Serikali iwamulike hawa manabii

Serikali iwamulike hawa manabii

ibanezafrica

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,261
Reaction score
6,556
Napata shida kuona hawa manabii wa sasa wakiwa na maisha ya juu sana wakati kundi la wafuasi ambao ni kubwa wengi wao wakiwa masikini wakutupa.

Sijafika katika mikutano yao ingawa mimi ni mkristo lakini through televisheni naweza kuona moja kwa moja aina fulani ya kujikusanyia pesa kwa njia rahisi sijaelewa kama ni mimi tu naeona haya au vipi?

Mungu amlaze pema mchungaji Moses Kulola ambae ni mfano tu wa mtumishi ambae nilihudhuria mikutano yake mingi tangu nikiwa mdogo kule Tabora.

Sikuwahi kuhisi kama anaenda ki biashara! Leo hoi tunashuhudia nadii akikodi tv station na anajielezea yeye binafsi,anajisifu yaani tofaiti na wale manabii wa mwanzo!

Nabii anatoa namba za m pesa na tigo esa airyel money...jamani wapi tunaelekea na analindwa na mabaunsa wa nne wanazunguka gari yake ya kifahari!

Mbona imeandikwa usimtegemee binadamu kama kinga yako?mbona yesu na hao manabii hawakua na magari wala walinzi?mbona wao hawakuomba wapewe pesa?

Zaidi angeweza fanya miujiza upatikane msaada na yeye kuwapa/kusaidia kusanyiko na si kusanyiko limsaidie yeye!

Jamani wapi tuendako?
 
Pole.Una mawazo mazuri lkn huwezi kuwarekebisha.Wako hivyo.Watazidi kuwanyonya "kondoo".Lakini kwa kuwa wanaishi kama mafarisayo Andiko la Mathayo 7:21-23 linawahusu.
 
Acha kuchafua deals za watu wewe, kila mbuzi ula kwa urefu wa kamba yake mjini hapa.
 
Mkristo gani asiyejua kwamba neno MUNGU huanza na kepito leta. wewe ni wale wale wa AS au saw.

wakipata utajiri wewe tatizo lako ni nini ? na wewe anza unabii kama umaskini umekuchosha tukuone.
au anza msikiti wa kilokole kwa waislamu upige hela. waambie wewe ni mjukuu wa mtume kwa yule mke wake mwenye umri mdogo.
 
Mkristo gani asiyejua kwamba neno MUNGU huanza na kepito leta. wewe ni wale wale wa AS au saw.

wakipata utajiri wewe tatizo lako ni nini ? na wewe anza unabii kama umaskini umekuchosha tukuone.
au anza msikiti wa kilokole kwa waislamu upige hela. waambie wewe ni mjukuu wa mtume kwa yule mke wake mwenye umri mdogo.

Mbona hajawataja akina Shehe Yahaya au anawaamini zaidi kuliko wakina Lusekelo aweke na ushahidi wautjiri sio kulete majungu
 
kondoo-mbwamwitu.jpg

...nabii mkuu ...!
 
Brother mjini mipango huoni masanja kawa mchungaji na anapata wafuasi si tushawazoea na inabidi iwe ivyo ili andiko lipate kutimia "wengi watakuja kwa jina langu wakisema mimi ni kristo nao watadanganya wengi"
 
Aliyepewa kibali na Mungu daima huwa juu, ukiona yupo chini basi hana kibali. Mungu hamwachi mja wake afe masikini.
 
Neno la Mungu lazima litimie, kila kitu kiko wazi kwenye biblia
 
Heri mie sijasema. Lakini ni kweli kuwa falsafa ya unabii inaakisi au kumfanya mchungaji au hao manabii kuwa matajiri? Na ni kwanini kwa nyakati hizi?
Mlio refer biblia ni wapi pameandikwa manabii wapewe pesa na utajiri? Kwangu mimi hao ni wapigaji tu kama walivyo wanyang'anyi wengine.
 
Serikali sikivu haina muda wa kumulika matajiri hata uibe bilioni moja nukta sita au uwe na vijisenti nje ya nchi. Ila utamulukwa kama wewe ni kada wa CHADEMA hata kama ni mjumbe utamulikwa kwa tochi ya betri tatu.
 
Acha mtapeliwe si mnasali ktk makanisa ya wanadamu baala ya kanisa alililoacha Yesu ambalo ni Catholics! badala yake mnatapeliwa kule 'mlima wa baridi', 'kanisa la kufukua', 'kanisa la efwatwa' kwa 'mzee wa upwakwa' 'kanisa la kikobe' nk
 
Maisha yanabadilika.
Baba yetu Ibrahim alikua tajiri sana, Mfalme Suleimani pia hata Mtume Paulo.
Kristo wa jana na leo habadiliki.
 
Kazi ipo mkuu na hawa manabii wetu.

Ingawa wame ni ban humu ila najaribu kutoa mchango sijui kama uta be submitted?

Manabii, wachungani, mitume na wanaofanana na hao wa uongo ni wengi sana tu. Kumtambua kuwa ni wa Mungu au wa shetani utaweza tu kwa kutumia ROHO MTAKATIFU WA MUNGU. Wengine hutambulika kwa maneno, fikra na matendo yao.

Ni matajiri sana kimwili kuliko kiroho. Wanajitukuza au wanatukuzwa sana kuliko Mungu aliye Mkuu. Utamuuliza mtu anatoka wapi? atakuambia kanisa la ....... (naogopa kutaja majina ya watu sababu labda watani ban tena hawa moderators wa humu). Wadanganyika wengi ni wanawake, ingawa pia wanaume wapo wengi tu. We ukiwa na kipato kikubwa hata kama hujui Bible ikoje utaweza kuteuliwa kuwa mzee wa kanisa. Wanajiita wao ni ma transformer, wazee wa upako. Ukiudhuria kwao utaponywa, utapata pesa, utapata watoto, mume na mengine meengi ya kimwili au ya kiduania. Ila ya kiroho kuhusu upendo wa ki Mungu na binadamu wenzako, kiacha dhambi na kutenda mema hawasisitizi hayo.

Haya sasa Moderator ni ban tena.
 
Back
Top Bottom