Serikali kutumia shs.bilioni 150 kuchunguza kwanini watoto wanamaliza hawajui kusoma wala kuandika

politiki

JF-Expert Member
Sep 2, 2010
2,376
1,507
Wanafunzi 5,000 waliofaulu hawajui kusoma, kuandika
Send to a friend
Monday, 09 April 2012 20:42
0diggsdigg

Fredy Azzah
IMEBAINIKA kwamba wanafunzi 5,200 waliofaulu na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu, hawajui kusoma wala kuandika.

Kutokana na sababu hiyo, habari kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi zinasema kwamba wanafunzi hao wataachishwa masomo na Serikali inaangalia uwezekano wa kuchukua hatua za kisheria wanafunzi hao na wakuu wa shule wanazotoka ili kukomesha tatizo hilo.

Wanafunzi hao wanatoka katika mikoa yote ya Tanzania bara, isipokuwa Kigoma ambao taarifa zake hazijafika katika wizara hiyo.

Wanafunzi hao wamebanika kutojua kusoma wala kuandika baada ya kupewa majaribio ya kupima uwezo wao wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) baada ya kuripoti shuleni kama ilivyoagizwa na Serikali.

Desemba 14, mwaka jana wakati akitangaza matokeo ya Mitihani ya Darasa la Saba, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo aliagiza wanafunzi wote watakaoingia kidato cha kwanza mwaka huu wapimwe kwanza uwezo wao wa Kusoma na Kuandika.

Agizo hilo lilitokana na udanganyifu uliojitokeza kwenye mtihani huo na kusababisha watoto 9,736 kufutiwa matokeo.

Wanafunzi waliofanya mtihani huo walikuwa 983,545 na waliofaulu ni 567,567. Kati yao wasichana walikuwa 278,377 sawa na asilimia 54.48 na wavulana walikuwa 289,190 sawa na asilimia 62.49.

Akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) mwishoni mwa wiki, Mulugo alisema tathmini inaonyesha kuwa Mkoa wa Kilimanjaro umeongoza kwa kuwa na wanafunzi wengi wasiojua kusoma na kuandika.

"Mkoa wa Kilimanjaro una wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika wapatao 660, Tanga 490 na Dar es Salaam 208," alisema Mulugo bila kutaja matokeo ya mikoa mengine.

"Hili ndilo janga la kitaifa sasa. Siyo hayo mengine ambayo watu wanasema ni majanga ya kitaifa. Lazima tujiulize kwa nini watoto wanamaliza darasa la saba wakiwa hawajui kusoma wala kuandika na halafu wanafaulu?" alihoji kuongeza:

"Je, siku hizi hakuna tena somo la kusoma na kuandika? Kwa nini mtoto amalize shule bila kuwa na maarifa ya KKK? Mitaala (mitalaa) mnayoandika kwa nini hamsaidii mtoto katika hili? Nataka leo nijue tatizo liko wapi, mengine (matatizo) ya Serikali; walimu, vitabu, miundombinu na majibu yake sisi tunayo."

"Jambo la kusikitisha kuna mpaka baadhi ya wanafunzi wa kidato cha tatu, ambao hawajui kusoma wala kuandika. Tulipofikia siyo pazuri hata kidogo, lazima tuwe makini jamani. Tuheshimu Baraza la Mitihani (Necta) tupate ufumbuzi wa mambo haya taifa hili ni letu sote, lazima tuhakikishe linasimama imara."

Alisema Serikali kwa upande wake, imejipanga kufanya utafiti na kujua chanzo cha tatizo na kuwa imepata Sh150bilioni kutoka Global Partnership for Education (GPE), kwa ajili hiyo.

Kaimu Mkurugenzi wa TET, Habib Fentu alisema mitalaa waliyoandika imesisitiza mwalimu kufanya tathmini ya kile alichofundisha kila baada ya mada husika kumalizikia.

"Kwa hiyo hapa sasa suala la uwajibikaji linakuja, inakuwaje mtoto amalize darasa la saba akiwa hajui kusoma, kuandika wala kuhesabu na mwalimu wa darasa yupo, mwalimu wa taaluma, mwalimu mkuu na kamati ya shule vipo?"

Katika matokeo ya darasa la saba yaliyotangazwa mwaka jana, Mkoa wa Manyara uliongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi waliofutiwa matokeo ukifuatiwa na Arusha.


MY TAKE: Pesa hizi zingeweza kutumika kujaza vitabu vya kiada, kuongeza waalimu na kuongeza madarasa ili
kupunguza idadi ya wanafunzi kujazana ktk darasa moja.
 
Unapofanya utafiti kwa jambo lilowazi unatafiti nini?
Walimu morari ya kufundisha imeshuka kama siyo kufa kabisa. Na watoto wasipofaulu shule au mkuu wa shule anawajibishwa na mabosi wake. Kukwepa adhabu, kwanini mwalimu au walimu wasiwafanyie mitihani wanafunzi na shule yao ikaonekana imefaulisha? Fedha hizo zingetumika kuwa jengea mazingira mazuri walimu na shule ili walimu hawa warudishe imani kwa serikali yao kuwa inawajali katika masirahi yao. Pandisha mishahara ya walimu na wapewe vitendea kazi tuone kama hilo tatizo halijaisha.
 
wanilipe mimi wala siitaji kufanya utafiti nitawashauri wazalishe waalimu wa kutosha, wana improve maslahi ya waalim, waongeze vifaa vya kufundishia na kujenga madarasa ili kupunguza idadi ya wanafunzi kwenye darasa moja ili waalim wawe na one to one discussion na wanafunzi wao
 
Waziri anakiri kwamba anajua matatizo ya walimu, vitabu, madarasa na mengineyo. Sasa kama anajua hayo matatizo, uchunguzi/utafiti ni wa nini?

Labda kama anataka kutafiti kwamba inakuwaje mwanafunzi ambaye hajui kusoma wala kuandika anafaulu na kuchaguliwa kuingia sekondari.

Lakini kiini cha kutojua kusoma na kuandika ni hicho alichokitaja hapo. Shule unakuta ina mwalimu 1 au 2, atafundishaje madarasa 7 ambapo kuanzia darasa la nne, kila darasa lina wastani wa masomo 8? Hakuna vitabu na wanasomea chini ya mti. Mtoto akiamua kwenda shule mara moja kwa wiki utamlaumu?

Mara nyingi huwa nasema Tanzania tuna fedha nyingi sana ili hatujui priorities na matokeo yake tunaishia kutumia kwenye warsha, semina na makongamano na huo utafiti mbuzi wa kutafiti kitu ambacho majibu yake yako obvious.
 
Duh! Haiingii akilini kabisa!? Huu ni ufujaji uliopitiliza kiasi kama ni kweli basi hatuna serikali! kinachothibitika hapa ni kwamba baada ya viongozi kubanwa kila angle wasiibe pesa ya nchi mathalani kulipa DOWANS. Sasa wanajaribu kila njia kuiba au kupata chanel ya kuiba ambayo ni justifiable!
 
Hii nikuonyesha dhahiri kabisa kwamba serekali ya JK haiko makini hata kidogo kwa sababu zifuatazo huwezi kuwapata waalimu wa mteremko (crash program) walio-fail form four kuja kufundisha watu unotarajia wafauli wakiwa wanauwezo zaidi ya mwalimu, haiwezekani wakaguzi wa elimu na wizara wakaridhika kwa maelezo ya hao waalimu juu ya kufeli kwa hao wanafunzi.
 
Jamani huu ni ulaji wa watu na vigogo tu hakuna lolote. Hizo hela waboreshe maslai ya walimu tu hapo ndio watoto wataanza kufundishwa lazivyo mgomo baridi bado utaendelea na taaluma itazidi kushuka. Hata leo bungeni swali aliulizwa hawa gasia kwanini graduate mwalimu na daktari mishahara yao tofauti ni kubwa na waziri alivyojibu ni dhahiri dharau kwa taaluma ya ualimu. Kazi tunayo hizo hela za kula bata eti utafiti na tatizo linajulikana. Wadanganyika.
 
Jamani, wanafunzi hawana vitabu, madawati, walimu na library mnaunda tume ili ifanye nini?
 
kikwete aliulizwa kwa nini AFRIKA MASKINI AKASEMA NI KWA VILE HAINA PESA ETI.
MTU HAJUI KUSOMA NA KUANDIKA SASA NANI HAUI SABABU? KWELI HII NCHI HAMUIPENDI KWELI MMESHAJISAHAU KABISAAAAA
 
Wanafunzi 5,000 waliofaulu hawajui kusoma, kuandika Send to a friend
Monday, 09 April 2012 20:42
0diggsdigg

Fredy Azzah
IMEBAINIKA kwamba wanafunzi 5,200 waliofaulu na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu, hawajui kusoma wala kuandika.

Kutokana na sababu hiyo, habari kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi zinasema kwamba wanafunzi hao wataachishwa masomo na Serikali inaangalia uwezekano wa kuchukua hatua za kisheria wanafunzi hao na wakuu wa shule wanazotoka ili kukomesha tatizo hilo.

Wanafunzi hao wanatoka katika mikoa yote ya Tanzania bara, isipokuwa Kigoma ambao taarifa zake hazijafika katika wizara hiyo.

Wanafunzi hao wamebanika kutojua kusoma wala kuandika baada ya kupewa majaribio ya kupima uwezo wao wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) baada ya kuripoti shuleni kama ilivyoagizwa na Serikali.

Desemba 14, mwaka jana wakati akitangaza matokeo ya Mitihani ya Darasa la Saba, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo aliagiza wanafunzi wote watakaoingia kidato cha kwanza mwaka huu wapimwe kwanza uwezo wao wa Kusoma na Kuandika.

Agizo hilo lilitokana na udanganyifu uliojitokeza kwenye mtihani huo na kusababisha watoto 9,736 kufutiwa matokeo.

Wanafunzi waliofanya mtihani huo walikuwa 983,545 na waliofaulu ni 567,567. Kati yao wasichana walikuwa 278,377 sawa na asilimia 54.48 na wavulana walikuwa 289,190 sawa na asilimia 62.49.

Akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) mwishoni mwa wiki, Mulugo alisema tathmini inaonyesha kuwa Mkoa wa Kilimanjaro umeongoza kwa kuwa na wanafunzi wengi wasiojua kusoma na kuandika.

"Mkoa wa Kilimanjaro una wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika wapatao 660, Tanga 490 na Dar es Salaam 208," alisema Mulugo bila kutaja matokeo ya mikoa mengine.

"Hili ndilo janga la kitaifa sasa. Siyo hayo mengine ambayo watu wanasema ni majanga ya kitaifa. Lazima tujiulize kwa nini watoto wanamaliza darasa la saba wakiwa hawajui kusoma wala kuandika na halafu wanafaulu?" alihoji kuongeza:

"Je, siku hizi hakuna tena somo la kusoma na kuandika? Kwa nini mtoto amalize shule bila kuwa na maarifa ya KKK? Mitaala (mitalaa) mnayoandika kwa nini hamsaidii mtoto katika hili? Nataka leo nijue tatizo liko wapi, mengine (matatizo) ya Serikali; walimu, vitabu, miundombinu na majibu yake sisi tunayo."

"Jambo la kusikitisha kuna mpaka baadhi ya wanafunzi wa kidato cha tatu, ambao hawajui kusoma wala kuandika. Tulipofikia siyo pazuri hata kidogo, lazima tuwe makini jamani. Tuheshimu Baraza la Mitihani (Necta) tupate ufumbuzi wa mambo haya taifa hili ni letu sote, lazima tuhakikishe linasimama imara."

Alisema Serikali kwa upande wake, imejipanga kufanya utafiti na kujua chanzo cha tatizo na kuwa imepata Sh150bilioni kutoka Global Partnership for Education (GPE), kwa ajili hiyo.

Kaimu Mkurugenzi wa TET, Habib Fentu alisema mitalaa waliyoandika imesisitiza mwalimu kufanya tathmini ya kile alichofundisha kila baada ya mada husika kumalizikia.

"Kwa hiyo hapa sasa suala la uwajibikaji linakuja, inakuwaje mtoto amalize darasa la saba akiwa hajui kusoma, kuandika wala kuhesabu na mwalimu wa darasa yupo, mwalimu wa taaluma, mwalimu mkuu na kamati ya shule vipo?"

Katika matokeo ya darasa la saba yaliyotangazwa mwaka jana, Mkoa wa Manyara uliongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi waliofutiwa matokeo ukifuatiwa na Arusha.

MY TAKE: Pesa hizi zingeweza kutumika kujaza vitabu vya kiada, kuongeza waalimu na kuongeza madarasa ili
kupunguza idadi ya wanafunzi kujazana ktk darasa moja.
Ujinga mtupu....haya ni matumizi mabaya ya fedha ya walipa kodi....wanataka wapige deal kwenye hizi pesa kama walivyozoea....Tatizo la watoto kumaliza wakiwa hawajui kusoma na kuandika serikali wanalijua sana tu......mbona zamani haikuwa hivi????jibu la tatizo hili ni kuwahudumia waalimu tu.....hamna ujanja mwingine....wewe leo unataka watoto wajue kusoma na kuandika wakati wale unaotgemea wawafundishe(waalimu)unawadharau na huwalipi vizuri..unategemea nini???na bado...kama itaendelea hivi itakuja kufika watoto wanamaliza form four hawajui kitu.....dawa ni waalimu tu.....hudumieni waalimu watoto wenu wafundishwe vizuri...
 
Kwanini wagharamike kufanya utafiti wakati inaeleweka wazi kuwa walimu wapo kwenye mgomo baridi siku nyingi.
 
Nyie endeleeni tu kutoa misharaha midogo kwa walimu, mtaona kama matatizo ya elimu yatapungua. Na bado huu ni mwanzo, si mmeamua kuwekeza kwenye madarasa, semina, n.k. Bila kujali mishahara ya walimu? mgomo kama kawa unaendelea, hadi siku mtakapoamua kuwathamini walimu ndio mtaona changes. Si huwa mnashughulikia ya madokta kwa sababu wataua miili ya watu, walimu wameamua kuua akili.
 
Mitihani yenyewe ni multiple choice ABCD hadi hisabati.

Nani atafeli? Labda Mwanaasha type
 
Wanafunzi 5,000 w
42




Alisema Serikali kwa upande wake, imejipanga kufanya utafiti na kujua chanzo cha tatizo na kuwa imepata Sh150bilioni kutoka Global Partnership for Education (GPE), kwa ajili hiyo.


Upuuzi mtupu! Hajui kuwa walimu wako kwenye mgomo toka Mkoba autangaze kabla ya 2012!!!!!!????? Hizo hela si mlipe madai ya walimu!!!!
 
Kweli wacha wenye meno watafune mifupa kwa kuwa bado meno ipo! Utafiti wa kutumia 150 billion uko wapi? Hizo pesa ni za kugawana tu. Wanipe million moja tu kesho nawapa sababu kwa kuwa ziko wazi na hazihitaji utafiti.
 
Ujinga mtupu....haya ni matumizi mabaya ya fedha ya walipa kodi....wanataka wapige deal kwenye hizi pesa kama walivyozoea....Tatizo la watoto kumaliza wakiwa hawajui kusoma na kuandika serikali wanalijua sana tu......mbona zamani haikuwa hivi????jibu la tatizo hili ni kuwahudumia waalimu tu.....hamna ujanja mwingine....wewe leo unataka watoto wajue kusoma na kuandika wakati wale unaotgemea wawafundishe(waalimu)unawadharau na huwalipi vizuri..unategemea nini???na bado...kama itaendelea hivi itakuja kufika watoto wanamaliza form four hawajui kitu.....dawa ni waalimu tu.....hudumieni waalimu watoto wenu wafundishwe vizuri...
Hivi unadhani hawalijui hilo?? Wanajua fika? CCM sasa wanatapatapa kutafuta watakapochota mabilioni ya uchaguzi 2015. Chunga sana tabia ya CCM. Hakuna kitu kama hicho eti hawajui kwanini wanafunzi wanafeli.
Kwanza huyo Waziri anastahili kuwajibishwa kabla ya yote, hakafu hatua zianze kuchukuliwa.
Mengi tutayafahamu tunavyozidi kukaribia 2015.
 
Back
Top Bottom