Serikali Izuie Watu Kuja Dar...

Serikali Izuie Watu Kuja Dar...

Kijakazi

Platinum Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
9,313
Reaction score
14,983
Nafikiri wakati umefika sasa kwa Serikali ianze kuzuia watu kutoka Mikoani kuja Dar, tumetosha sasa! ikiwezekana Waruhusiwe wale tu ambao wamepata kazi au walioitwa kwenye usahili... Hali inatisha sana ukienda Ubungo Mabasi yanakuja yamejaa na yanaondoka tupu, kwa nini hamkai huko Mikoani mbona mnatutambia kuna kuna Hali ya Hewa nzuri, sasa ni nini kinawaleta Dar?
 
Nafikiri wakati umefika sasa kwa Serikali ianze kuzuia watu kutoka Mikoani kuja Dar, tumetosha sasa! ikiwezekana Waruhusiwe wale tu ambao wamepata kazi au walioitwa kwenye usahili... Hali inatisha sana ukienda Ubungo Mabasi yanakuja yamejaa na yanaondoka tupu, kwa nini hamkai huko Mikoani mbona mnatutambia kuna kuna Hali ya Hewa nzuri, sasa ni nini kinawaleta Dar?

Wewe na hiyo Dar yako unalalamika hivyo je wenzetu wa New York ambapo biashara ya kimataifa inafanyikia pale nao wasemeje?
 
Wewe uko wapi na kwa nn upo hapo ulipo. Wewe unafanya nn ambacho yule hawwezi kufanya? Unaposema mikoani kwani dar sio mkoa?
 
Naunga mkono hoja tena kwa nguvu zote,tena hii imechelewa sana na ngoja kidogo nitashuka na sababu na data juu!
 
Ngoja bandari ya bagamoyo ianze na pale Tanga ndo hutawaona. Hujui hao unaowasema ndo wajengaji wa hiyo dar?
 
Dar esalam. Ikulu ikienda dodoma na balalozi zote unafikiri utaiona hyo dar ni tamu tna nenda mwanza uone mji unavyokuja juu
 
Mkuu hayo yalikuwa enzi hizo ya chama kimoja kilichoshika hatamu.. Nchi wakati huo ilikuwa ni ya wakulima na wafanyakazi.. Kama hufanyi kazi basi ulitakiwa kulima.. Na bahati nzuri wakati huo vijijini hakukuwa na shida ya ardhi maana wanavijiji walikuwa wanagaiwa maeneo makubwa tu ya kulima.. So hawakuwa na sababu ya kukimbia vijiji vyao na kuja kuuza maji na njugu mjini.. Siku hizi huko vijijini ardhi zimeshaporwa unategemea hao vijana watafanya shughuli gani kama sio kukimbilia mijini..
 
Wewe uliyekaa Dar miaka nenda rudi ndio uende huko mikoani...
 
Nafikiri wakati umefika sasa kwa Serikali ianze kuzuia watu kutoka Mikoani kuja Dar, tumetosha sasa! ikiwezekana Waruhusiwe wale tu ambao wamepata kazi au walioitwa kwenye usahili... Hali inatisha sana ukienda Ubungo Mabasi yanakuja yamejaa na yanaondoka tupu, kwa nini hamkai huko Mikoani mbona mnatutambia kuna kuna Hali ya Hewa nzuri, sasa ni nini kinawaleta Dar?

Wewe ndio urudi huko unakokuita mikoani!
 
Nafikiri wakati umefika sasa kwa Serikali ianze kuzuia watu kutoka Mikoani kuja Dar, tumetosha sasa! ikiwezekana Waruhusiwe wale tu ambao wamepata kazi au walioitwa kwenye usahili... Hali inatisha sana ukienda Ubungo Mabasi yanakuja yamejaa na yanaondoka tupu, kwa nini hamkai huko Mikoani mbona mnatutambia kuna kuna Hali ya Hewa nzuri, sasa ni nini kinawaleta Dar?
Intarahamwe lingine hili
 
Hii sijui ni Xenophobia??? Hata sijui imekaaje!!
 
Ha ha ha ha, umenichekesha sana. Mie bado ni vere quaternary hapa Dar.
 
Nafikiri wakati umefika sasa kwa Serikali ianze kuzuia watu kutoka Mikoani kuja Dar, tumetosha sasa! ikiwezekana Waruhusiwe wale tu ambao wamepata kazi au walioitwa kwenye usahili... Hali inatisha sana ukienda Ubungo Mabasi yanakuja yamejaa na yanaondoka tupu, kwa nini hamkai huko Mikoani mbona mnatutambia kuna kuna Hali ya Hewa nzuri, sasa ni nini kinawaleta Dar?
Mjini hafukuzwi mtu tutabanana hapa hapa
 
Nafikiri wakati umefika sasa kwa Serikali ianze kuzuia watu kutoka Mikoani kuja Dar, tumetosha sasa! ikiwezekana Waruhusiwe wale tu ambao wamepata kazi au walioitwa kwenye usahili... Hali inatisha sana ukienda Ubungo Mabasi yanakuja yamejaa na yanaondoka tupu, kwa nini hamkai huko Mikoani mbona mnatutambia kuna kuna Hali ya Hewa nzuri, sasa ni nini kinawaleta Dar?

Ukiisoma katiba ya Tanzania kuna guaranteed freedom of movement kwa Watanzania.

Huwezi kukataza watu kuja Dar, Tanzania hatuna udikteta kama China.

Anzisheni mashamba makubwa nje ya Dar muwape watu kazi, watakuwa wapo karibu na Dar na pia wana kazi.

Vinginevyo wapelekeeni huduma muhimu huko vijijini.

Sio mnawanyima huduma muhimu vijijijini, wakizifuata mjini mnawasimanga.

Kama wenyewe ambao Dar ni kwetu kabla Azania Front haijajengwa tungetaka kuendekeza kukataza watu kuja Dar Nyerere asingejua kuvaa suruali.

Watu tuna pedigree Dar kabla Misheni kota haijajengwa, tangu Wanyamwezi hawajaenda kulima viazi kinyasini, tangu kabla Shomvi hajatupa Mzizima.

Na huwezi kusikia tunakataza watu kuja mjini, sanasana tutatafuta viunga vingine tu.
 
......Achaneni na Mourinho...sikiliza kisa hiki
cha kusisimua kilitokea Keko miaka ya
nyuma....Timu ya Ubatani na Bogota zilicheza
mechi ya robo fainali kugombea seti ya
TV....mechi ikaenda katika hatua ya matuta
lakini giza likaingia mechi ikalala. wachezaji wa
Ubatani wakawa wameingiwa na uoga kurudiana
penalti kesho yake asubuhi. Jamaa mmoja
anaitwa Jabir Rumba anachezea ubatani akaona
wenzake wajinga. asubuhi peke yake akachukua
jezi ya kipa na mpira akaenda uwanjani
akakutana jamaa wa Bogota wote wapo uwanjani
na refa. akawaambia anawakilisha timu yake
penalti zipigwe. yeye mwenyewe akawa kipa
akapangua penalti tatu, na akapiga zote za timu
yake akatupia nne. Mida ya saa nne asubuhi
anarudi mtaani..wenzake wanashangaa
kachafuka.. akawaambia 'Tumepita tunacheza
nusu fainali'.....Jamaa nimemuingiza katika
orodha ya mashujaa wangu wa SOKA!!! tehe tehe
tehe
 
Nafikiri wakati umefika sasa kwa Serikali ianze kuzuia watu kutoka Mikoani kuja Dar, tumetosha sasa! ikiwezekana Waruhusiwe wale tu ambao wamepata kazi au walioitwa kwenye usahili... Hali inatisha sana ukienda Ubungo Mabasi yanakuja yamejaa na yanaondoka tupu, kwa nini hamkai huko Mikoani mbona mnatutambia kuna kuna Hali ya Hewa nzuri, sasa ni nini kinawaleta Dar?


nasubiri merck sadiki na kova waisome maana ndio sehemu ya safisha jiji!! maana sasa hivi ukiendesha pikipiki town unaulizwa kitambulisho unafanya kazi wapi kweli bongo nyoso!
 
Taratiiiiibu ubaguzi unaanza, nashangaa hata hawa walioko uamishoni wanasema dar ni yao, nyie ni wazaramo? ngoja nimuone K - vant yeyote kaja mbeya kuchukua mchele na viazi
 
Back
Top Bottom