Serikali: Mpaka sasa hakuna taarifa rasmi kuhusu kukataliwa kwa Mahindi, ni kikaratasi tu cha mtandaoni

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,501
9,280
Serikali ya Tanzania imesema mazungumzo yanaendelea kati yake na Serikali ya Kenya kuhusu kuzuiwa kwa mahindi katika mpaka wa Namanga.

Zuio la mahindi kutoka Tanzania lilitolewa Machi 5 2021na Mamlaka ya Kilimo na Chakula ya nchini Kenya ikidai kuwepo kwa sumu kuvu katika mahindi yanayotoka Tanzania na Uganda.

Akizungumza jijini Dodoma leo Jumatatu Machi 8, 2021 msemaji mkuu wa Serikali ya Tanzania, Dk Hassan Abbas amesema hadi sasa hakuna taarifa rasmi kuhusu kukataliwa kwa mahindi kutoka Tanzania kwenda nchini Kenya zaidi ya kikaratasi ambacho kimeonekana kwenye mtandao.

“Ni kweli mahindi ya Tanzania yamezuiwa kwenye mpaka wa Namanga lakini Hororo yanapita na mipaka mingine yanaendelea kupita sasa katika hali kama hiyo sisi Serikali kwa Serikali lazima tuzungumze,” amesema.

Amesema suala hilo linaendelea kufanyiwa kazi na mazungumzo yanaendelea kati ya pande hizo mbili.

“Kwa nini katika mpaka wa Hororo mahindi kutoka nchini yanapita lakini Namanga yamezuiwa,” amehoji Dk Abbas.

Mwananchi
 
Mitano tena ndiyo zao kukanusha. Ndiyo maana watu wanapukutika kwa korona lkn wanasema hakuna korona.
 
Huu umekuwa mchezo wa kitoto sasa.

Kama mpaka uliozuiwa ni hapo Namanga, basi peleka malori kwenye mipaka mingine yanaporuhusiwa kuingia.

Hata kama patakuwepo suluhisho, hili liwe fundisho la kufanyia kazi.

Wakulima wetu hawawezi kutegemea soko la aina hii kila mwaka. Ni lazima juhudi kubwa zifanyike kutafuta masoko mengine mbali ya hili la ubabaishaji mwingi.

Wakati mahindi yetu yanazuiwa, wao malori yao yenye bidhaa zao yanaingia bila kikwazo kwetu.

Ni wakati wa kutafuta bidhaa ya kuzuia sawia na mahindi yetu, ili hasara iwe sawia pande zote.

Michezo ya namna hii ya kuwaumiza wakulima wetu haivumiliki.
 
Shida ya hii serikali inajifanya much knows.. Unasema hujapata taarifa rasimi huku ukisema Namanga hayaingii na mazungumzo yanaendelea! Sasa umepeleka maafisa kufanya mazungumzo ya nini ilihali taarifa hujaikubali? Weka mambo wazi watu wasiendelee kula hasara maana kutoa mzigo Songea mpaka Tanga ama Namanga ni gharama halafu ufike uambiwe no Entrance...utaupeleka wapi na nani atacover costs?
 
Shida ya hii serikali inajifanya much knows.. Unasema hujapata taarifa rasimi huku ukisema Namanga hayaingii na mazungumzo yanaendelea! Sasa umepeleka maafisa kufanya mazungumzo ya nini ilihali taarifa hujaikubali? Weka mambo wazi watu wasiendelee kula hasara maana kutoa mzigo Songea mpaka Tanga ama Namanga ni gharama halafu ufike uambiwe no Entrance...utaupeleka wapi na nani atacover costs?
u much know wa serikali uko wapi kwenye hili sasa!!!!

serikali ya kenya inatakiwa itoe katazo rasmi,sio stori za twitter.
 
Serikali imechanganyikiwa.

Hakuna taarifa maalumu alafu muda huo huo wanafanya mazungumzo.

Serikali bwana!!
 
Shida ya hii serikali inajifanya much knows.. Unasema hujapata taarifa rasimi huku ukisema Namanga hayaingii na mazungumzo yanaendelea! Sasa umepeleka maafisa kufanya mazungumzo ya nini ilihali taarifa hujaikubali? Weka mambo wazi watu wasiendelee kula hasara maana kutoa mzigo Songea mpaka Tanga ama Namanga ni gharama halafu ufike uambiwe no Entrance...utaupeleka wapi na nani atacover costs?
Serikali ime panic
 
u much know wa serikali uko wapi kwenye hili sasa!!!!

serikali ya kenya inatakiwa itoe katazo rasmi,sio stori za twitter.
Katazo la twiter kwako, sasa kama la twitter maafisa wa Tanzania wanafanya mazungumzo ya nini na serikali ya Kenya? Kenya imeshaitangazia dunia kuwa Mahindi yetu si salama na Haya kenya wakikubali kulegeza kamba bado dunia haiwezi kubadiri msimamo wake juu ya taarifa hii, Serikali ya Tanzania haikupaswa kujipendekeza tena kwa mkenya. Yale maroten food yanayoingia nchini kutoka kenya yangeshapigwa ban tayari.
 
Katazo la twiter kwako, sasa kama la twitter maafisa wa Tanzania wanafanya mazungumzo ya nini na serikali ya Kenya? Kenya imeshaitangazia dunia kuwa Mahindi yetu si salama na Haya kenya wakikubali kulegeza kamba bado dunia haiwezi kubadiri msimamo wake juu ya taarifa hii, Serikali ya Tanzania haikupaswa kujipendekeza tena kwa mkenya. Yale maroten food yanayoingia nchini kutoka kenya yangeshapigwa ban tayari.
mkuu mahindi ni bidhaa ya lazima kwa mteja.hawezi kukuringia kununua mahindi atakula nini!!!!serikali inatafuta uhalali wa hilo tamko.
maana kama lengo ni kuchafuana nyuma ya pazia,basi likanushwe.

hicho unachosema kuhusu bidhaa za kenya,ni mipira yao ya kupumulia ICU.ndio maana lazima tuwaulize kwanza kabla ya kukata,ni kweli wameamua kufa???
 
mkuu mahindi ni bidhaa ya lazima kwa mteja.hawezi kukuringia kununua mahindi atakula nini!!!!serikali inatafuta uhalali wa hilo tamko.
maana kama lengo ni kuchafuana nyuma ya pazia,basi likanushwe.

hicho unachosema kuhusu bidhaa za kenya,ni mipira yao ya kupumulia ICU.ndio maana lazima tuwaulize kwanza kabla ya kukata,ni kweli wameamua kufa???
Wakenya wamepata soko jipya la kununua mahindi kutoka Mexico na ndiyo maana wamesambaza upuuzi huu.
 
Kwani wapi serikali ya Kenya imetoa katazo kwa mahindi ya Tanzania?
 
Wakenya wamepata soko jipya la kununua mahindi kutoka Mexico na ndiyo maana wamesambaza upuuzi huu.
mahindi ya tz ni bei rahisi zaidi na ni bora zaidi pia.

na kama itathibitika hivyo basi na bidhaa zao za viwanda itabidi wakatafute soko huko.

sisi tunatafuta uhalali wa kauri yao.
 
Serikali ya Tanzania imesema mazungumzo yanaendelea kati yake na Serikali ya Kenya kuhusu kuzuiwa kwa mahindi katika mpaka wa Namanga.

Zuio la mahindi kutoka Tanzania lilitolewa Machi 5 2021na Mamlaka ya Kilimo na Chakula ya nchini Kenya ikidai kuwepo kwa sumu kuvu katika mahindi yanayotoka Tanzania na Uganda.

Akizungumza jijini Dodoma leo Jumatatu Machi 8, 2021 msemaji mkuu wa Serikali ya Tanzania, Dk Hassan Abbas amesema hadi sasa hakuna taarifa rasmi kuhusu kukataliwa kwa mahindi kutoka Tanzania kwenda nchini Kenya zaidi ya kikaratasi ambacho kimeonekana kwenye mtandao.

“Ni kweli mahindi ya Tanzania yamezuiwa kwenye mpaka wa Namanga lakini Hororo yanapita na mipaka mingine yanaendelea kupita sasa katika hali kama hiyo sisi Serikali kwa Serikali lazima tuzungumze,” amesema.

Amesema suala hilo linaendelea kufanyiwa kazi na mazungumzo yanaendelea kati ya pande hizo mbili.

“Kwa nini katika mpaka wa Hororo mahindi kutoka nchini yanapita lakini Namanga yamezuiwa,” amehoji Dk Abbas.

Mwananchi
Seri*£ ya kipumbavu
 
Back
Top Bottom