akajasembamba
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 1,004
- 1,471
Miaka ya mwanzo ilikuwa utaratibu wa lazima kwamba mume ambaye ni mtumishi wa Serikali anapohama basi lazima mkewe kama naye ni mtumishi anapoomba kumfuata huko alikohamia lazima apewe naye transfer kumfuata, lakini kwa sasa utaratibu huo umekufa kabisa. Spouse anapoomba kumfuata mwenza wake hujibiwa hakuna nafasi na atapewa vitisho kwamba achague kazi au mume! Lakini hapo hapo watumishi wengine wenza wao wanapohamishwa na wao wakiomba uhamisho maombi yao hukubaliwa haraka haraka.Uhamisho wa sasa unafanywa kwa kujuana, upendeleo,rushwa(ya pesa na ya ngono) Maana ya NDOA ni kuishi wawili sasa ni NDOA gani ambayo Mume Yupo Mtwara na Mke Kagera! Au serikali yenyewe inaona wenye haki ya kuishi na wenza wao ni vigogo tu ambao wake zao hutafutiwa nafasi popote pale waume au wake zao vigogo wanapohamia lakini watumishi wa chini huambiwa hakuna nafasi na hukaa miaka tele mbali na wenza wao. Kuna matukio ya wakubwa kuwahamisha waume vituo ili wapate nafasi za kujivinjari na wake wa watumishi hao. Serikali inajua kuajiri tu watumishi bila kujali hao watumishi nao walizaliwa na wanahitaji malezi ya wazazi wawili! Mtu anapokaa mbali na mwenza wake obviously ataelemewa na vishawishi ambavyo kama angekuwa na mwenzake angeweza kuvihimili, katika zama hizi za ukimwi tuzidi kuona siyo kuvunjika ndoa tu ila vifo zaidi!