Serikali mnawanyonga Walimu!

karumbeta

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2014
Posts
214
Reaction score
39
Asalaam alekyum wana ukumbi!

Jana nimeshuhudia walimu mbalimbali wilaya ya Nyamagana wakipaza sauti zao kwa pamoja; kupinga makato ya sh 10,000/= kwenye mishahara yao kwa lengo la kujenga maabara sekondari.

Kujenga maabara ni jambo jema sana tena sana! Lakini kitendo cha kukata pesa bila kuwashirikisha walimu ni uonevu na ukiukwaji na utawala wa kisheria.

Mbona pesa za kuwalipa wajumbe wa bunge la katiba hazikuleta shida zilipatikana na mabilioni yaliteketea Dodoma? Kwa nini serikali isitafute pesa kama ilivyofanya kwenye bunge la katiba ili maabara zijengwe? Inakuwaje mtumie ubabe kwa njia kandamizi wakati wachache ndiyo wanafaidi keki ya Taifa walio wengi wanaumia!

Ukienda vijijini wananchi wanakamatwa eti hawakwenda kwenye maendeleo ya shule za kata na ujenzi wa maabara; hili linapaswa kukemewa kwa nguvu zote na kila raia mpenda haki; na maendeleo, kwani ccm wanatumia nguvu za wanyonge kujinufaisha wenyewe.

Nawaomba msiwanyanyase walimu laana itawaumbua nyie wote mlio shika madaraka! Kwa nini hamkuwakata wajumbe wa bunge la katiba! badala yake wakatwe watumishi wa umma wakiwemo walimu ambao mishahara yao inaishia kwenye kulipa riba kwenye mabenki?

Watanzania acheni kulala usingizi fanyeni maamuzi magumu! Hii ni vita pambaneni haki itendeke kwani pesa zinatumika vibaya hili halikubariki.

Chanzo taarifa ya habari ITV.
 
Kunawalimu wanaolishangilia hilo. Tanzania tanzaniano
 
Aisee wanakatwa kwenye mshahara????sio wanaambiwa wachange???Ikulu ilishatoa maelezo kuwa ni hiyari kwa mtumishi wa umma kuchanga pesa kwa ajili ya mirad ya maendeleo. Sio lazima-kama wanakatwa wanaweza kushtak maana mkataba wa ajira hausemi hivo na KATIBU MKUU KIONGOZI ALISHALITOLEA UFAFANUZ HILO
 

Ngugu! Ni hatariii!! Ungeona jana mama mmoja (mwalimu) alipokuwa akipaza sauti akitoa machozi ungelia ndugu! Tuwe na busara katika kufanya maamuzi hii ni nchi yetu sote tusikubali hata kidogo.
 
Ngugu! Ni hatariii!! Ungeona jana mama mmoja (mwalimu) alipokuwa akipaza sauti akitoa machozi ungelia ndugu! Tuwe na busara katika kufanya maamuzi hii ni nchi yetu sote tusikubali hata kidogo.
Hapo linaumia Taifa kwa ujumla wake wala sio walimu kama inavyoonekana, walimu walishachagua jinsi ya kuweka mambo yao sawa siku nyingi sana na matokeo si yanasema nini walimu wanafanya!!!!

Ukiongea nao wenyewe wanakuambia kabisa hali mbaya na kama una uwezo peleka mtoto private!!!!
 

Umeua! Hahahaha!!! Walimu ni nomaaa!! Wanachukua hatua mdogomdogo na matokeo ni kweli yalionekana pale serikali ilipopanua magoli ili watoto wafunge kiulaini. Nimekusoma over!
 
Mtwara manispaa walimu wanalazimishwa kuchanga
30,000 ya maabala.
13,000 ya mwenge
5,000 mfuko wa Elimu. HII NDIO SERIKALI SKIVU DUNIANI
 
Walimu hawana umoja kudai haki zao - huwezi kudai haki yako kwa mafungu mafungu!!
 

JIULIZE huyo aliyetoa agizo la KUJENGA MAABARA yeye anakatwa shilingi ngapi katika MSHAHARA wake?!

PIA huyo aliyewakata WAALIMU, yeye AMEJIKATA shilingi ngapi katika mshahara wake kuchangia ujenzi wa maabara.

TATIZO la waalimu pamoja na USOMI wao wanasubiri HAKI yao waletewe kwenye KISAHANI CHA DHAHABU. Hiyo haijawahi na haitatokea kamwe. Wake up teachears of this country.
 
Mtwara manispaa walimu wanalazimishwa kuchanga
30,000 ya maabala.
13,000 ya mwenge
5,000 mfuko wa Elimu. HII NDIO SERIKALI SKIVU DUNIANI

Dah! Inauma sana! Tuwaombe walimu nchi nzima waungane na kuwa kitu kimoja kwani sauti yao ni sauti ya umma! Walimu kunekucha tushikamane tunaibiwa na ccm
 

Hapo sasa! Yani walimu ni shidaaa!! Wako wengi nchi nzima lakini maamuzi hawafanyi! Walimu we need changes amkeni!
 
Hii nchi imeoza,nashangaa dawa ni kuwatoa ccm madarakani basi
 
Walimu hawana umoja kudai haki zao - huwezi kudai haki yako kwa mafungu mafungu!!

Mkuu, waalimu Ni jeshi kubwa lisilojitambua. Hawana umoja Na sijui Kama wanao huo mpango wa kuwa wamoja siku moja. Mi nadhani hawajapewa kitu inauma. Madhila wanayopitia halafu unakuta May Day wanajitoa ufahamu badala ya kuonyesha hisia zao wanabaki wanachekacheka halafu yakiwafika wanakimbilia JF.
Mi nadhani wawakate mishahara pasu kwa pasu Ili kisu kiguse mfupa. Vinginevyo mwenyewe huwa anasema kelele za mlango hazina madhara kwenye usingizi. Watapiga kelele bila kuchukua hatua Na kukatwa mishahara watakatwa, wakitangatanga watapigwa Ili watulie tuliii......
 

Watu mnahasira sana! Tuwaombee walimu jamani wainusuru nchi yetu kwani wao wakiamua changes will come!
 

pamoja na kwamba wewe ni kada wa ccm lakini kwa hili umechangia kizalendo sana mkuu ,sina budi kukupongeza kumbe huwa mnayaona mapungufu pia,ingawa kuna makada wenzio watakuja na maneno ya kukejeli sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…