Serikali:tunapenda kujua hatma ya wale ''tuner-fish''

Serikali:tunapenda kujua hatma ya wale ''tuner-fish''

Teamo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2009
Posts
12,271
Reaction score
1,069
Wengi wetu tulifurahia ''uwingi'' wa tani za wale samaki gharama kabisa duniani ''tuna-fish'' waliokutwa kwenye meli ya wa-asia.

Wengi wetu huenda tulimfurahia sana magufuli kwa kile tunachoweza kuita ''kazi nzuri'' aliyoifanya

Wengi wetu pengine tulichekelea sana kuwaona wale waasia kwa luninga wakiburuzwa mahakamani-keki-mahakamani!

SWALI LANGU SASA:NIni ilikuwa hatma/suluhisho la serikali:
-wale samaki walikwenda wapi baada ya kuchukuliwa?
-wale wa-asia kesi yao ni aje ni vipi?

Ndugu zangu wana jamii nimeuliza hili makusudi tu,kwasababu sitaki kujiongezea hasira au chuki dhidi ya hii serikali na maamuzi yake mengi.Nimeuliza hili ndugu zangu kwa sababu sitaki kuamini kile ninachokihisi

Mtu mwenye data zozote juu ya hili sakata naomba anitoe dukuduku......
 
Last edited:
Swali zuri mkuu, hope raia watatoa data.
 
Hapa mkuu wangu, mimi ningependa sana kuelewa nchi yetu tunafanya nini kuhakikisha samaki hao wanazalishwa nchini na kusafirishwa nje kama wanavyofanya hao Wa ASIA..Tuna fish wana soko kubwa dunia nzima yaani naweza sema soko lake ni kubwa kuliko samaki yeyote.. sisi kina Uchumi Tunao Tunaukali.( UTUTU) . kaazi yetu ni sawa na yule nyoka wa mdimuni, kugonga watu wanaukuja chuma wakati hatuli ndimu hizo..
Lini sisi tutaondoka ktk fuko hili la umaskini wa akili?.. Wa asia wanakuja nchini kuchua samaki madini na kadhalika kuelepeka China (Hong Kong) sisi tunashindwa kipi kuwawezesha wananchi waifanye biashara hizo hizo kisheria.
Leo hii nchi imejaa matapeli wa kila aina kwa sababu wanajua fika wananchi wetu hawawezi kufikkisha mzigo yaani tumepata bahati wanunuzi (walanguzi) wanakuja hadi nchini bado hatujashtuka wakati hizi sii biashara haramu.
 
Hao "Tuner" lol nina uhakika watu wameshakula dili, nilikuwa naangalia kwenye habari (CNN) samaki mmoja anafika hadi $1000! kwenye soko la Japani. Sasa hapo unafikiri wazee wetu wa 20% watazubaa?!!?
 
GT kwani umesikia kitu gani? ...hili suala zuri sana ambalo jibu lake sidhani kama ni jepesi kupatikana.
samaki wameenda wapi?
 
Samaki bado wamehifadhiwa katika kampuni ya Bahari Foods wakisubiri amri ya mahakama kuu wapigwe mnada. Kesi ipo mahakama ya Kisutu lakini inatakiwa kuamishiwa mahakama kuu ndio maana amri ya mwanzo ya mahakama ya kisutu ya kuuza wale samaki imesimamishwa.
Wale waasi wanataka kupewa dhamana na mahakama imeamuru meli yao ifanyiwe valuation ili itumike kuwadhamini wale waasia.
 
jamaii tatizo langu me ni mahakama mpaka leo wameshindwa kutoa maamuzi kesi inaendelea na storage charges zinaongezeka! Me nadhan wanasheria waanze kuendezesha kesi kibiashara zaidi manake mpake kesi iishe hasara inaweza kuwa kubwa kuliko! Nadhani kuna haja ya kufikilia namna ya kuwasaidia mahakimu na mfumo wetu wa mahakama hapa kwetu! There is a problem ktk uchunguzi!
 
Mpaka kukamatwa kwa hao Tuna serikali haijafanya lolote wanaoza tu bora wagawe ferry pale kila mlalahoi anunue kwa bei ya kutupwa.
Kingine licha kuonekana hao samaki wapo kwa wiki kwenye mipaka yetu baharini serikali inaendelea na uvivu wake ule ule wa karne hadi karne imeshindwa kujitengenezea mazingira ya soko wa hii bidhaa adimu duniani wamebaki kusinzia si bora waachie tu hao wavuvi haramu maana mnawashikilia samaki wanazaliana kwa wingi mnashindwa hata kupanga mikakati endelevu ya kuvuna samaki aina hiyo sasa hii ni nini?
 
kwa nijuavyo tangu siku zile wanapakua samaki .....ni kwamba magufuli alisema wana majokofu yenye uwezo wa kuhifadhi hao samaki kwa more than 10 yrs,sasa tukiamni kwamba wamehifadhiwa...ukishapita mwaka mmoja tu,nobody will ask for that...kwahiyo itakuwa diloi lao,itz better tujue what nex there..........
 
Vichekesho nchi hii, kwanza tujiulize serikali ilitaka kuachieve kitu gani kwa kukamata meli ile na shehena yake. Meli imeshikwa haifanyi kazi na inaharibika bandarini shauri ya sea corrosion, samaki wapo sehemu ambapo storage charges ni kubwa kuliko kawaida mabaharia wako ndani muda wote toka meli iliposhikwa.

Mpaka hapo utaona serikali yetu ina liabilities tatu meli kuharibika kwa kutotumika, samaki kuhifadhiwa kwa gharama kubwa na kuwanyima uhuru mabaharia wa meli hiyo.

Chukua scenario hii upande wa mashtaka unashindwa kuthibitisha kesi na mabaharia wanachiwa, mwenye meli atafungua kesi dhidi ya serikali kudai fidia ya loss of business, kuharibika meli, kuharibika bidhaa zake. Mabaria nao wanaweza kufungua madai kwa kufunguliwa kesi isivyo halali. In that situation serikali italipa kiasi kikubwa sana, na hatutaachive kitu apart from international reputation.

Walipa kodi tusiombee hiyo scenaio itokee we will pay through our noses.
 
Back
Top Bottom