Serikali kuanza 'kuchunguza' matangazo ya massage mitandaoni

Serikali kuanza 'kuchunguza' matangazo ya massage mitandaoni

McLaren

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2025
Posts
1,089
Reaction score
3,444
Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, imeanza kufuatilia kwa kina malalamiko ya wananchi kuhusu matangazo ya huduma za massage yanayosambazwa mitandaoni, hususan Instagram.

Waziri Dkt. Dorothy Gwajima ameeleza kuwa hatua hiyo inakuja baada ya kubainika kuwa baadhi ya matangazo hayo yanachochea mmomonyoko wa maadili na hayazingatii utamaduni na misingi ya Kitanzania.

Dkt. Gwajima amebainisha kuwa Serikali itafanya uchunguzi wa kina ili kubaini usajili wa vituo hivyo pamoja na uhalali wa maudhui wanayochapisha kwa mujibu wa sheria na kanuni za maadili.

Licha ya Waziri kukiri kutoyaona matangazo hayo moja kwa moja kwenye kurasa zake, amewapongeza wananchi kwa kuendelea kuwasilisha vielelezo na ushahidi wa picha na video ambao utasaidia katika hatua za kisheria zinazofuata.

Aidha, Serikali imetoa onyo kali kuwa haitasita kuvifunga vituo na kuwafungulia mashtaka wahusika wote watakaobainika kukiuka taratibu, ikirejea hatua kali zilizowahi kuchukuliwa hapo awali.

Wananchi wamehimizwa kuendelea kuwa walinzi wa maadili kwa kuhifadhi na kutoa ushahidi wa matangazo yoyote yanayokiuka utu na heshima ya jamii ili kudumisha nidhamu na utulivu ndani ya nchi.

itv.png
 
Serikali ya hovyo. Kama maisha ni magumu hata kutoa ruzuku kwenye mafuta tu wameshinda maisha ya mlala hoi yamekuwa magumu balaa. Watu wanawaza massage.
 
Serikali mna mambo mengi sana ya msingi ya kuchunguza! Mfano mauaji na utekaji wa raia, wizi na ufisadi kwenye fedha za walipa kodi, utoroshwaji wa raslimali zetu kwenda nje ya nchi, utakatishaji wa fedha, ujambazi na uhalifu mwingine kwenye jamii, nk.

Na bahati nzuri Waziri mwenye dhamana upo humu jukwaani. Mimi nakushauri dada yangu mzuri kabisa Dorothy Gwajima, achana na hizi mambo. Waacheni wananchi wapate riziki zao.

Hata mimi ni vile tu kipato changu ni kidogo. Ila ningekuwa nina kipato kikubwa, siku moja na mimi ningeenda kufanyiwa hiyo massage na kufikia ile hatua ya mwisho kabisa ya 'happy ending' 😋
Kiufupi msiyafanye maisha yetu kuwa magumu saaana! Au mnataka ubakaji ushamiri kwenye jami yetu?
 
Sitawalaumu saana coz ndivo akili zenu zilivo. Watekaji hamfatilii, wauaji hamfatilii, tanesco inaibia watu hamfatilii eti mfatilie watu kushkwashka miili na mikono laini. Ni kipi mnachunguza hapo na huku massage ni kushkwa shkwa na kukutanisha vikojoleo. Buure kabisa!
 
Back
Top Bottom