Serikali ina mpango gani kwa barabara ya Morogoro kuanzia Kimara mwisho mpaka Mbezi mwisho?

Omukitwe

Member
Mar 29, 2016
91
91
Najiuliza hata sipati jibu. Ni nani aliplan barabara ya mwendo kasi iishie kimara mwisho na si mbezi mwisho? Hapo ndo nakosa jibu kabisa. Hii barabara ya morogoro ni barabara pekee inayopeleka magari mengi sana ikiwemo mabasi, maroli, na magari ya watu binafsi yanayoenda na kutoka mikoani na nchi jirani. Lakini ebu fuatilia shida iliyopo kuanzia kimara mwisho mpaka mbezi mwisho. Mtu unaweza kutumia zaidi ya saa moja kutoka mbezi kwenda kimara. Hapa najiuliza, hivi serikali haioni umuhimu wa kupanua hii barabara angalau kuwa njia nne?? Ninaomba kuuliza kama kuna yeyoye ana taarifa za kuwekwa kwenye mpango wowote wa serikali kwa kuondoa hii kero anajuze.
 
Najiuliza hata sipati jibu. Ni nani aliplan barabara ya mwendo kasi iishie kimara mwisho na si mbezi mwisho? Hapo ndo nakosa jibu kabisa. Hii barabara ya morogoro ni barabara pekee inayopeleka magari mengi sana ikiwemo mabasi, maroli, na magari ya watu binafsi yanayoenda na kutoka mikoani na nchi jirani. Lakini ebu fuatilia shida iliyopo kuanzia kimara mwisho mpaka mbezi mwisho. Mtu unaweza kutumia zaidi ya saa moja kutoka mbezi kwenda kimara. Hapa najiuliza, hivi serikali haioni umuhimu wa kupanua hii barabara angalau kuwa njia nne?? Ninaomba kuuliza kama kuna yeyoye ana taarifa za kuwekwa kwenye mpango wowote wa serikali kwa kuondoa hii kero anajuze.


Hiyo sehemu ndiyo utumbo mwembamba wa jiji mwanangu
 
mkuu mimi nimetoka mbezi na lisaa ndiyo kwanza nipo apa kwa msuguri yaani mpaka niione pale suka si saa 3 ?
 
Unaweza kutumia hata masaa matatu kutoka Kimara hadi mbezi na mimi hiyo imewahi kunitokea tena weekend iliyopita baada ya gari kuungua pale maeneo ya stop over. Hata mimi nashangaaga sana aliyeplan lanes za mwendokasi ziishie kimara sijui alipiga mahesabu gani akajiona yuko sahihi yaan badala ya jam kupungua ndio kama imeongezeka.

Kuna njia zingine kama babara ya morroco hapakuwepo na haja kubwa ya kupeleka mwendokasi sababu hakuna magari mengi, mji una miundo mbinu mibovu huu.
 
mkuu mimi nimetoka mbezi na lisaa ndiyo kwanza nipo apa kwa msuguri yaani mpaka niione pale suka si saa 3 ?

Ndo mimi nataka nitoke huku mbezi,kama bado kuna foleni inanilazimu kuendelea kusubiria mpaka badae tena!foleni huku mbezi ni janga kubwa sana
 
Tatizo sio kuipanua hiyo barabara

Ila zingetengenezwe barabara za michepuko mfano hapo mbezi kuna michepuko ya goba hadi kawe pia kuna ya kinyerezi ambazo zingepunguza magari mengi kuelekea moro road.
Mkuu hizo barabara ndoo zinajengwa sasa
 
Barabara hapo zitanuliwe mpk kibaha sio Mbezi tu, mji unakua miundo mbinu lazima iendelezwe
 
Najiuliza hata sipati jibu. Ni nani aliplan barabara ya mwendo kasi iishie kimara mwisho na si mbezi mwisho? Hapo ndo nakosa jibu kabisa. Hii barabara ya morogoro ni barabara pekee inayopeleka magari mengi sana ikiwemo mabasi, maroli, na magari ya watu binafsi yanayoenda na kutoka mikoani na nchi jirani. Lakini ebu fuatilia shida iliyopo kuanzia kimara mwisho mpaka mbezi mwisho. Mtu unaweza kutumia zaidi ya saa moja kutoka mbezi kwenda kimara. Hapa najiuliza, hivi serikali haioni umuhimu wa kupanua hii barabara angalau kuwa njia nne?? Ninaomba kuuliza kama kuna yeyoye ana taarifa za kuwekwa kwenye mpango wowote wa serikali kwa kuondoa hii kero anajuze.
Mkuu ni kweli tunapata shida sana maana hiyo ndoo barabara inayotumika na karibia asilimia 80 ya watu wa mikoani waliohamia Dar, iwe unakaa mbezi kimbamba, kibaha lazima uitumie hii barabara

Na hao wanaokaa masaki, Osterbay, mikocheni lazima waitumie hiyo barabara maana lazima waende makwao huko mikoani.

Nadhani iko kwenye mpango wa kuitanua mwaka wa fedha 2020 , ila wanampango wa kuhamisha stendi ya ubungo hio ndoo itapunguza foleni kidogo maana mabus mengi yataishia mbezi na maofisi, ma garage na mayard yao yatahamia mbezi huko huko hapo foleni itapungua kwa asimia kubwa.
 
Mbona plan yake tayari, inajengwa njia sita hadi Chalinze, inaanza April mwakani kama sikosea, jitahidi uwe una soma soma, hii ishu ilianza tangu Magu akiwa waziri four years back
 
Mbona plan yake tayari, inajengwa njia sita hadi Chalinze, inaanza April mwakani kama sikosea, jitahidi uwe una soma soma, hii ishu ilianza tangu Magu akiwa waziri four years back
Mbona plan yake tayari, inajengwa njia sita hadi Chalinze, inaanza April mwakani kama sikosea, jitahidi uwe una soma soma, hii ishu ilianza tangu Magu akiwa waziri four years back
Mkuu wewe unayosema ni ile inayopita mbagala. Wala haitokei ubungo kupitia mbezi. Kwa hiyo, hiyo barabara nahisi serikali haina mpango nayo kabisa.
 
Mkuu wewe unayosema ni ile inayopita mbagala. Wala haitokei ubungo kupitia mbezi. Kwa hiyo, hiyo barabara nahisi serikali haina mpango nayo kabisa.

Si kweli, hiyo ya Morogoro Road njia sita hadi Chalinze
 
Si kweli, hiyo ya Morogoro Road njia sita hadi Chalinze
Ni wapi huo mpango umewekwa mkuu?? Kwa maana bajeti zote zilizopita na ya sasa hwaongelei hii barabara wanaongelea barabara itakayoanzia chamazi kule mbagala mpaka moro kupitia kibamba, mlandizi, chalinze hadi moro. Naomba kama unao ushahidi yalipoandikwa hayo ya njia sita kutoka mpaka chalinze kupitia kimara, mbezi mpaka chalinze uniwekee hapa. Mkuu wa mkoa alitamka juu ya kuhamishia stand ya mabasi mbezi mwisho na akatoa siku kumi na nne lkn hakuna kitu. Nahisi mpaka sasa siku 14 hazijafika. Ndo maana nasema hakuna mpango wa makusudi wa kuondoa hii kero ya foleni kimara mpaka mbezi.
 
Ni wapi huo mpango umewekwa mkuu?? Kwa maana bajeti zote zilizopita na ya sasa hwaongelei hii barabara wanaongelea barabara itakayoanzia chamazi kule mbagala mpaka moro kupitia kibamba, mlandizi, chalinze hadi moro. Naomba kama unao ushahidi yalipoandikwa hayo ya njia sita kutoka mpaka chalinze kupitia kimara, mbezi mpaka chalinze uniwekee hapa. Mkuu wa mkoa alitamka juu ya kuhamishia stand ya mabasi mbezi mwisho na akatoa siku kumi na nne lkn hakuna kitu. Nahisi mpaka sasa siku 14 hazijafika. Ndo maana nasema hakuna mpango wa makusudi wa kuondoa hii kero ya foleni kimara mpaka mbezi.
Hebu jaribu kutafuta taarifa kidogo.iyo barabara ipo kwny mpango na bajeti yake ishapita
 
Hebu jaribu kutafuta taarifa kidogo.iyo barabara ipo kwny mpango na bajeti yake ishapita
Mkuu nimefuatilia hadi kwenye bageti ya 2016/2017 inasema kuwa watakarabati madaraja ya kibamba, kiluvya na mpigi na kupanua sehemu za miinuko tu kwa barabara ya kutoka kimara mpaka kibaha 25.7km. (Ukurasa wa 33 wa hotuba ya waziri wa ujenzi, mawasiliano na uchukuzi ya bageti ya 2016/2017) Hakuna mpango wa kuiongeza ukubwa kuwa njia hata nne.
 
Back
Top Bottom