Serikali imeishiwa haina pesa za mishahara

Hili nalo litapita, sijui tumlaumu JK ama wale waliomtangulia kwa kufisadi fedha za watz
 
Hapana Mkuu, halitapita isipokuwa tutalipitisha

Nakuunga mkono 100% kwamba tutalipitisha. Inasikitisha jinsi watanzania tusivyokuwa na ari ya kupigania maslahi yetu. Kusema kweli sijui mpaka kitokee nini ndio watanzania tuone kuna haja ya kupambana na kupigania haki yetu ya msingi ya kuwa na mazingira mazuri ya watu kujiendeleza.
 
Katika Hali iliyokuwa inatarajiwa kabisa, serikali ya Mheshimiwa Kikwete haina pesa kwa sasa za kulipa mishahara ya wafanyakazi wake na kutoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu. Kwa habari za uhakika wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe wameandikiwa barua kuambiwa hakuna mishahara mpaka pale serikali itakapotuma pesa. Mwanzoni tuliambiwa hapa JF kulikuwa na uwezekano wa kuwalipa tarehe 5/9.2008 lakini sasa ni mpaka serikali itakapotuma pesa.

Kama hilo halitoshi vyuo vyote vya serikali ambavyo vilikuwa vifunguliwe mwishoni mwa mwezi wa 8 hafitafunguliwa mpaka tarehe 29/9/2008. Tayari wanafunzi wote wameshataarifiwa kuhusu kuahirishwa huku. Hii ni kutokana na bodi ya mikopo kutopatiwa fungu lake la mikopo mpaka sasa hivi.



Hivi hili la kusema pesa zote za EPA (karibia billioni 200) ziingizwe serikalini sio katika kujaribu kuficha kwamba serikali haina pesa kwa sasa?

Kama ni kweli huu utakuwa ni ushahidi mkubwa kuwa Serikali ya Kikwete imeshindwa! Nasema ni ushahidi mkubwa kwasababu ushahidi mwingine haujawafikia baadhi ya Watanzania hasa vijijini na wale wanazi wa CCM. lakini katika hili watakubali tu, walimu na wauguzi wapo hadi vijijini. Hata wale wavumilivu sana wataguswa sasa na kukataa kuendelea kuvumilia.

Eti wafanyakazi wakakosa mishahara, wanafunzi wakakosa kwenda vyuoni eti tatizo hakuna fedha! wakati huo huo safari za viongozi zinashamiri, mafisadi wa EPA, Richmond, CIS nk wakitesa mitaani, ndege ya Rais ikiendelea kufanyiwa matengenezo US kila baada ya miezi mitatu. Lazima uwe ni mwisho wa utawala usiowajali wafanyakazi na wanafunzi. TUCTA watatusaidia kuanzisha vuguvugu la kudai 'nguvu ya umma' ishike hatamu.
 
ZIPO dalili kuwa serikali imefilisika. Au labda mapato hatyaingii kama ilivyotarajiwa au kuna matundu makubwa ambayo yanaruhusu kuvuja kwa hazina ya serikali wakati serikali yenyewe haina habari.

Kwa lugha nyingine inawezekana kuwa wahasibu wa Tanzania wamekuwa na akili kuliko wanasiasa mara kadhaa. Hili kwa kawaida hutokea kwenye makampuni mengi ambayo wakubwa huandika kijikaratasi tu kwamba mlipe fulani milioni 5 na wahasibu wakawa wanaongeza 1 mbele kwa hiyo akalipwa na cashier milioni 15. Kumi zake na tano za baamkubwa!

Muda si muda wafilisi hutua mlangoni. Je, ndicho kilichotokea Tanzania? Kwamba wakubwa walikuwa wakindika lipa milioni 50 na mhasibu anaongeza 1 mbele inakuwa 150. Milioni mia moja zake na milioni 50 za baamkubwa?

Kama sivyo, kwanini serikali imekwama kwenye kulipa mishahara ya watu wadogo wasio na kitu kidogo??

Na ndugu yangu unayejiuza kwa bei rahisi kwa Marekani na Benki ya Dunia wengi tunakushangaa hivi kweli Tanzania inajua inachokifanya. Miaka 50 baada ya Uhuru Tanzan ia yajipeleka yenyewe kuwa Koloni la Marekani kwa sababu tu watoto wetu wa ndani ya ndoa na nje ya ndoa wanasoma huko?

Mara nyingi nchi inayofanya ukuruba na Marekani basi nchi hiyo kubwa ikipiga chafya ya uchumii wake kudhoofika nchi masikini iliyojiweka kwenye kwapa zake husambaratika au husambaratishwa kwa sababu hii au ile?

Serikali kwa hakika ina kazi kubwa ya kuhakikisha kwamba sio tu inajidhibiti katika matumizi yake bali pia kuwa na mfumo usio na matundu na unaoweza kutumiwa na rais na mawaziri wake wakajua kila shilingi inayoingia na inayotoka.

La sivyo, bado kuna vilio vingi tu vyaja! Uongozi si ziara na matembezi bali ni kuhakikisha utendaji unakwenda kama ilivopangwa na kwamba kuna udhibiti wa kila kitu nchini kwa kiasi ambacho hata mkuu akihamia nje kwa miezi mitatu bado mambo hayataharibika lakini si hivi sasa.

Inavyoelekea kwa hivi sasa kila mkuu akisafiri na magoli kumi yanafungwa. Ilikuwa timu ya mpira ndio kichwa cha mwenda wazimu sasa nchi imegeuka kichwa cha mwendawazimu. Tunafungwa kila kukichwa achilia magoli ya kujifunga wenyewe!!!!

Haiwezekani pia kuwa nchi inayoongozwa bila delegation of authority na decentralization. Ama kwa hakika vitu hiviwili ndivyo vinavyotuadhiri kila kukichwa! Hakuna uongozi wa mtu mmoja ila uongozi wa pamoja. Na kiongozi mzuri ni yule anayefanya kazi zake kupitia kwa watu wengine na sio vinginevyo.

Tusisahau jamani huwezi kujenga nchi bila msingi imara. Nchi haina msingi huo kwa sasa nyumba tunaijenga mchangani kando ya bahari..... sasa machozi ya nini?

Mungu tuepushe na Lucifer wa dunia!!!
 
walifikiriaa kuongoza nchi ni kama kuongoza stori za vijiweni?ndio waone sasa
 
..ni uzembe na ubinafsi tu. nchi imejaa fedha tele hii.

..kwani za magari ya fahari na safari zisizo hesabu zinatoka wapi?
 
NA MIMI nina wasiwasi kama huu. Dalili zote za kufilisika zipo.
Angalia misafara inayokwenda nje. Nadhani kila msafara sio chini ya bilioni ukijumlisha mishahara isiyofanyiwa kazi na marupurupu ya safari. Sio mkuu mwenyewe si mawaziri wake.

Utitiri wa magari ya milioni 200 na ambayo inakunywa dizeli ya kama milioni 200 vilevile kwa mwaka.

Ndege tusiyoimudu kwa gharama zake. Achilia mbali kuingilia biashara kama vile za vyombo vya habari ambavyo sekta binafsi inaweza ikabeba mzigo huu kwa nafuu ya umma.

Tumeachiwa wajanja watunyoe kwa kuuza biashara ya usafishaji na usafirishaji na usambazaji mafuta.

Karatasi tu zinatula mabilioni, yaani, makaratasi na stationery nyingine. Simu za mkononi zinatunywa mabilioni kuliko yale simu hizo zinazolipa kama kodi na usiseme ndugu!


Haya yote yanaumiza watu vichwa. Hivi kweli kwenye serikali kuna watu wangapi wana idea na Book-keeping, Accounting na Auditing au sasa ndio zamu ya wakaguzi na wahasibu wa nje kugeuka kupe tukibebeshwa mzigo usio na sababu na uongozi uliopo?

Rudini shuleni jamani, mnatumaliza!
 
NI-IGE NISI-IGE? Eti msichana mrembo, mwenye siha, mtaratibu, mstahimilivu, mlimbwende uliyechumbiwa miaka 50 na mabepari ukawakataa. Wakati huo Wajamaa kama China, Urusi na wengineo Ulaya Mashariki walikuwa hoi bin taaban.

Ukamkataa yule bepari wakati huo pamoja na ukwasi wake iweje leo miaka 50 imeptia eti anarudi kukuchumbia kwa ahadi hizo hizo za miaka ya 60??

Hakika tuwachovu sio tu wa fikira bali hata wa kuona ukweli uliotuzunguka. Mungu atusaidie!!
 
TUKASOME MENEJIMENTI HATA HAPA HAPA NYUMBANI JAMANI!

MENEJIMENTI NA Utwala ni jambo pana zaidi ya kuitisha vikao na kutoa hotuba hapa na pale.

Uongozi unataka kiongozi asimamie mipango, kupangia watu kazi, oganaizesheni na uratibu wa mambo, udhibiti wa uendeshaji na kuhamasisha watendaji.

Inavyoelekea uongozi wetu una matatizo ya kupangia watu kazi wanazozimudu, oganaizesheni, uratibu na uzingatiaji wa utawala wa kisheria na maadili, udhibiti wa yale yanayofanywa na walio chini ya viongozi pamoja na kukosa mikakati inayoeleweka ya kuhamasisha watendaji.

Niliambiwa na mwalimu wangu wa menejimenti, hayati Prof. Peter Drucker kwamba kiongozi anapaswa kujua MUDA wake unakwenda wapi au unatumika VIPI? Ni nini MCHANGO wake kwa taasisi au nchi anayoongoza; ni nini UBORA na UDHAIFU wa walio chini yake; aweke uaula au kiswahili nisichokipenda KIPAUMBELE na mwisho wa yote asichelewe hata siku moja kufanya MAAMUZI ikiwa ni pamoja na yale ya kusahihisha makosa yake mwenyewe au ya wale walio chini yake.

Mkitaka utamu zaidi wa haya nipeni na mimi haki yangu ndio niendelee:...................


Vinginevyo naendelea kutafakari haya ya Mwalimu Jr. hapa chini:

ZIPO dalili kuwa serikali imefilisika. Au labda mapato hatyaingii kama ilivyotarajiwa au kuna matundu makubwa ambayo yanaruhusu kuvuja kwa hazina ya serikali wakati serikali yenyewe haina habari.

Kwa lugha nyingine inawezekana kuwa wahasibu wa Tanzania wamekuwa na akili kuliko wanasiasa mara kadhaa. Hili kwa kawaida hutokea kwenye makampuni mengi ambayo wakubwa huandika kijikaratasi tu kwamba mlipe fulani milioni 5 na wahasibu wakawa wanaongeza 1 mbele kwa hiyo akalipwa na cashier milioni 15. Kumi zake na tano za baamkubwa!

Muda si muda wafilisi hutua mlangoni. Je, ndicho kilichotokea Tanzania? Kwamba wakubwa walikuwa wakindika lipa milioni 50 na mhasibu anaongeza 1 mbele inakuwa 150. Milioni mia moja zake na milioni 50 za baamkubwa?

Kama sivyo, kwanini serikali imekwama kwenye kulipa mishahara ya watu wadogo wasio na kitu kidogo??

Na ndugu yangu unayejiuza kwa bei rahisi kwa Marekani na Benki ya Dunia wengi tunakushangaa hivi kweli Tanzania inajua inachokifanya. Miaka 50 baada ya Uhuru Tanzan ia yajipeleka yenyewe kuwa Koloni la Marekani kwa sababu tu watoto wetu wa ndani ya ndoa na nje ya ndoa wanasoma huko?

Mara nyingi nchi inayofanya ukuruba na Marekani basi nchi hiyo kubwa ikipiga chafya ya uchumii wake kudhoofika nchi masikini iliyojiweka kwenye kwapa zake husambaratika au husambaratishwa kwa sababu hii au ile?

Serikali kwa hakika ina kazi kubwa ya kuhakikisha kwamba sio tu inajidhibiti katika matumizi yake bali pia kuwa na mfumo usio na matundu na unaoweza kutumiwa na rais na mawaziri wake wakajua kila shilingi inayoingia na inayotoka.

La sivyo, bado kuna vilio vingi tu vyaja! Uongozi si ziara na matembezi bali ni kuhakikisha utendaji unakwenda kama ilivopangwa na kwamba kuna udhibiti wa kila kitu nchini kwa kiasi ambacho hata mkuu akihamia nje kwa miezi mitatu bado mambo hayataharibika lakini si hivi sasa.

Inavyoelekea kwa hivi sasa kila mkuu akisafiri na magoli kumi yanafungwa. Ilikuwa timu ya mpira ndio kichwa cha mwenda wazimu sasa nchi imegeuka kichwa cha mwendawazimu. Tunafungwa kila kukichwa achilia magoli ya kujifunga wenyewe!!!!

Haiwezekani pia kuwa nchi inayoongozwa bila delegation of authority na decentralization. Ama kwa hakika vitu hiviwili ndivyo vinavyotuadhiri kila kukichwa! Hakuna uongozi wa mtu mmoja ila uongozi wa pamoja. Na kiongozi mzuri ni yule anayefanya kazi zake kupitia kwa watu wengine na sio vinginevyo.

Tusisahau jamani huwezi kujenga nchi bila msingi imara. Nchi haina msingi huo kwa sasa nyumba tunaijenga mchangani kando ya bahari..... sasa machozi ya nini?
 
Hii serikali choka mbaya sijapata kuona. Inaonekana kuwa walipokuwa wanakubali kuongeza mishahara walikuwa wanafanya hivyo kwa kujitafutia sifa. Kwa nini lakini wafanye hivyo? Mtu unatakiwa kufanya mambo kwa vipimo, wao wanafanya mambo wka sifa, tutafika kweli?
 
Hii ni moja ya athari ya kubebana kirafiki watu walipo kwenye system bado wanamawazo yale yale ya kale hawajabadilika.......fumua serikali weka wazee kisha changanya na damu changa uone kazi JK.
 
Sio siri wana JF hali si shwari. Mimi ni mtumishi wa Serikali katika Idara ya Uhamiaji. Maisha ni magumu sana hasa hasa kutokana na Serikali kuchelewesha mishahara ya August
 
message from NMB 'Your Salary has been Deposited into your account' jamani mishahara ya August imetoka.
 
Jamani suala la mishahara kwenye secta binapsi wangewaachia waajiri wenyewe waamue. Haiwezekani serikali itoe tamko mwalimu wa shule binafsi alipwe 350,000 wkt wa serikalini analipwa 150,000/=.

Pili house girl akilipwa sh 65,000/= je wewe unayemlipa huyu binti shi 65,000 wewe unalipwa shilling ngapi?????.

Sio Serikali inakurupuka tu kuamua mambo ianze yenyewe kwenye secta zake kupandisha mishahara ndio na secta binafsi zifate.

Kwa mtaji huu ajira nyingi sana zitapungu na lile swala la Mh. Rais kuongeza ajira 1,000,000 jalitawezekana na matokeo yake zitapungua ajira 900,000/=

Watanzania tuwe macho.


Kuwa na house girl ni lazima?
 
Serikali haina hela ilikuwa inasubiri bajeti ipite kwanza, baada ya ku-overspend bajeti iliyopita, yaani jamani hata hizi nazo zinatakiwa kuwa data? Pleasee!


FMES

[*]Kusema Serikali haina hela "baada ya ku-overspend " halafu kusema tena "inasubiri bajeti ipite kwanza" najiuliza hio hela walizotumia ni zipi. Hapa naona serikali imevuka kiwango walichowekewa na Bunge (kama ilivyo kawaida yao) then wanajisafisha kwa kusema wanasubiri Bajeti ipe, wanasubiri nini kama walisha anza kutumia.
 
No,jamani mbona mnatia chumvi sana?Hao wafanyakazi wa serikalini ambao mnasema hawajalipwa ni wepi?Mimi niko serikalini.Mshahara uliochelewa ni wa mwezi uliopita tuu, ambao leo tarehe 01.09.2008 tayari umeshatoka.Naomba tujaribu kuwa na facts, tusipotoshe watu.Ni kweli serikali yetu ina makosa mengi,lakini pale panapokuwa na ukweli tuuseme kama ulivyo.
 
No,jamani mbona mnatia chumvi sana?Hao wafanyakazi wa serikalini ambao mnasema hawajalipwa ni wepi?Mimi niko serikalini.Mshahara uliochelewa ni wa mwezi uliopita tuu, ambao leo tarehe 01.09.2008 tayari umeshatoka.Naomba tujaribu kuwa na facts, tusipotoshe watu.Ni kweli serikali yetu ina makosa mengi,lakini pale panapokuwa na ukweli tuuseme kama ulivyo.

No, siyo chumvi wenzio huku hata salary slip bado, tumeambulia tangazo la kwamba tuwe wavumilivu!
 
No,jamani mbona mnatia chumvi sana?Hao wafanyakazi wa serikalini ambao mnasema hawajalipwa ni wepi?Mimi niko serikalini.Mshahara uliochelewa ni wa mwezi uliopita tuu, ambao leo tarehe 01.09.2008 tayari umeshatoka.Naomba tujaribu kuwa na facts, tusipotoshe watu.Ni kweli serikali yetu ina makosa mengi,lakini pale panapokuwa na ukweli tuuseme kama ulivyo.

Serikalini wapi?
 
Back
Top Bottom