Serikali iitishe harambee tuimarishe reli ya Dar - Kigoma - Mwanza

Serikali iitishe harambee tuimarishe reli ya Dar - Kigoma - Mwanza

Ntemi Kazwile

JF-Expert Member
Joined
May 14, 2010
Posts
2,182
Reaction score
309
Kufuatia mikakati ya nchi za Kenya, Uganda and Rwanda kuiengua nchi yetu kwenye mipango ya jumuia ya Afrika Mashariki nashauri yafuatayo yafanyike haraka iwezekanayo ili kuliwezesha taifa kuwa na uwezo wa kusafirisha mizigo kwa haraka na kwa gharama kidogo ili kuhakikisha kuwa mizigo ya nchi marafiki kama Burundi na DRC inapitia Dar.
  • Serikali iitishe hambee ya wananchi wote ili kuchangia mfuko utakaowezesha ujenzi wa reli hii kwa haraka, kwa mfano ikiwaomba wananchi wake wachangie angalau 1,000 kila mtu ndani ya mwaka mmjo serikali inaweza kukusanya zaidi ya bil.100, mchango huu uwe wa hiari au
  • Serikali ikaribishe wananchi wake kununua hisa kwenye kampuni ya reli, hisa hizi ziuzwe kwa bei ndogo kabisa ili kuwawezesha watanzania wengi zaidi kushiriki, hamasa iwekwe kwa wananchi wengi zaidi kuchangia ili kuliwezesha taifa kuwa na uwezo wa kushindana kibiashara na mataifa mengine kwa kupunguza gharama za usafirishaji/uzalishaji

Naamini njia hii ni rahisi na ikitekelezwa ipasavyo itawezesha kupatikana pesa nyingi na kwa haraka bila kuliweka taifa rehani.
 
mimi nipo tayari kutoa mara kumi ya hiyo lakini hela zisisimamiwe na maccm.
 
Mkuu wazo lako ni zuri sana

Lakini nadhani kama serikali ikipata muwekezaji wa maana kutoka nje au ndani mwenye uwezo wa kuitengeneza vizuri reli ya kati basi tutafika mbali.
 
Mkuu wazo lako ni zuri sana

Lakini nadhani kama serikali ikipata muwekezaji wa maana kutoka nje au ndani mwenye uwezo wa kuitengeneza vizuri reli ya kati basi tutafika mbali.

Mkuu hii makitu ya wawekezaji tuachane nayo, nchi itajengwa na wananchi wenyewe. Shirika letu la reli liwe public Company ambapo wananchi wote wawe na uwezo wa kuwekeza na wahimizwe kuwekeza kama njia ya kuisaidia nchi yao.
 
Kiongozi wazo lako zuri sana ila kama hizo zingine wanatafuna na hatupati majibu mujarabu, bado tunaimani tukijichanga tena buku buku zetu hawatakula????

Mtazamo wangu tatizo sio pesa, tatizo letu ni uongozi kutokuwa na Vision.
tusifanye kwa vile "Kenya, Rwanda is doing it", bali tunafanya kwa sababu mipango yetu ni 1,2,3.....!!
 
Mkuu wazo lako ni zuri sana

Lakini nadhani kama serikali ikipata muwekezaji wa maana kutoka nje au ndani mwenye uwezo wa kuitengeneza vizuri reli ya kati basi tutafika mbali.

Mawazo kama hayo yako Lukosi peleka kwa wauza unga wenzako. Rasilimali zilizopo nchini zinatutosheleza kujenga hyo reli ya kati. Tukianzia na utalii bahari na maziwa migodi ya kila aina ya madini tunayo. Gasi mafuta tunavyo kwanini tukatafute mwekezaji tena? Kama niwawekezaji tumekua nao wengi lakin wametuletea maendeleo gani? Au nawewe umeshapata wahuni wenzako unataka kuwaleta tanzania kuja kutuibia ukisema niwawekezaji? Chris Lukosi jitizame upya naona mabox yanaendelea kupunguza upeo wako wa kufikiri.
 
Mkuu wazo lako ni zuri sana

Lakini nadhani kama serikali ikipata muwekezaji wa maana kutoka nje au ndani mwenye uwezo wa kuitengeneza vizuri reli ya kati basi tutafika mbali.

Wawekezaji wazalendo wapo lakni wataambulia matusi kutokana na serikali ya chama chenu CCM. Utasikia mitaji yenu niya kwenye juisi soda na maji.
 
Mkuu hii makitu ya wawekezaji tuachane nayo, nchi itajengwa na wananchi wenyewe. Shirika letu la reli liwe public Company ambapo wananchi wote wawe na uwezo wa kuwekeza na wahimizwe kuwekeza kama njia ya kuisaidia nchi yao.
Ndio maana nikasema wawekezaji toka ndani na nje.

Mimi nina uhakika kama reli ikibinafsishwa na kupewa wawekezaji wa maana wenye uwezo na hisa zikauzwa kwa wananchi basi reli itasonga mbele kwani wengi watakuwa na machungu.

Lakini pamoja na hilo, mimi naamini kwa kasi iliyoonyeshwa na serikali yetu kwenye ujenzi wa barabara nchi nzima, basi serikali inauwezo wa kuiboresha reli ya kati na si tu kuiboresha iliyopo bali kujenga line nyingine ili treni ziwe zinapishana kuongeza kasi ya usafirishaji . pia nina uhakika kama rasilimali zetu zilizopo zikitumiwa vyema reli ya kati yaweza kuwa tu sawa na zile nilizowahi ziona south africa.

Uzuri ni kwamba reli ipo tayari kinachotakiwa ni kuboresha miundombinu na utendaji.

Kwa hili siasa tuweke kando. NAKUUNGA MKONO !
 
Mkuu tupo milion 44 tunaondoa watoto na wazee,kwa hesabu ya elfu elfu.bilioni 100 haifiki.
Pia upembuzi yakinifu haujafanywa kujua actual cost ya maintanance ya miundombinu ya reli ni kiasi gani,kumbuka reli yetu ni chakavu.
Vilevile kuwapa wananchi mzigo huo ni kuwaonea kwani wanakamuliwa kodi mpaka basi,na matumizi ya kodi katika nchi hii ni ya israfu.
Selikali ipunguze matumizi yasiyokuwa ya lazima wajenge reli,wao wamekazana na viwanja vya ndege tuu.
Mfano ni mipango mibovu kutumia mabilioni ya shilingi kujenga kiwanja kingine cha ndege sumbawanga kuacha kutoa reli mpanda mpaka bandari ya kasanga takribani km 130.
Reli ni usafiri wa wanyonge na ndio wengi nchi hii.
 
Kiongozi wazo lako zuri sana ila kama hizo zingine wanatafuna na hatupati majibu mujarabu, bado tunaimani tukijichanga tena buku buku zetu hawatakula????

Mtazamo wangu tatizo sio pesa, tatizo letu ni uongozi kutokuwa na Vision.
tusifanye kwa vile "Kenya, Rwanda is doing it", bali tunafanya kwa sababu mipango yetu ni 1,2,3.....!!

Mkuu,

Wakati mwingine maamuzi ya kibiashara hutokana na nini competitors wanafanya. Kwa mfano Airtel wakija na promotion fulani, automatically washindani wao itabidi wajipange na kuja na counter offer vinginevyo baada ya muda mfupi watapoteza wateja wao. Bandari na uchumi wetu unakuwa threatened na mipango inayoendelea kuhusu bandari ya Mombasa na tusipochukua uamuzi mapema tutajikuta mizigo yote ya nchi jirani kama DRC, Uganda, Burundi na Rwanda inatuhama lakini tukireact tutaweza kuwabakiza wafanya biashara hata wa zile nchi zinazoshiriki kwenye mpango wa Mombasa kwani at the end of the day wafanya biashara wanaangalia ni wapi watapata faida zaidi
 
Mkuu tupo milion 44 tunaondoa watoto na wazee,kwa hesabu ya elfu elfu.bilioni 100 haifiki.
Pia upembuzi yakinifu haujafanywa kujua actual cost ya maintanance ya miundombinu ya reli ni kiasi gani,kumbuka reli yetu ni chakavu.
Vilevile kuwapa wananchi mzigo huo ni kuwaonea kwani wanakamuliwa kodi mpaka basi,na matumizi ya kodi katika nchi hii ni ya israfu.
Selikali ipunguze matumizi yasiyokuwa ya lazima wajenge reli,wao wamekazana na viwanja vya ndege tuu.
Mfano ni mipango mibovu kutumia mabilioni ya shilingi kujenga kiwanja kingine cha ndege sumbawanga kuacha kutoa reli mpanda mpaka bandari ya kasanga takribani km 130.
Reli ni usafiri wa wanyonge na ndio wengi nchi hii.

Hii itafika na kuzidi kwani kuna makampuni na wananchi ambao watachangia zaidi ya 1,000. Kama hili jambo likisimamiwa vizuri na upembuzi yakinifu ukafanyika basi watu wengi zaidi watashiriki ili mradi kusiwe na lazima na wananchi na mashirika yahimizwe kuchangi nyingi kadri iwezekanavyo.

MUHIMU kuwe na uwazi kwenye mapato na matumizi ili kuhakikisha kuwa kuna uwajibikaji wakutosha
 
Hii itafika na kuzidi kwani kuna makampuni na wananchi ambao watachangia zaidi ya 1,000. Kama hili jambo likisimamiwa vizuri na upembuzi yakinifu ukafanyika basi watu wengi zaidi watashiriki ili mradi kusiwe na lazima na wananchi na mashirika yahimizwe kuchangi nyingi kadri iwezekanavyo.

MUHIMU kuwe na uwazi kwenye mapato na matumizi ili kuhakikisha kuwa kuna uwajibikaji wakutosha

Wananchi,mashirika,taasisi na asasi naamini hawatakuwa na tatizo kuchangia.Tatizo ni hii kitu kugeuka ulaji.
Labda wafanye hivi,paundwe tume huru ya bunge kutoka kamati ya miundombinu,papatikane timu ya wataalamu wafanye upembuzi yakinifu,tume hiyo ya bunge ilatibu mchakato mzima kuanzia uchangiaji sambamba na kutangaza zabuni hadi kupata mkandarasi ujenzi hadi kukamilika kwa reli ndipi ikabidhiwe selikali.
Wakati huo bodi ya reli na uongozi,kanuni na taratibu zimebadilishwa na kuweka zenye kukidhi matakwa ya reli na watumiaji.
Vinginevyo pesa yetu italiwa na mie sitochanga nitatoa sadaka kanisani.
 
Kufuatia mikakati ya nchi za Kenya, Uganda and Rwanda kuiengua nchi yetu kwenye mipango ya jumuia ya Afrika Mashariki nashauri yafuatayo yafanyike haraka iwezekanayo ili kuliwezesha taifa kuwa na uwezo wa kusafirisha mizigo kwa haraka na kwa gharama kidogo ili kuhakikisha kuwa mizigo ya nchi marafiki kama Burundi na DRC inapitia Dar.
  • Serikali iitishe hambee ya wananchi wote ili kuchangia mfuko utakaowezesha ujenzi wa reli hii kwa haraka, kwa mfano ikiwaomba wananchi wake wachangie angalau 1,000 kila mtu ndani ya mwaka mmjo serikali inaweza kukusanya zaidi ya bil.100, mchango huu uwe wa hiari au
  • Serikali ikaribishe wananchi wake kununua hisa kwenye kampuni ya reli, hisa hizi ziuzwe kwa bei ndogo kabisa ili kuwawezesha watanzania wengi zaidi kushiriki, hamasa iwekwe kwa wananchi wengi zaidi kuchangia ili kuliwezesha taifa kuwa na uwezo wa kushindana kibiashara na mataifa mengine kwa kupunguza gharama za usafirishaji/uzalishaji

Naamini njia hii ni rahisi na ikitekelezwa ipasavyo itawezesha kupatikana pesa nyingi na kwa haraka bila kuliweka taifa rehani.

Harambee ya nini? wakati wana kila kitu.
Mie ningewashauri ya kwamba,
-Nzega resolute mining wape wawakezaji wachimbe miaka 10, harafu hao wawekezaji wajenge bandari kubwa za kutosha Tanga, Mtwara na Dar.

-Nyamongo mining wape wawakezaji wachimbe miaka 10, watengeneze electrical power source kwa maji/uranium utoshe kuendesha mahitaji yetu yote mhimu na usalie kuwauzia jirani kama watahitaji.

-Biharamulo mining wape wawekezaji wachimbe miaka 10, wakujengee viwanja vya ndege vya kimataifa mwanza, dar,kigoma na mbeya.
-Gas mtwara wape miaka 20, wajenge reli na train za kasi zinazotumia umeme, kutoka mtwara hadi mipakani kote huko kusini. kutoka dar mpaka mipakani mwa burundi,rwanda na congo, kutoka Tanga mpaka mpakani mwa kenya na ziwa victria.

Ukiamaliza hapo shusha bei ya mizigo za bandari kwa bei nusu ya wengine wote washindani, kwenye bandari na aiport. Ondoa ukiritimba wote, mbona hapo utanifaika sana na unaendelea kwa kasi sana na resource zako zinakuwa zimekulipa vyema ahata wakizimalizamo, utakuwa umebaki na sustainable market.
 
Mkuu,

Wakati mwingine maamuzi ya kibiashara hutokana na nini competitors wanafanya. Kwa mfano Airtel wakija na promotion fulani, automatically washindani wao itabidi wajipange na kuja na counter offer vinginevyo baada ya muda mfupi watapoteza wateja wao. Bandari na uchumi wetu unakuwa threatened na mipango inayoendelea kuhusu bandari ya Mombasa na tusipochukua uamuzi mapema tutajikuta mizigo yote ya nchi jirani kama DRC, Uganda, Burundi na Rwanda inatuhama lakini tukireact tutaweza kuwabakiza wafanya biashara hata wa zile nchi zinazoshiriki kwenye mpango wa Mombasa kwani at the end of the day wafanya biashara wanaangalia ni wapi watapata faida zaidi

Mkuu,
DRC kwa sasa anajenga barabara toka Sumbawanga hadi Kasanga ziwa Tanganyika,hii inamaana kwamba atakiwa anatoa mizigo Dar kupitia Mbeya-Sumbawanga then anapeleka katika bandari yake anayojenga hapo kasanga ili avushe kiurahisi kwenda DRC.
Sasa reli ya kati imeishia Mpanda mkoani Katavi,hii ina maana tukivuta reli toka Mpanda hadi Kasanga tutamkamua jamaa kwani atatumia reli Dar-tabora-mpanda-kasanga,then tutamkamua na njia ya barabara Dar-mbeya-sumbawanga-kasanga.
 
Back
Top Bottom