Crucifix
JF-Expert Member
- Feb 20, 2011
- 1,651
- 588
Serikali ilihusika kusababisha ajali ya basi la TAQWA na lori la AZAM
Namsikitikia sana dereva wa lori la Azam na msaidizi wake walivyopotezewa maisha yao kwa uzembe wa dereva wa Taqwa na Tanroads. Nasikitika pia kwa maisha yaliyopotea ya abiria wasio na hatia. Jibu la haraka la mkuu wa polisi na mkuu wa wilaya ya Biharamulo ni kuwa ajali ilisababishwa na uzembe wa madereva. SIO KWELI.
Barabara eneo la Lusahunga ina mashimo mashimo, na mengine ni makubwa kiasi cha kuweza kusababisha ajali endapo dereva atalikwaa bila tahadhari. TANROADS wanafanya ukarabati usioisha wa kufukia mashimo yale. Kwa kujihami ili wasigongwe na magari, vibarua wa TANROADS huweka mawe makubwa barabarani ili magari yapunguze mwendo. Pia huweka kibao chenye maneno, "man at work."
Kilichotokea Lusahunga ni kwamba, mawe makubwa yalipangwa karibu kabisa na mashimo yaliyokuwa yakizibwa na kibao kiliwekwa karibu kabisa na mawe yale. Dereva mzembe wa Taqwa alipuuza kibao kilichokuwa kimeziba mawe yale na pengine angekisukumia pembeni tu na kujiendea zake na mbio kama kawaida. Lakini kutahamaki aliona mzigo wa mawe makubwa mbele tu ya kibao na hivyo akahamia upande wa kulia na kukutana na dereva wa Azam ambaye alikuwa akijitembelea kwenye site yake na kilichofuata wote mnakifahamu.
Ni makosa basi kwa mkuu wa polisi kuhitimisha kwa kusema ajali ilisababishwa na uzembe wa madereva. Alipaswa kusema ajali ilisababishwa na uzembe wa dereva wa Taqwa na wafanyakazi wa Tanroads.
chanzo cha habari : dereva wa lori la mafuta T909 ASU aliyekuwa eneo la tukio akielekea Bujumbura na ambaye yuko tayari kuhojiwa na kuelezea ukweli huo bila woga.
Namsikitikia sana dereva wa lori la Azam na msaidizi wake walivyopotezewa maisha yao kwa uzembe wa dereva wa Taqwa na Tanroads. Nasikitika pia kwa maisha yaliyopotea ya abiria wasio na hatia. Jibu la haraka la mkuu wa polisi na mkuu wa wilaya ya Biharamulo ni kuwa ajali ilisababishwa na uzembe wa madereva. SIO KWELI.
Barabara eneo la Lusahunga ina mashimo mashimo, na mengine ni makubwa kiasi cha kuweza kusababisha ajali endapo dereva atalikwaa bila tahadhari. TANROADS wanafanya ukarabati usioisha wa kufukia mashimo yale. Kwa kujihami ili wasigongwe na magari, vibarua wa TANROADS huweka mawe makubwa barabarani ili magari yapunguze mwendo. Pia huweka kibao chenye maneno, "man at work."
Kilichotokea Lusahunga ni kwamba, mawe makubwa yalipangwa karibu kabisa na mashimo yaliyokuwa yakizibwa na kibao kiliwekwa karibu kabisa na mawe yale. Dereva mzembe wa Taqwa alipuuza kibao kilichokuwa kimeziba mawe yale na pengine angekisukumia pembeni tu na kujiendea zake na mbio kama kawaida. Lakini kutahamaki aliona mzigo wa mawe makubwa mbele tu ya kibao na hivyo akahamia upande wa kulia na kukutana na dereva wa Azam ambaye alikuwa akijitembelea kwenye site yake na kilichofuata wote mnakifahamu.
Ni makosa basi kwa mkuu wa polisi kuhitimisha kwa kusema ajali ilisababishwa na uzembe wa madereva. Alipaswa kusema ajali ilisababishwa na uzembe wa dereva wa Taqwa na wafanyakazi wa Tanroads.
chanzo cha habari : dereva wa lori la mafuta T909 ASU aliyekuwa eneo la tukio akielekea Bujumbura na ambaye yuko tayari kuhojiwa na kuelezea ukweli huo bila woga.