sosoliso
JF-Expert Member
- May 6, 2009
- 8,539
- 9,462
Serikali, kupitia mamlaka ya mawasiliano, imetangaza kuandikishwa kwa watumiaji simu wa mitandao yote hapa Tanzania. Maana yake ni kwamba, kabla ya kumiliki simcard, unatakiwa utambuliwe wewe ni nani, unakaa wapi na shughuli unayoifanya. Then utoe iwe ni kitambulisho, kadi ya kupigia kura, leseni au barua toka kwa mtendaji au mwenyekiti wa serikali za mitaa. Wametoa sababu ya wao kufikia maamuzi hayo. Kwanza wanasema ni kuzuia wizi wa simu, halafu kuzuia matusi, vitisho na manyanyaso yanayofanyika kwa sasa. Maana wanadai ukishasajili, basi itakuwa rahisi kufuatilia namba ya simu yenye utata na kumfahamu mwenyewe.
Upande wa pili, kuna watumiaji ambao hawapendezwi na suala zima la kujisajili ili kuweza kutumia simu. Suala la simu ni suala huru ambalo halihusiani na mtumiaji kuingiliwa haki zake za faragha. Anaweza kutumia simu leo, kesho akabadilisha nk. Kuna baadhi ya watu wako very sensitive na haki zao za faragha. Wana JF, mnasemaje kuhusu hii debate?
Upande wa pili, kuna watumiaji ambao hawapendezwi na suala zima la kujisajili ili kuweza kutumia simu. Suala la simu ni suala huru ambalo halihusiani na mtumiaji kuingiliwa haki zake za faragha. Anaweza kutumia simu leo, kesho akabadilisha nk. Kuna baadhi ya watu wako very sensitive na haki zao za faragha. Wana JF, mnasemaje kuhusu hii debate?