Serikali na malipo kwa 'wafanyakazi hewa'

Tanzania ina mafisadi kuanzia kwenye vijiji mpaka ikulu kwa JK. Tena wengine tunashinda nao hapa huku huko makazini kwao wanaiba au hawatoi haki kwa Watanzania wenzao.

JK angelikuwa serious, kinachotakiwa hapa ni kuanzisha mapambano na mahakama maalumu ya kupambana na ufisadi.

Hizo pesa zote zinapotea kwenye wizara moja na hakuna anayewajibika? Sasa kwanini tuna makatibu wakuu, mawaziri na watendaji wengine? Kama waziri amelaza tumbo lake tu kwenye shangingi huku 3.5B zinaibiwa, kweli mtu kama huyo anatufaa?

Nchi hii inasikitisha sana.
 
Tanzania ina mafisadi kuanzia kwenye vijiji mpaka ikulu kwa JK. Tena wengine tunashinda nao hapa huku huko makazini kwao wanaiba au hawatoi haki kwa Watanzania wenzao.

JK angelikuwa serious, kinachotakiwa hapa ni kuanzisha mapambano na mahakama maalumu ya kupambana na ufisadi.

Hizo pesa zote zinapotea kwenye wizara moja na hakuna anayewajibika? Sasa kwanini tuna makatibu wakuu, mawaziri na watendaji wengine? Kama waziri amelaza tumbo lake tu kwenye shangingi huku 3.5B zinaibiwa, kweli mtu kama huyo anatufaa?

Nchi hii inasikitisha sana.


hapa ni kuonyesha ni kwa kiasi gani mizizi ya ufisadi imekomaa. Kila mwenye nafasi anachofikiria ni kuchukua chake mapema, tena bila woga kwa kuwa ana uhakika hakuna anayeweza kumwajibisha kwa vile hao wanaotegemewa kuwajibisha nao wanachukua vyao mapema.
 
Sawa.... solution ni kuwa na National Identity cards!

kwanza ni kukata hiyo mizizi ya ufisadi. Idendity cards hata zenyewe zaweza chezwa shere na hao mafisadi. Tanzania hakuna kinachoshindikana kama hii mashina na mizizi ya ufisadi itaendelea kuwepo huko kwenye utumishi wa umma.
 
Sawa.... solution ni kuwa na National Identity cards!

Hata identity cards nazo si wataiba? Dawa ni mahakama tu, tena hakuna haja ya uchunguzi wa miaka. Hivi Masha anafanya nini wizara ya mambo ya ndani?

Hii hali isipomeshwa ndio mwanzo wa matatizo chungu nzima kwa Afrika. Uongozi usio wa haki ndio mwanzo wa migogoro na vita vya ajabu ajabu kwenye nchi za Afrika.
 
Hata identity cards nazo si wataiba? Dawa ni mahakama tu, tena hakuna haja ya uchunguzi wa miaka. Hivi Masha anafanya nini wizara ya mambo ya ndani?

Hii hali isipomeshwa ndio mwanzo wa matatizo chungu nzima kwa Afrika. Uongozi usio wa haki ndio mwanzo wa migogoro na vita vya ajabu ajabu kwenye nchi za Afrika.


Anampa bendera Miss Tanzania kwenda kuiwakilisha Tanzania Miss World.
 
Bilioni 7.5 zatumika kulipa watumishi hewa - Hawa Ghasia

Uzembe unaendelea....

SERIKALI imepoteza shilingi bilioni 7.5 kwa kuwalipa watumishi hewa 2,924, Bunge limeelezwa.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais , Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia, amewaeleza wabunge kuwa, wahusika katika wizi huo wameiba jumla ya sh 7,568, 625, 519/-.

“Waajiri waliobainika kuwa na malipo mengi hewa ni pamoja na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili” Amesema Waziri Ghasia bungeni wakati anajibu swali la Mbunge wa Singida Kusini, Mohamed Misanga.

Mbunge huyo aliuliza, katika miaka minne kuanzia mwaka 2006, Serikali imepoteza fedha kiasi gani kwa kuwalipa watumishi hewa na ni kutoka katika Wizara na taasisi zipi. Katika swali la nyongeza, Mbunge huyo alimuuliza Waziri Ghasia kuwa, waliosababisha hasara hiyo wamechukuliwa hatua gani.

Ghasia amesema, watumishi hao hewa wanalipwa mishahara kwa kuwa waajiri hawajawaondoa kwenye orodha ya malipo wakati utumishi wao umekoma.

Kwa mujibu wa Ghasia, utafiti umebanisha kuwa, watumishi hewa walikuwa ni waajiriwa serikalini lakini utumishi wao umekoma kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kustaafu, kufariki dunia, na pia kufukuzwa kazi.

Waziri Ghasia amelieleza Bunge kuwa, majina ya waliosababisha wizi huo yamepelekwa kwenye vyomvo vya ulinzi na usalama, vinalifanyia kazi suala hilo.

Mbunge wa Kisarawe, Athumani Janguo, aliuliza kwamba, uchunguzi kuhusu suala hilo utamalizika lini, na Serikali itachukua hatua gani.

Ghasia amemjibu kwamba, uhakiki katika sekta ya afya umekamilika mwaka jana, Serikali ikijiridhisha itapeleka majina kwenye vyombo vya ulinzi na usalama.

Kwa mujibu wa Waziri huyo, Serikali imepata taarifa za awali kuhusu wahusika kwenye sekta ya elimu, hivi karibuni watachukuliwa hatua za kinidhamu na kushitakiwa.

Source: Gazeti la HabariLeo
 
Ni ushauri tu, uundwe utaratibu wa kutambua wafanyakazi hewa nnchi nzima,zoezi lichukue mwezi mmoja,utakuwa umetatua tatizo kwa nchi nzima,sio taasisi moja,ipigwe sensa na hapo itakuwa unawajua waliopo na feki
 
Back
Top Bottom