#COVID19 Serikali moja ya Dunia na chanjo ya COVID-19

Matanga

JF-Expert Member
Nov 13, 2019
2,281
3,973
TAARIFA KWA UMMA wa na Dr Lugendo

Karibuni,

SERIKALI MOJA YA DUNIA NA CHANJO YA COVID-19

Hii ni mada ndogo iliyo katika MADA kubwa isemayo “ KUNA NINI NYUMA YA CORONA ?” ndiyo tunayoendelea nayo.

Hebu tutazame kidogo yanayoendelea ulimwenguni.

Huko Marekani: “Juni 23, 2021—Zaidi ya watumishi 150, wa Hospitali ya Houston Methodist, wamefukuzwa na wengine kuamua kwa hiali kuacha ajira baada ya kukataa kufuata masharti yanayowataka waajiriwa wa HOSPITALI hiyo kuchanjwa chanjo ya COVID-19.” Habari kama ilivyotoripotiwa na The Associated Press[1]

Wakati hayo yakijili Serikali ya Punjab, Pakstani yenyewe imetangaza kuwafungia laini za simu raia wote watakao kataa kuchanjwa chanjo ya COVID-19.[2]

Naam, habari hizo ni nzuri au ni mbaya?

Katika mada yetu, iliyopita ikiwa imebeba kichwa cha mada mama, “Kuna Nini Nyuma ya Corona?”

tulitazama kwa ushahidi tele ya kwamba kilicho nyuma ya Corona ni “Serikali Moja ya Dunia”

Na ya kwamba, Corona ni nyenzo tu inayotumika kufanikisha usimikwaji wa serikali, hiyo.

Ambayo pia itahitaji raia wote wanaoishi kwenye sayari dunia kupewa siku moja ya pumziko.

Hiyo ndiyo vita inayoendelea nyuma ya kile kiitwacho Covid-19.

Ukweli ni kwamba kilicho nyuma ya corona ni cha hatari kuliko covid-19 yenyewe.

Ezekieli 7:5 “Bwana MUNGU asema hivi; Ni jambo baya, jambo baya la namna ya peke yake; angalia, linakuja.”

Uhusika wa Chanjo ya Covid-19


Kama lengo la corona ni kufanikisha usimikwaji wa serikali moja na dini moja ya dunia, kama tulivyoona. Kwa nini chanjo tena?

Ahaa! Vizuri kama umeuliza swali hilo.

Tukizingatia kwamba Chanjo ya Covid-19, walioileta ndio wale wanaotafuta kusimika hii serikali.

Sasa kumbe kupokea chanjo hiyo ni kufanyaje?

Jibu ni rahisi sana. Ni Kupokea au kukubaliana kabisa na matakwa ya serikali hii ya ulimwengu.

Naam, ndivyo!
Na kuikataa pia nikupingana nayo vile vile.

Weka akilini kwamba kilicho nyuma ya Covid-19 ni kizito mno kuliko Covid-19, yenyewe.

Sahau yote lakini hilo kamwe usisahau.

Chanjo ya corona ina mambo matatu muhimu :

(a)kuwaandaa watu kiakili (kuwabadili wakazi wa dunia kifikra wamwabudu Lucifa pasipo kushituka wala kuhoji.

Kinachofanyika kwenye chanjo hii ni kile kiitwacho genetic engineering kubadili viasili (vina saba).

kwa lugha iliyonyepesi sana, ni kwamba Chanjo hii, inakwenda mpaka pale utu wako ulipo, inaupakuwa utu huo kisha inakuwekea utu mpya, uliotengenezwa na wakuu hao.

Kwa hivo Covid-19 imebeba genetic modifiers -viasili vinavyofanya deliberate modification ya kiumbe.

Covid-19 Vaccine -ni modifier materials- vilivyotengenezwa kisayansi kuchochea mwelekeo wa tabia wanayoitaka wakuu hao iwe ndani ya wakazi wote wa dunia, ili wamwabudu Lusifa.

Kwakufanya hivyo wana uhakika ye yote atakayejidanganya kupokea chanjo hiyo atakuwa tayari amekubali kubadilishwa fikra kukubaliana na matakwa ya kile serikali hiyo moja na dini yao ya ulimwengu inacholeta.

Biblia ikasema:
“Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia.

Mtu akiwa na sikio na asikie.” -Ufunuo 13:8-9

(b) kazi namba mbili ya chanjo hii, ni kupunguza idadi ya wakazi wa dunia.

Hii chanjo itafanya kazi ya mass depopulation .

Kwa namna ambayo hatuwezi sana kuileza sasa lakini ambayo itadhihilika baada ya ulimwengu mzima kuwa umechanjwa.

(c) kazi nyingine ya chanjo ni kuwasajili watu katika daftari la kudumu la raia wa dunia, kisha kuwapa kitambulisho cha dunia (covid passport).

Na hatimaye mtu hataweza kuuza wala kununua chochote pasipokuwa na kitambulisho hicho.

Katika tukio la kufukuzwa, na wengine kwa hiali yao kuacha kazi, lililotokea katika hospitali ya Kanisa la Methodist, hapo juu; kabla Uliwekwa utaratibu wa sheria iliyowataka wafanyakazi wa hospitali hiyo waliopata 26000, wachague ama wachanjwe au wafutwe kazi.

Miongoni mwao 178, walikataa kuchanjwa, na wakapewa matazamio ya kujirekebisha ndani ya wiki mbili. Ambao hata hivyo hawakubadili msimamo wao.[4], The Associated Press reported.

Tukio kama hilo liko mbele ya umma mzima wa dunia. Utachanika vipande viwili, vilivyowazi kila mahali. Kuanzia kwenye ajira, hadi kwenye ndoa, familia, kitongoji, hadi ndani ya ukoo kutakuwa na mipasuko, mpaka ngazi ya taifa na kimataifa.

Ni wale tu watakao kuwa na kitambulisho hicho cha chanjo ya covid-19, ndio wataruhusiwa kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine, kupata huduma za kijamii, kama maji, umeme, matibabu ya hospitali n.k..

Kwa hiyo jaribio lolote la kukataa Chanjo ya Covid-19, au kutofuata masharti yanayotolewa juu Covid-19, ni kusaini hati ya kifo.

Maana utakuwa unawakwamisha mipango yao.

Kukataa Chanjo hiyo au kubalina na masharti yake ni kukwamisha usimikaji wa serikali moja na Dini moja ya dunia.

Dunia nzima tunasiamama katikati ya uamzi mgumu sana; kuwako au kutokuwako.

Tuko kwenye kizingiti cha umilele -kufa au kupona. Uzima na mauti VYOTE viko mbele yetu.

Fikiria kama ilivyokuwa mlengo wa rais huyu na raia wake walio wengi kupinga swala la CHANJO ya COVID-19.

“Tumewabana kisawa sawa ” alisema rais huyo na kuongeza “ adui yao mkubwa ni mimi; kwa sababu nina kwamisha mambo yao .

Lakini mimi ninakwamisha kwa niaba yenu….hawawezi wakafurahi.

…kwenye swala la Corona tulitakiwa tufungiwe wote
…" alisema rais Magufuli na kuendelea:

" Tukaambiwa tujifungie kwenye nyumba .

Ukiwa na boda boda yako, usiende kuiendesha, ukiwa na duka lako kioski usiende kufungua, ukiwa na basi lako usiende kuliendesha,
_
hutakiwi kutoka mahali fulani kwenda mahali fulani, ukiwa na shamba usiende kulipalilia. Ulikuwa ni utumwa mkubwa_ .

Walitaka walete machanjo ya ajabu…tutumike sisi kama wanayama wakufanyiziwa majaribio, NIMEWAKWAMISHA, Tanzania MMEWAKWAMISHA . …

Lakini kujitoa hivyo ni sadaka, hawawezi wakafurahi .” --Hotuba ya Rais Magufuli, akiwa Segerea.

Sasa KUMBUKA tena kauli ya mzee wetu Papa Francis alivyosema ya kwamba: “ hatua ya watu kukwepa kupata chanjo ya Covid-19 ni mauaji ya kujitakia

Huku akiongeza tena kwamba watu wa jinsi hiyo wanacheza na Manisha yao lakini pia“ wanacheza na maisha ya watu wengine.” [3]

Kwa hiyo kama tulivyoona, kufikia hapo; Tanzania ilikuwa tayari imecheza na maisha ya watu, pale ilipo kataa kutii sheria za kimataifa juu ya janga la Covid-19 .

Na wakuu wa serikali moja ya dunia ilikuwa sharti wafanye jambo, litakalo badili hali ya mambo Tanzania, ili isiendelee kukwamisha harakati za SERIKALI MOJA YA dunia.

Fuatilia sana nyendo za rais Magufuli baada, na hata wakati mchache kabla ya kifo chake.

Utaona kwamba alikuwa akivutana uso kwa uso na viongozi wa Vaticani , akafikia kusema “Viongozi wa dini msitupotoshe!” pale alipotoa hotuba yake akiwa huko Chato.

Je, Mzee wetu Francis hakuwa miongoni mwa viongozi wa Dini, ambao Magufuli alisema wasiwapotoshe watu?

Jibu ni kwamba ujumbe wa rais Magufuli ulikuwa ukienda Kwa viongozi wote wa Dini hususani Papa Francis na timu yake.

Hebu, tazama kile kinachoendelea sasa kati ya serikali na viongozi wa Vatican mathalani kwenye kikao cha Mh. Rais na Baraza la Maaskofu Katoliki –TEC ., ambao kiprotokali wanatekeleza maagizo ya Papa Francis, je, hawapotoshi? WANAPOTOSHA! tena 100%

Sasa Tanzania sio tena mgeni wala mpitaji katika swala la Covid-19. Ila ni mshiriki na mlithi wa mikopo ya Benki ya dunia na IMF , ili kufadhili na kurubuni akili za wanaosimama mbele, wafuate matakwa ya serikali hii moja.

Je, ni akina nani walio nyuma ya agenda hii?

Una bahati, kama umethubutu kuuliza swali hilo. Walio nyuma ya agenda hii ni hawa: (I) Mnyama , (II) Sanamu yake .-

Hao ndio wahusika wakubwa wa kinachoendelea.

Ufunuo 14:9-12
“Na mwingine, malaika wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake , na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu. Naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo.”

Tuungane wote wakati ujao. Tutakapoanza kuwachambua wahusika hao wawili kina. Ufunuo 14:9-12.

Huo ndio unabii wa mwisho wa Dunia unaosukumwa sasa kupitia Covid-19 , nasi tutauhubiri

Kuukwepa ni kuamua kutembea kwa miguu yako miwili kuingia jehanam

Asomae na Afahamu
 
Kuna mwingine huko kaandika uzi kasema sijui ni lisayari gani litaigonga dunia hivi karibuni maana huko liliko lipo speed kuja kuigonga dunia, na huo ndio utakuwa mwisho wa dunia. Huku tena tunakutana na vitisho vya chanjo ya covid 19. Aisee mbona siku hizi watu wanakitabiria sana kiyama??
 
Kuna mwingine huko kaandika uzi kasema sijui ni lisayari gani litaigonga dunia hivi karibuni maana huko liliko lipo speed kuja kuigonga dunia, na huo ndio utakuwa mwisho wa dunia. Huku tena tunakutana na vitisho vya chanjo ya covid 19. Aisee mbona siku hizi watu wanakitabiria sana kiyama??
Kiama kipo na kikaribu Sana maandiko yako wazi kabisa

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Katika hali ya kawaida, kuishi kuna namna mbili, kimwili na kiroho (physical and spiritual worlds). Yanayoendelea kuhusu ugonjwa wa corona na kinga au matibabu yake yako physical na yanauthiri mwili in physical form. Kinachoumia ni mwili na mwisho kama ni kufa kinachokufa ni mwili.

Sasa tupo duniani tunaishi kimwili. Linapotokea jambo kama hili, mwili unaepuka vipi hatari inayoandamana na kadhia hiyo ikiwa binadamu kama social being hatapata mahitaji ya kimwili (chakula, kazi, safari, matibabu, maji etc) ambayo yako kijamii hawezi kuyapata peke yake kwa kujitegemea, kimwili huyu anapona vipi, au ndio akubali kufa ?

Jambo la pili ni la kiroho na zaidi kiimani, unayoyasema na kuyahusisha na biblia hayo yanachukua sura ya kiimani. Sasa swali ikiwa kiroho mtu atapona kwa imani hiyo ya maandiko, kimwili anaponaje ili aishi na wanadamu wengine?
 
Katika hali ya kawaida, kuishi kuna namna mbili, kimwili na kiroho (physical and spiritual worlds). Yanayoendelea kuhusu ugonjwa wa corona na kinga au matibabu yake yako physical na yanauthiri mwili in physical form. Kinachoumia ni mwili na mwisho kama ni kufa kinachokufa ni mwili. Sasa tupo duniani tunaishi kimwili. Linapotokea jambo kama hili, mwili unaepuka vipi hatari inayoandamana na kadhia hiyo ikiwa binadamu kama social being hatapata mahitaji ya kimwili (chakula, kazi, safari, matibabu, maji etc) ambayo yako kijamii hawezi kuyapata peke yake kwa kujitegemea, kimwili huyu anapona vipi, au ndio akubali kufa ?

jambo la pili ni la kiroho na zaidi kiimani, unayoyasema na kuyahusisha na biblia hayo yanachukua sura ya kiimani. Sasa swali ikiwa kiroho mtu atapona kwa imani hiyo ya maandiko, kimwili anaponaje ili aishi na wanadamu wengine?
Nimekusoma mkuu naomba na Mimi nikuulize swali "UNAAMINI KTK MAANDIKO MATAKATIFU JUU YA DALILI ZA KURUDI KWA YESU??"

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Katika hali ya kawaida, kuishi kuna namna mbili, kimwili na kiroho (physical and spiritual worlds). Yanayoendelea kuhusu ugonjwa wa corona na kinga au matibabu yake yako physical na yanauthiri mwili in physical form. Kinachoumia ni mwili na mwisho kama ni kufa kinachokufa ni mwili. Sasa tupo duniani tunaishi kimwili. Linapotokea jambo kama hili, mwili unaepuka vipi hatari inayoandamana na kadhia hiyo ikiwa binadamu kama social being hatapata mahitaji ya kimwili (chakula, kazi, safari, matibabu, maji etc) ambayo yako kijamii hawezi kuyapata peke yake kwa kujitegemea, kimwili huyu anapona vipi, au ndio akubali kufa ?

jambo la pili ni la kiroho na zaidi kiimani, unayoyasema na kuyahusisha na biblia hayo yanachukua sura ya kiimani. Sasa swali ikiwa kiroho mtu atapona kwa imani hiyo ya maandiko, kimwili anaponaje ili aishi na wanadamu wengine?
Swadakta.....

Hapo ndipo pale wenye majibu mepesi kwa maswali magumu wanaposhindwa KUTUSHIBISHA HOJA KUNTU.....
 
Nimekusoma mkuu naomba na Mimi nikuulize swali "UNAAMINI KTK MAANDIKO MATAKATIFU JUU YA DALILI ZA KURUDI KWA YESU??"

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
Ndipo ilipo hoja yangu hapo. Umegusa upande wa maisha ya rohoni (imani) ambayo katika hali ya kawaida hata kwa tafsiri ya maana ya imani yenyewe ni kuamini tu bila kuwa na mashaka kitu ambacho hakipo bado au kilikuwepo “zamani” kabla yako kuona au kukisikia mwenyewe. Hii ni spiritual world ambayo hata kama nikisema naamini, bado dunia ina watu wa imani tofauti na yangu/yako, na ni wengi tu ukichukua sensa ya dunia nzima, sasa hata nikijibu kuwa naamini, swali langu ni kuwa, kimwili (physical being) mtu atakaye kataa chanjo ya covid (kwa kuongozwa na imani) je kimwili atapona vipi? Au ni kukubali kufa? Au ataishi kwa namna nyingine ikiwa maisha ya kimwili yatamzuia asipate huduma za muhimu zinazolinda maisha ya “kimwili” kama afya, maji safi na salama, kusafiri, kuuza au kununua?

ninachouliza ni simple, ikiwa dunia itaweka utaratibu kuwa wenye chanjo tu ndio wapate huduma, wale ambao hawatakuwa wamechanjwa sababu ya imani wataishi vipi?
 
Ndipo ilipo hoja yangu hapo. Umegusa upande wa maisha ya rohoni (imani) ambayo katika hali ya kawaida hata kwa tafsiri ya maana ya imani yenyewe ni kuamini tu bila kuwa na mashaka kitu ambacho hakipo bado au kilikuwepo “zamani” kabla yako kuona au kukisikia mwenyewe. Hii ni spiritual world ambayo hata kama nikisema naamini, bado dunia ina watu wa imani tofauti na yangu/yako, na ni wengi tu ukichukua sensa ya dunia nzima, sasa hata nikijibu kuwa naamini, swali langu ni kuwa, kimwili (physical being) mtu atakaye kataa chanjo ya covid (kwa kuongozwa na imani) je kimwili atapona vipi? Au ni kukubali kufa? Au ataishi kwa namna nyingine ikiwa maisha ya kimwili yatamzuia asipate huduma za muhimu zinazolinda maisha ya “kimwili” kama afya, maji safi na salama, kusafiri, kuuza au kununua?

ninachouliza ni simple, ikiwa dunia itaweka utaratibu kuwa wenye chanjo tu ndio wapate huduma, wale ambao hawatakuwa wamechanjwa sababu ya imani wataishi vipi?
Bora nichague kufa niende mahali salama kuliko nichague kuishi nikifa nipate mateso milele mkuu

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
We umejitahid kuandika lk kuna watu watakupinga sana tena bila aibu na watakao kupinga hawana sabbu maalum zaid ya chuki, na watakaokupinga ni wale wafuas wa chadema na waliokuwa wakimchukia yule bwana, nu kwel kuwa upinzan ama kumchukia mtu kusikufanye uyachukie na yale mazur aliyoyatenda, maana wew unaemchukia hakuna jema ulilotenda kumzid huyo unaemchukia,,mm haya nishawai ongea sana lkn watz wamelogwa na siasa zakipuuz yaan hawaon, hawasikii wala hawatak kusikia, kila uwaambialo wao watakupinga tu sabbu wanaemuam nae anapinga...kiukwel tupo ktk zama mbaya ambazo ndzo zilizotabiliwa na manabii lkn cha ajabu watu wamekaza mioyo hawatak kuelewa, na sabbu ya wao kukaza mioyo ilishaejieleza hata ktk maandiko kuwa kuna watu watapinga tuu ukwel na hawa ndyo watakuwa mfano wa mateso na watajutia maamuz yao baada ya kupoteza nafasi,,Tz tuna bahat kubwa nchi yetu imekuwa ikioonea ktk majanga meng sana, na kwel itapona majanga meng sana, lkn mujue kuwa hakuna wakuustopisha mwisho mbaya hata awe nan, hata mtu abisheje ule mwisho ni lazma ujee na utawaumiza wengi sana, na kwa dalili hizi watu walvyo kaza nyoyo, ni waz kuwa watakaoangamizwa na agenda za shetan( mtu mweupe) n weng mno, mujue kuwa, target kubwa ya mzungu na agenda yake ya kuitawala dunia ni afrika tuu,

kuitawala kwenyewe ni kupitia iman ya lazima, na la mwisho ni kuangusha dola kubwa zinazotawala dunia, ili ile dola ya siri itawale ni lazma dola za USA, Russia, china, india, uarabuni, dola za ulaya zianguke ama kupoteza nguvu, na kuanguka kwenyewe ni lazma ziungane ili ku give up mamlaka kwa kiongoz mpya ama kuyakabiz mamlaka kwa njia ya nguvu za kijeshi yaan THE THIRD WORLD WAR, ambayo itahusisha mataifa makubwa yenye nguvu kinyuklia yatakaposhambuliana na kupoteza nguvu zao kijeshi na kiuchumi, bas mujue kuna dola ya siri itaamka na kuitawala dunia kiurahisi sana, kuitawala afrika ni rahisi sana lkn kinachokwamisha ni wao wenyew kupingana, yaan mataifa ya wazungu, waarabu na wachina Kutofautiana ktk sera za kiuchumi,kijamii,kidini na kisiasa, mfano USA akitaka kuifanya afrika ifuate itikad zake kinguvu

bas china atakuja kuraisisha maisha kwa itikadi zake, jambo linalomkwamisha USA ko wanabaki kukwamishana wao kwa wao, na hil hii mikwamisho ikome, ni lazima itokee vurugu(vita) ya kuua nguvu hizo ama itokee njia ya amani kuwaunganisha wote mabepar,, na mujue kuwa afrika ikisha tiwa mikononi ni dunia nzma imetiwa mikonon, maana mbishi aliebaki kufuata sera na itikadi mpya za dunia ni muafrika tu, kwa bahat nzur ama mbaya Mungu wa asiri yaan Muumba hawez ruhusu Mwafrika akamatike kiurahisi maan ndye taifa teule, na haitotokea siku muafrika akafutika ktk uso wa dunia hata kitokee kitu gan hawez toweka maana ndye mbegu haris ya ulimwengu, vivo hivyo, hizo jitihada wafanyazo wazungu haztofanikiwa kama malengo yao waliyotegemea kuwa covid ingepukutisha mamilion ya waafrika na weng wangekubar chanjo, majibu yamekuja negative, mwisho uliotabiliwa ni ngumu kutimia maana bado kuna vichwa vya waafrika bado havijaamka, nakuakikishia leo hii kila muafrika akirudsha akil na ufaham kama mwanzo bas kila kitu kitakwisha, yaan dunia itakwishaa, maan steling wa dunia ni muafrika ambaye amekuwa akiwindwa tangu karne na karne, so msiogope wandugu hakuna wakuangamia mapema hivi

FB_IMG_16249105410350704.jpg
 
Back
Top Bottom