Serikali kupeleka muswada kuzuia ndoa chini ya miaka 18

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,811
4,533
1680770332299.png

Serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria imesema ina nia ya kupeleka muswada wa mabadiliko ya sheria ya ndoa 1971 katika Bunge hili la Bajeti linaloendelea, ili kuweka umri wa miaka 18 kama umri wa chini wa kuolewa na kuoa.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro amesema hayo leo Ofisi kwake, Mtumba Dodoma alipokutana na kufanya mazungumzo na Jukwaa la Wakurugenzi Wanawake waliowakilisha Mashirika takribani 400 yanayotetea haki za Wanawake, Wasichana na Watoto Nchini Tanzania.

Wakurugenzi kutoka Jukwaa la Wakurugenzi Wanawake wametumia fursa hiyo kumhakikishia Waziri na Ofisi yake ushirikiano katika kuhakikisha mchakato huo unapelekea kuwa na sheria nzuri yenye mlengo wa kujinsia kwa ajili ya kuimarisha ulinzi kwa Watoto hasa Watoto wa kike.

Kwa mujibu wa sheria ya ndoa inayotumika sasa ya mwaka 1971 (kifungu namba 13), Mtoto wa kike anaweza kuolewa kuanzia umri wa 14 kwa ridhaa ya Mahakama na kifungu namba 17 kinasema anaweza kuolewa kwa miaka 15 kwa ridhaa ya Wazazi lakini sheria hiyohiyo inasema Mtoto wa kiume ananza kuoa kuanzia umri wa miaka 18.
 
Hili suala linahitaji umakini sana. Kwanza nini lengo la hao wanaotaka kubadillisha Sheria hiyo ya ndoa ya Mwaka 1971. Kwa sasababu hizi taasisi za kijamii siku hizi zina malengo mengi sana, likiwemo la kueneza ushoga nchini mwetu. Sasa isije wakaja tena na sheria ya kutaka wanaume waowane wao kwa wao na wanawake waowane wao kwa wao.

Kwasababu wanataka kuzuia ndoa kwa mabinti walio chini ya Miaka 18, lakini hawazuii mabinti hao kufanya ngono chini ya miaka 18 au wakiwa bado ni wanafunzi. Tena wanawahamashisha wafanye ngono lakini watumie uzazi wa mpango. Kumbuka lile tangazo la Habiba na Shangazi yake.

Kama haitoshi, pia wanahamasishwa wabebe mimba halafu waende wa kazae na warudi kuendelea na shule. Yaani wao kuzaa bila ndoa ni halali kisha warudi waendelee na Shule lakini ni Marufuku kuolewa hatakama sio wanafunzi hadi wafikike umri huo wanaoutaka wao.

Sitaki kuamini kua watu wenye Akili na Busara wameisha Duniani.
 
Back
Top Bottom