheria inavyowataka. Tunachohitaji ni kuwepo kwa amani wakati na baada ya kumalizika uchaguzi mkuu" alisema
Chanzo: Mwananchi la leo, ukurasa wa 1 na 3
Swali langu binafsi: Polisi watatoa vibali hivyo?