Serikali itabakia Dodoma?

Serikali itabakia Dodoma?

....

Ila nafikiri kwa Project zenye manufaa kwa taifa hasa hizi mbili SGR na Bwawa la Umeme basi tuzimalizie tu - zingine zisizo na tija tuachane nazo - ile midege mikubwa iliyopaki tunaweza kuiazimisha kwenye airline nyingine.. nk
... umenikumbusha habari ya midege; sijui itaendelea kuwa na ile chapa maarufu ya HAPA KAZI TU?
 
Dodoma ni halinacha. Taifa huanzia kwenye kiini cha familia mojamoja imara Dodoma ilivuruga familia kwa kiasi cha kutosha na ilinifanya nikaripiwe. Achilia mbali utapanyaji wa raslimali za nchi.
 
Kwanza kabisa kama mtanzania niungane na watanzania wenzangu katika kuombeleza msiba huu mzito uliolikumba taifa letu.

Tumeona na kushuhudia juhudi za mwendazake Rais John Pombe Magufuli kuifanya Dodoma kua Makao makuu ya serikali, mengi yamefanywa kuanzia miundo mbinu, kuhamishwa taasisi nyeti za serikali pamoja na rais na viongozi wakuu wa serikali kuhamia Dodoma.

Jee baada ya kifo chake ari na kasi ya kuifanya Dodoma kua mji wa Serikali na makao makuu itaendelea?
YEYE HAYUPO LAZMA TUFATE ALICHOTAKA YEYE
 
Hivi kuna nchi ya maana ambayo ilikua ishahamishia ubalozi wake Dodoma?
wote walipewa vijanja wajenge.... nafikiri waliokwisha kuchimba msingi ni wa ushelisheli, comoro na malawi - ha ha ha
 
Kwanza kabisa kama mtanzania niungane na watanzania wenzangu katika kuombeleza msiba huu mzito uliolikumba taifa letu.

Tumeona na kushuhudia juhudi za mwendazake Rais John Pombe Magufuli kuifanya Dodoma kua Makao makuu ya serikali, mengi yamefanywa kuanzia miundo mbinu, kuhamishwa taasisi nyeti za serikali pamoja na rais na viongozi wakuu wa serikali kuhamia Dodoma.

Jee baada ya kifo chake ari na kasi ya kuifanya Dodoma kua mji wa Serikali na makao makuu itaendelea?
Athubutu imeisha hiyooooo!!
 
Pamoja na yote yashapita tusamehee tumuombe dua njema Mungu ampokee.
Tumjengee mnara wa kumbukumbu.Tutazame mema yake
 
Hayakuwa maamuzi sahihi ya kupeleka watu kule Dodoma ndoa zimevunjika watu wamekufa kwa presha kisa mtu anataka sifa tu eti kafanya kitu ambacho Baba wa Taifa alishindwa matokeo yake anawapeleka watu kule yeye anakimbilia kutibiwa Dar, tulikosea sana watanzania
Pole sana, Samia huenda akafanya usiyoyapenda zaidi.
Dodoma ni CC na Ikulu itakuwa Dodoma.

Kuhusu kupatiwa matibabu Dar ni ukosefu wako wa maarifa tu mimi sijawahi kumpenda wala kumuunga mkono Magufuli ila wakati mwingine ujinga tuweke pembeni.

Dodoma kuna hospital moja tu yenye uwezo ambao unaweza ukawa unafanana kwa kiasi fulani na Muhimbili nayo ni BMH what about Mzena unaijua au unaisikia?
 
walionunua maviwanja makubwa makubwa matumbo moto - inategemea sasa na hisani ya mama yetu na washauri wake, vinginevyo wazanaki tunaita "mali ganyanja"
 
itategemea na utashi wa Mama yetu na wasaidizi wake wa karibu - hata kama ni kurudi Dar basi itakuwa kwa style ya kimya kimya - si lazima hadi utangaziwe !!

Ila nafikiri kwa Project zenye manufaa kwa taifa hasa hizi mbili SGR na Bwawa la Umeme basi tuzimalizie tu - zingine zisizo na tija tuachane nazo - ile midege mikubwa iliyopaki tunaweza kuiazimisha kwenye airline nyingine.. nk
Mi naona SGR iishie Dodoma..tuendelee na mambo mengine , kulishana michicha kisa SGR mi hapana kabisa
 
iPamoja na yote yashapita tusamehee tumuombe dua njema Mungu ampokee.
Tumjengee mnara wa kumbukumbu.Tutazame mema yakeu
cha msingi umekisema kweli kwamba TUSAMEHE - ni kweli wengi wameumia mno ila kusamehe ni moja na nguzo katika dini zetu - tumekwishalifanya hilo, ila masuala ya kupokelewa huko mbinguni sisi hatuna mamlaka nalo ni Mungu baba Mwenyezi ndiyo atashughulika nalo.

Ila haya ma project mengine yasiyokuwa na tija kwa taifa - tusameheane.
 
itategemea na utashi wa Mama yetu na wasaidizi wake wa karibu - hata kama ni kurudi Dar basi itakuwa kwa style ya kimya kimya - si lazima hadi utangaziwe !!

Ila nafikiri kwa Project zenye manufaa kwa taifa hasa hizi mbili SGR na Bwawa la Umeme basi tuzimalizie tu - zingine zisizo na tija tuachane nazo - ile midege mikubwa iliyopaki tunaweza kuiazimisha kwenye airline nyingine.. nk
Duh, ww ni kiazi kweli, imagine ndio uwe Rais
 
Mawazo yako ni sahihi , Dar ilikuwa imeshajitosheleza kufanya reallocation ya funds kumeleta matatizo mengi Sana , na Kwa urahisi wa mawasiliano uliopo kulikuwa hamna haja tena , just to open zones .... Kiufupi Maghufuli alikuwa na mawazo ya kijima Sana
Ikulu ya dodoma igeuzwe chuo kikuu cha ufundi afrika mashariki itoe elimu kuanzia veta Hadi PhD.Ikulu mbili ni gharama ibakie ya dar tu.
Uwanja wa ndege wa Chato wapewe jeshi Ili isipotee.Uitwe Magufuli airwing.
 
Duh, ww ni kiazi kweli, imagine ndio uwe Rais
kwa hiyo unataka tuendelee kujenga hospitali ya Rufaa Chato?, tuendelee kujenga chuo kikuu chato? hiyo ndiyo busara ya kwako? tuendelee kuruhusu midege iendelee kupaki viwanja vya ndege tu kwa hasara kubwa - hivi wewe unajua gharama ya dream-liner moja kupaki kwa siku ?
 
Mawazo yako ni sahihi , Dar ilikuwa imeshajitosheleza kufanya reallocation ya funds kumeleta matatizo mengi Sana , na Kwa urahisi wa mawasiliano uliopo kulikuwa hamna haja tena , just to open zones .... Kiufupi Maghufuli alikuwa na mawazo ya kijima Sana
Ishu ya dodoma ni outdated kwa ulimwengu wa kisasa,labda tu kama ilitumika kutakasishia Kodi zetu na kuukimbia mzimu wa ben 8 dar.Lkn Si mantiki kiuchumi.Pia aliitelekeza akaanza kuijenga Chato huku akiiwaza Karagwe pia.Pesa zetu nyingi Sana zimepotea kusipotija.
 
Kwanza kabisa kama mtanzania niungane na watanzania wenzangu katika kuombeleza msiba huu mzito uliolikumba taifa letu.

Tumeona na kushuhudia juhudi za mwendazake Rais John Pombe Magufuli kuifanya Dodoma kua Makao makuu ya serikali, mengi yamefanywa kuanzia miundo mbinu, kuhamishwa taasisi nyeti za serikali pamoja na rais na viongozi wakuu wa serikali kuhamia Dodoma.

Jee baada ya kifo chake ari na kasi ya kuifanya Dodoma kua mji wa Serikali na makao makuu itaendelea?
Kwani amekufa na Serikali yote?.Si wamebaki watakaoendeleza mipango yake?!!.
 
Hayakuwa maamuzi sahihi ya kupeleka watu kule Dodoma ndoa zimevunjika watu wamekufa kwa presha kisa mtu anataka sifa tu eti kafanya kitu ambacho Baba wa Taifa alishindwa matokeo yake anawapeleka watu kule yeye anakimbilia kutibiwa Dar, tulikosea sana watanzania
Hakukosea Mkuu hiyo mipango ilikuwepo tangu enzi za Nyerere.
 
kwa hiyo unataka tuendelee kujenga hospitali ya Rufaa Chato?, tuendelee kujenga chuo kikuu chato? hiyo ndiyo busara ya kwako? tuendelee kuruhusu midege iendelee kupaki viwanja vya ndege tu kwa hasara kubwa - hivi wewe unajua gharama ya dream-liner moja kupaki kwa siku ?
Wewe unajua gharama zake, au hazina wamekwambia hizo gharama hawazimudu.
Alafu uko chato, hawakidhi vigezo kupata hizo huduma au wanaishi nyumbu kule
 
Back
Top Bottom