Serikali kinara wa kunyanyapaa wagonjwa wa UKIMWI

Tyupa

JF-Expert Member
Aug 11, 2013
802
653
Serikali pamoja na vyombo vingine vya haki za binadamu vimekuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu juu ya kuondoa aina zote za kunyanyapaa wagonjwa wa ukimwi.

Kuwatenga wagonjwa wa ukimwi kwa jinsi yeyote ile ni aina ya unyanyapaji ulio mbaya zaidi kuliko aina zingine zote.

Lakini wakati serikali na vyombo vingine vya haki za binadamu vinafanya jitihada za kuondoa aina zote za unyanyapaji kwa wagonjwa wa ukimwi, serikaki hiyo hiyo ndio kinara wa unyanyapaaji.

Mimi ni moja wa watoa huduma kwa wagonjwa wa ukimwi. Hospitali zote ziwe za serikali au binafsi zina vituo maalum za kutolea huduma za matibabu zinazojulikana kama CTC yaani "care and treatment center".

Ugonjwa wa ukimwi hauambukizwi kwa njia ya hewa wala kugusana kwa hiyo kuwatenga wagonjwa hawa na wagonjwa wengine wanaopata matibabu kwa kuwajengea mabanda yao pembeni ni moja ya aina ya unyanyapaji uliokubuhu.Ugonjwa wowote alionao mgonjwa ni siri yake na daktari wake.

Kuwajengea mabanda yao (CTC) wagonjwa wa ukimwi ni moja ya njia ya kuwanyanyapa.
Wanapokuwa wamekusanyika pamoja wanapewa huduma, jamii nyingine moja kwa moja wanakuwa wametambua kuwa wale wote wanaumwa ukimwi.

Hapa siri ya ugonjwa wa mhusika unakuwa umetangazwa kwa asili mia moja.Hali hii ya kuwatangazia siri ya ugonjwa alionao mhusika imeleta changamoto zifuatazo katika kupambana na mambukizi ya ukimwi:

Kwanza wagonywa wengi wanasita kwenda kupima afya zao.Wagonjwa wengi huhama vituo vilivyoko jirani na nyumbani kwake kwa kuhofia kuonwa na watu wanaomfahamu.
Inakuwa nafuu kwake kwenda mbali wasikomjua kupata huduma.

Baadhi ya wagonjwa wamekuwa wakitumia fedha kununua dawa za ARV kinyemela kwa sababu hawataki ugonjwa wao ujulikane na watu wengine kwa kutengwa kwenye mabanda ya CTC.

Rai yangu kwa mamlaka zinazohusika na mipango hii hasa wizara ya afya iweke utaratibu ambao wagonjwa wote wenye kisonono, malaria, nimonia, ukimwi nk.wapate huduma kwa kuchangywa pamoja.Daktari pekee ndiye abebe dhamana ya kujua SIRI za magojwa kwa wagonjwa wake wote.
 
Wenyewe ndio hawapendi wachanganyike na wagonjwa wengine eti kwa sababu watajulikana kwa hiyo sirikari ikabidi iwawekee faragha ili wachukue dawa zao kwa uhuru sasa wewe unakuja na hoja nyepesii kama ivo sijui watakueleje sasa. Btw mi naona ni utaratibu mzuri.
 
Serikali pamoja na vyombo vingine vya haki za binadamu vimekuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu juu ya kuondoa aina zote za kunyanyapaa wagonjwa wa ukimwi.

Kuwatenga wagonjwa wa ukimwi kwa jinsi yeyote ile ni aina ya unyanyapaji ulio mbaya zaidi kuliko aina zingine zote.

Lakini wakati serikali na vyombo vingine vya haki za binadamu vinafanya jitihada za kuondoa aina zote za unyanyapaji kwa wagonjwa wa ukimwi, serikaki hiyo hiyo ndio kinara wa unyanyapaaji.

Mimi ni moja wa watoa huduma kwa wagonjwa wa ukimwi. Hospitali zote ziwe za serikali au binafsi zina vituo maalum za kutolea huduma za matibabu zinazojulikana kama CTC yaani "care and treatment center".

Ugonjwa wa ukimwi hauambukizwi kwa njia ya hewa wala kugusana kwa hiyo kuwatenga wagonjwa hawa na wagonjwa wengine wanaopata matibabu kwa kuwajengea mabanda yao pembeni ni moja ya aina ya unyanyapaji uliokubuhu.Ugonjwa wowote alionao mgonjwa ni siri yake na daktari wake.

Kuwajengea mabanda yao (CTC) wagonjwa wa ukimwi ni moja ya njia ya kuwanyanyapa.
Wanapokuwa wamekusanyika pamoja wanapewa huduma, jamii nyingine moja kwa moja wanakuwa wametambua kuwa wale wote wanaumwa ukimwi.

Hapa siri ya ugonjwa wa mhusika unakuwa umetangazwa kwa asili mia moja.Hali hii ya kuwatangazia siri ya ugonjwa alionao mhusika imeleta changamoto zifuatazo katika kupambana na mambukizi ya ukimwi:

Kwanza wagonywa wengi wanasita kwenda kupima afya zao.Wagonjwa wengi huhama vituo vilivyoko jirani na nyumbani kwake kwa kuhofia kuonwa na watu wanaomfahamu.
Inakuwa nafuu kwake kwenda mbali wasikomjua kupata huduma.

Baadhi ya wagonjwa wamekuwa wakitumia fedha kununua dawa za ARV kinyemela kwa sababu hawataki ugonjwa wao ujulikane na watu wengine kwa kutengwa kwenye mabanda ya CTC.

Rai yangu kwa mamlaka zinazohusika na mipango hii hasa wizara ya afya iweke utaratibu ambao wagonjwa wote wenye kisonono, malaria, nimonia, ukimwi nk.wapate huduma kwa kuchangywa pamoja.Daktari pekee ndiye abebe dhamana ya kujua SIRI za magojwa kwa wagonjwa wake wote.
Umesema sahihi Mkuu!
 
Mimi ni mmoja wa watoa huduma kwa wagonjwa hawa, kwa hiyo ni kweli matatitizo haya yapo.Utamwona mgonjwa kwa mfano anaishi Mbagala lakini atakwenda Temeke kupewa huduma hiyo, na wa Temeke ataondoka kwenda Mwananyamala kujificha huko ili apate huduma hiyo.Wengi wanaobaki kwenye maeneo yao ni wale ambao hawana uwezo wa kusafiri kwenda mbali.Njia kuu ya kuambukizwa ukimwi ni njia ya kujamiani, sasa basi mgonywa yeyote wa ukimwi hua anajenga hisia kuwa watu wakisha mgundua kuwa ni mwathirika atadhani kwamba watu watamwona yeye alikuwa mzinzi wa kupindukia.Hisia za aibu ya namna hii ndiyo inayowafanya wagonjwa wa ukimwi watange tange kutafuta vituo vya faragha vya kuwahudumia.
 
Kwenye ajira hasa serikalini nadhani ukikutwa nao sio kigezo cha kukosa kazi.Ila baadhi ya taasisi za serkali kama majeshi ukikutwa nao huwezi kuajiriwa.Nadhani sababu kuu ni kwa vile kazi za majeshi muda mwingi zinaambatana na shughuli za mabavu mabavu.Lakini nadhani hata wao baadae akili ikiwaajia watafuta kigezo hicho cha kukosa kazi ukikutwa na ukimwi.Ikumbukwe kuwa ukimwi ni janga la dunia na ni mzigo wa kila taasisi na kila mtu.Majeshi hayo hayo yanayo kataa kuajiri wenye ukimwi wanajeshi wao ndio wahanga wakubwa na gonjwa hili maana wanapuputika kweli kama majani ya miembe.Ni heri hata hayo majeshi wangeondoa tu hicho kigezo cha ukikutwa nao unakosa kazi kwa sababu kuna HIV infection yaani mtu ana virusi lakini haumwi chochote na inaweza kumchukua miaka mingi ndio aanze kuumwa.Kwa hiyo watu wa hali hii wapewe tu ajira.Halafu kuna AIDS diseases yaani mtu amechoka kwa sababu magonjwa nyemelezi tayari yamemzingira mwili mzima.Kwa hawa ndio wangekuwa wakikutwa nao wasipewe ajiri kwa sababu tayari hawana nguvu tena za kuitumikia hiyo kazi wanayoiomba.
 
Mgeni jina lake nani......
Ameingia chumbani kwa baba na mama...
NB
Kinga ni bora kuliko tiba ...bila...inawezekana kabisa
 
Serikali ya Uganda imefanikiwa kuondoa hii kero ya kuwanyanyapaa wagonjwa baada ya kuondoa vituo vya kuwatenga vya kutolea huduma kwa wagonjwa wa ukimwi.Wagojwa wote wanachanganyikana pamoja na ni vigumu mtu kujua shida ya mgonjwa mwingine.
 
Mkuu hiyo point yako Ni ya msingi, lakini unafahamu kuwa wafanyakazi wengi wa CTC wana special training na wameandaliwa kwa kazi hiyo hasa Kati vituo vya afya?
Tofauti na ilivyo kujipanga kwa kila mgonjwa kwenda kwa CO au AMO au MD ambao wengine wana moody mbaya

Huku ukijua dhahiri kuwa kuwatunza na kuwalea wagonjwa Kuna emotion ndani yakee na pia Kuna hajaa ya kuchukuliana kwa wepesi?
Labda hoja yako ingekuwa, wahudumu wote wa afya wapewe mafunzo maalum kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI kitu ambacho ni kigumu, maana ile kazi inahitaji uvumilivu na hekima Sana,

Niliwahi ona mama aliejifungulia nyumbani mapacha kaletwa vingunguti h/c kupimwa wote wameathirika...ilikuwa vilio Sana hadi walio nje wakajua nini kinaendelea lakini namna yule mtoa huduma alivyo I-handle ile situation vizuri, ndipo utaelewa umuhim wa kuwa na clinic za peke Yao
Kama ilivyo kwa Sukari na Onco, Derma na hata Macho
Sidhani kama ni kunyanyapaliwa mkuu, specialization inasaidia sana
 
Serikali ya Uganda imefanikiwa kuondoa hii kero ya kuwanyanyapaa wagonjwa baada ya kuondoa vituo vya kuwatenga vya kutolea huduma kwa wagonjwa wa ukimwi.Wagojwa wote wanachanganyikana pamoja na ni vigumu mtu kujua shida ya mgonjwa mwingine.
Hapa sasa utawatesa kuwaweka kwenye foleni muda mrefu. Mi nafikiri nia ya serikali ilikuwa ni njema tu na bila shaka ilishirikisha wadau wakiwemo baadhi ya waathirika. Naamini dhamira ilikuwa ni kuwapunguzia adha waathirika wasikae muda mrefu kwenye foleni. Ni mtizamo tu.
 
Mkuu hiyo point yako Ni ya msingi, lakini unafahamu kuwa wafanyakazi wengi wa CTC wana special training na wameandaliwa kwa kazi hiyo hasa Kati vituo vya afya?
Tofauti na ilivyo kujipanga kwa kila mgonjwa kwenda kwa CO au AMO au MD ambao wengine wana moody mbaya

Huku ukijua dhahiri kuwa kuwatunza na kuwalea wagonjwa Kuna emotion ndani yakee na pia Kuna hajaa ya kuchukuliana kwa wepesi?
Labda hoja yako ingekuwa, wahudumu wote wa afya wapewe mafunzo maalum kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI kitu ambacho ni kigumu, maana ile kazi inahitaji uvumilivu na hekima Sana,

Niliwahi ona mama aliejifungulia nyumbani mapacha kaletwa vingunguti h/c kupimwa wote wameathirika...ilikuwa vilio Sana hadi walio nje wakajua nini kinaendelea lakini namna yule mtoa huduma alivyo I-handle ile situation vizuri, ndipo utaelewa umuhim wa kuwa na clinic za peke Yao
Kama ilivyo kwa Sukari na Onco, Derma na hata Macho
Sidhani kama ni kunyanyapaliwa mkuu, specialization inasaidia sana
Mimi naungana nawewe mkuu. Nadhani hiki ndicho kilichofanya serikali ifanye hivyo. Lengo sio kunyanyapaa bali ni kuboresha huduma
 
Mkuu hiyo point yako Ni ya msingi, lakini unafahamu kuwa wafanyakazi wengi wa CTC wana special training na wameandaliwa kwa kazi hiyo hasa Kati vituo vya afya?
Tofauti na ilivyo kujipanga kwa kila mgonjwa kwenda kwa CO au AMO au MD ambao wengine wana moody mbaya

Huku ukijua dhahiri kuwa kuwatunza na kuwalea wagonjwa Kuna emotion ndani yakee na pia Kuna hajaa ya kuchukuliana kwa wepesi?
Labda hoja yako ingekuwa, wahudumu wote wa afya wapewe mafunzo maalum kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI kitu ambacho ni kigumu, maana ile kazi inahitaji uvumilivu na hekima Sana,

Niliwahi ona mama aliejifungulia nyumbani mapacha kaletwa vingunguti h/c kupimwa wote wameathirika...ilikuwa vilio Sana hadi walio nje wakajua nini kinaendelea lakini namna yule mtoa huduma alivyo I-handle ile situation vizuri, ndipo utaelewa umuhim wa kuwa na clinic za peke Yao
Kama ilivyo kwa Sukari na Onco, Derma na hata Macho
Sidhani kama ni kunyanyapaliwa mkuu, specialization inasaidia sana
Kwenye sehemu za kazi kuna semina na washa, humo itatolewa elimu mpya juu ya kitu fulani.Kwa hiyo special training inaweza kutolewa pia hata kwa wahudumu wengine ambao awali hawa kuwa na mafunzo juu ya CTC.
 
Back
Top Bottom