Bukyanagandi
JF-Expert Member
- Jun 24, 2009
- 11,626
- 18,228
Mkuu mbona kama kuna kasi ya kufufua reli ya kati ni ndogo sana, wanakazia barabara tu sijui kwa nini - hivi tungekuwa serious tukazungumza na wachina mbona ukarabati wa reli ya kati ungechukua muda mdogo sana, kwanza ballast zinapatikana locally, sleepers zinaweza kumiminwa huko Mbeya TAZARA kiwanda cha kumimina sleepers kilijengwa siku nyingi na wachina, kitu ambacho kinge agizwa kutoka nje ni reli tu - sasa tatizo liko wapi?? Wakati mwingine nakuwa na feeling kwamba labda wafanya biashara wenye trucks za kubeba mizingo wanataka project hii isi-take off - kusua sua kumezidi ni as if Serikali haijui umuhimu wa usafirishaji kupitia njia ya reli, kama hawawezi basi wawape watu binafsi/wawekezaji.