Serikali, Maendeleo siyo kuipamba Dar es Salaam kwa gharama ya nchi nzima

Hatimaye leo humu JF nimekutana na mtu mwenye mtazamo kama wangu. Nadharau sana kuona jiji la Dar lina wakazi almost milioni 5 wakati linalofuatia, hata robo ya watu halifiki. Ukihesabu skyscrapers za Dar, ujaribu kulinganisha na Majiji yanayofuatia kwa skyscrapers - Arusha na Mwanza, utagundua namna tulivyo bado vilaza kama Nchi.
Wazungu hasa wa Uingereza na Ufaransa, wanajilaumu sana kwa namna walivyoruhusu London na Paris kudominate kila kitu katika maisha ya mataifa hayo na kuyafanya maeneo mengine kuwa marginalized.
Angalao by 1960s - 1990s London ilikuwa inapungua kutokana na uwekezaji kusambaa maeneo yote ya Nchi. Leo hii, watu wabasifia Ujerumani kwa kuwa na balance katika maendeleo bila ya kuwa na dominant metropolitan city - Berlin (East), Hamburg (North), Munich (south), Frankfurt (central) na Cologne (west): yote hiyo inazidiana katika sifa tofauti tofauti.
Ndiyo umuhimu wa Sera ya Majimbo ya CHADEMA huwa naiona inaleta maana.
Ndiyo maana naunga mkono kwa zaidi ya asilimia 100% HQ kwenda Dom angalao kubalance maendeleo kwa maeneo ya mbali.
Ajabu ni kuwa, Kanda ya Ziwa yenye watu zaidi milioni 16, haina Chuo Kikuu cha Umma, kweli?
Nilishangaa sana Watanzania wenzangu wanaodai kuumia na wingi wa abiria kwenye kivuko cha MV Nyerere. Waambieni waende Ukerewe na Uzinza (Maisome, Kome) wataelewa hasara ya kukalia kujenga eneo moja na kusahau mengine - wakazi wa Visiwa hivyo wanezoea shida hizo na wanaona kawaida. Kanda ya Ziwa wanashukuru sana anachofanya Magufuli hasa kutangaza kujenga meli mpya ya kwenda Bukoba na pia kivuko kingine cha Ukara.
Ukisoma meseji za hapa JF ndo utagundua ujuha tulionao. Kuna watu wanadhani iko siku Dar itakuwa kama London au New York. Ukiwauliza wansema tuwe kama nchi za wenzetu. Halafu wanasema eti Dar ni jiji kubwa lakini, hawajiulizi ni kwa nini iwe hivyo. Hawajui matatizo ya kuifanya Dar iwe hivyo. Hawajui kwamba hakuna siku Dar itakuwa nzuri maana kila maskini anakimbilia huko akiamini atafaidika. Maji hakuna, Nyumba ni vibanda, barabara hoi, hospitali uchafu tu!

Umetoa mfano mzuri sana!! Anayeishi Berlin, Ujerumani anaweza kutofika Frankfurt kwa miaka 20! Hana sababu maana kila kitu kipo anapoishi. Leo hii TZ hii kufika Dar au kuishi Dar eti ni sifa. Hata kama anakesha kifua wazi kwa kukosa hewa. Serikali lazima iwe makini. Serikali huendeshwa na watu wachache sana lakini wawe ni wenye akili na maono muhimu sana. Siyo hawa wachangiaji wanaojiandikia kwa hisia za mitandaoni na kuona filamu za Hollywood. Bado tunahangaika kupanua barabara wakati ulaya wanapunguza barabara na kuboresha usafiri wa umma! Halafu tunasema jiji linapendeza.

Wale mbumbumbu nawaomba wafike Lagos, waone flyover kwa wingi halafu waseme kama hizo zimeondoa vurugu za usafiri.
 
Nilitegemea asilimia 90 ya wanainchi wanaotegemea kilimo na wanaoishi vijijini wangepewa kiupaumbele katika kuboresha kilimo cha kisasa,maji safi na salama,huduma bora za afya,kuwa na soko la uhakika wa bidhaa zao nk. Lakini pesa nyingi zinawekezwa kwa asilimia 10 tu za wale wanaoishi mjini.
 
Mapato ya halmashauri ya jiji na siyo mapato yote yanayopatikana Dar
Barrick au Ashanti gold wakienda kuchimba dhahabu shinyanga na Buhemba, wakaichenjua na kupata thamani yake, halafu ofisi yao ya Dar ikaandika cheki ya mrahaba wa serikali, wewe unasema ni mapato yanayotokana na shughuli za kiuchumi Dar?
Kampuni ikipandisha watu mlima Kilimanjaro, ikalipa gharama kwa TANAPA. TANAPA makao makuu pale arusha wakahamisha pesa kwenda hazina au benki kuu iliyoko Dar, wewe unaona ni mapato yatokanayo na utalii wa Dar?

Shule bado. Usitegemee kuambiwa na wanasiasa au redio za FM nawe ukanyonya.
 
Mha wa Kigoma


Oa tu si unafikiri wote humu mashoga!!!
Haha...na wewe ni mtani wangu, ila watani zangu wahaya huwa wanazingua sana, kujisifia kusiko na mpango. Hivi siku hizi wanakula nini, nasikia migomba ilikwisha kwa ugonjwa. Waambie waje mara tuwafundishe kula ugali wa mtama
 
Hivi kwa uelewa wako flyover zinajengwa kama mapambo ya mji na siyo kupunguza foleni? Tabora kuna foleni?
Hahaha..anataka flyover zikajengwe huko kijijini kwao ili kusiwepo upendeleo, hii nchi haiishi vituko
Kweli nchi hii tuna vilaza wengi wenye upeo mdogo sana wa kuchambua
Hebu tuchangie hoja badala ya kuandika vicheko!
Anayeamini flyover zinapunguza foleni ujue hajawahi kumaliza shule.

Afrika hii hakuna mji wenye flyover kuliko Lagos. Dar haitaweza kuzijenga kama Lagos. Je, foleni zimekwisha Lagos? Ni sawa na kuamini kwamba ukipanua barabara unaondoa foleni, that is rubbish! Utaalamu unasema foleni zinapungua kwa kuongeza barabara mbadala na kuimarisha usafiri wa umma, Finito!

Kwa ufahamu dhaifu huu siamini kama huko mitaani mutaweza kupata ajira au hata kuweza kujiajili. Elimu na ufahamu wenu uko matatani! Halafu mtu anaandika kicheko chake akiamini ubongo wake unamuongoza vizuri.
 
Hebu tuchangie hoja badala ya kuandika vicheko!
Anayeamini flyover zinapunguza foleni ujue hajawahi kumaliza shule.

Afrika hii hakuna mji wenye flyover kuliko Lagos. Dar haitaweza kuzijenga kama Lagos. Je, foleni zimekwisha Lagos? Ni sawa na kuamini kwamba ukipanua barabara unaondoa foleni, that is rubbish! Utaalamu unasema foleni zinapungua kwa kuongeza barabara mbadala na kuimarisha usafiri wa umma, Finito!

Kwa ufahamu dhaifu huu siamini kama huko mitaani mutaweza kupata ajira au hata kuweza kujiajili. Elimu na ufahamu wenu uko matatani! Halafu mtu anaandika kicheko chake akiamini ubongo wake unamuongoza vizuri.
Tatizo bangi zinawaharibu, ambaye hana ajira hapa ni nani? tunapoongelea umuhimu wa kuendelea kutenga pesa kuboresha jiji la Dar hatujawa restricted kwenye flyovers. Kwa vilaza kama nyie tutapata shida sana kupiga hatua
 
Katika utawala uliopita tulishuhudia miradi mikubwa ikipangwa kutekelezwa jijini Dar na Pwani. Naikumbuka miradi ya Mloganzila, bandari ya Bagamoyo, by-pass ya daraja la salander, BRT, nk. Hii ni miradi mikubwa sana kwa umaskini wetu. Miradi hiyo ilikuwa mikopo ambayo inalipwa na wananchi wa nchi nzima. Naona tena kuna muendelezo wa miradi mikubwa ndani ya jiji letu bila kujali shida zilizoko mikoani. Rais ametoa tena ahadi ya ujenzi wa flyover zingine ndani ya jiji la Dar es salaam.

Sababu ya maamuzi kama haya haieleweki lakini huenda ni kwa sababu watoa maamuzi wana makazi jijini Dar na wanajisikia kupamba makazi yao. Mikoa ya kati yaani Dodoma, singida, Tabora hadi shinyanga haina hospitali hata moja ya rufaa. Je, kwa nini Muloganzila haikusogezwa mikoa hiyo? Tukumbuke mikoa ya kusini pia haina hospitali ya maana. Ile ya Mbeya ni alama ya malengo na wengi wanajikuta wakielekea hospitali ya wamisionari, Peramiho. Kuna kundi linasifia jiji la Dar na kusema ni kitovu cha biashara. Huo si ukweli. Dar ni njia ya biashara. Mapato yetu makubwa ni Utalii na madini. Utalii uko Serengeti na Kilimanjaro, madini yako kanda ya ziwa. Kwa nini tuendelee kutumia pesa nyingi kiasi hicho kwa hisia ya jiji tu, bila sababu ya maana?

Najaribu kujiuliza, MV Nyerere imepoteza maisha ya watu kwa umaskini wao. Je, leo hii rais hawezi kutangaza maamuzi magumu na kuhamisha hizo pesa za flyover mpya za Dar pamoja na daraja la salander akijumulisha na pesa ya kivuko kipya kilichoahidiwa ili kuwajengea wana Ukara daraja refu kwa safari ya kisiwa chao? Je hatuwezi kuunganisha visiwa vya Jamuhuri hii kwa madaraja badala ya flyover mpya?

Flyover ni nzuri lakini tuwe na kiasi. Tugawane maendeleo badala ya kupamba jiji moja ndani ya nchi kubwa kama hii. Maamuzi mabovu kama haya husababisha ukuaji wa jiji moja na kuongeza wahamiaji kutoka mikoani kila siku. Mifano ya maamuzi kama hayo ziko ktk nchi zetu za kimaskini: Kongo DRC, Afrika ya kati, nk. Huko kila mtu anataka akaishi mji mkuu wa nchi maana hakuna mji mwingine wa maana!

Nchi haiendelei kwa kuipamba Dar. Tunahitaji maji safi, shule za kiwango, hospitali na barabara kwa nchi nzima.
ADA YA MJA KUNENA MUUNGWANA VITENDO
 
Back
Top Bottom