Serikali kubana matumizi zaidi, sasa kuunganisha taasisi zote zinazofanya kazi zinazofanana

chinchilla coat

JF-Expert Member
May 16, 2016
5,107
10,969


Serikali imepanga kuunganisha taasisi zote zinazofanya kazi zinzazofanana ili kuendelea kubana matumizi zaidi, hayo yamesemwa na waziri Angela Kairuki alipokuwa anajibu swali la mbunge wa viti maalum Ruth Molel aliyetaka kujua serikali imeokoa kiasi gani kwa kuunganisha wizara.

Amesema serikali inafanya uchambuzi kujua taasisi zinazofanya majukumu yanayofanana na kisha kuunganishwa na wafanyakazi wake kuondolewa.

Amesema pia kama kuna idara na taasisi ambazo zitakuwa hazina majukumu ya kutosha kuhalalisha majukumu yake zitaondolewa.
 
Dah, mapema sana mbona, ila ni muhimu kwa kuwa kulikuwa na mlundikano mkubwa wa taasis zinazoongeza urasimu wa kutoa huduma, ila ni vizur sana ikafanywa kwa makini kupunguza athari hasa za watakaopoteza ajira zao kwa sababu hizo
 


Serikali imepanga kuunganisha taasisi zote zinazofanya kazi zinzazofanana ili kuendelea kubana matumizi zaidi, hayo yamesemwa na waziri Angela Kairuki alipokuwa anajibu swali la mbunge wa viti maalum Ruth Molel aliyetaka kujua serikali imeokoa kiasi gani kwa kuunganisha wizara.

Amesema serikali inafanya uchambuzi kujua taasisi zinazofanya majukumu yanayofanana na kisha kuunganishwa na wafanyakazi wake kuondolewa.

Amesema pia kama kuna idara na taasisi ambazo zitakuwa hazina majukumu ya kutosha kuhalalisha majukumu yake zitaondolewa.

Kama watafanya ivyo sawa ila utaanza lini utaratibu huo?
 
Haya sina shida nayo make yalianza toka Tanganyika iwepo, mjerumani aliyoyajenga yalibomolewa na mwingereza, aliyojenga mwingereza yalibomolewa na mchina kupitia kwa mwl.Nyerere, yaliyojengwa na Nyerere yalibomolewa na mwinyi mzee wa ruksa, yaliyojengwa na mwinyi yalibomolewa na mkapa mzee wa globalization, yaliyojengwa na mkapa yalibomolewa na kikwete mzee wa WAMA, yaliyojengwa na kikwete yanabomolewa na magufuli mzee wa bana matumizi.

Na ndiyo dira ya taifa kila anaekuja itategemea anaegemea upande upi.
 
Back
Top Bottom