Chivundu
Platinum Member
- Dec 17, 2012
- 13,054
- 26,192
napendekeza huu mpango usimamiwe na NCHEMBA
Ohoo,hili likiingizwa siasa basi imeisha.
CC: Ntemi Kazwile
napendekeza huu mpango usimamiwe na NCHEMBA
ni wazo zuri lakini tatizo wenye malori watakubali? rejea kauli za Maige za kupata hela za kununua nyumba ya usd 700,000.00.Kufuatia mikakati ya nchi za Kenya, Uganda and Rwanda kuiengua nchi yetu kwenye mipango ya jumuia ya Afrika Mashariki nashauri yafuatayo yafanyike haraka iwezekanayo ili kuliwezesha taifa kuwa na uwezo wa kusafirisha mizigo kwa haraka na kwa gharama kidogo ili kuhakikisha kuwa mizigo ya nchi marafiki kama Burundi na DRC inapitia Dar.
- Serikali iitishe hambee ya wananchi wote ili kuchangia mfuko utakaowezesha ujenzi wa reli hii kwa haraka, kwa mfano ikiwaomba wananchi wake wachangie angalau 1,000 kila mtu ndani ya mwaka mmjo serikali inaweza kukusanya zaidi ya bil.100, mchango huu uwe wa hiari au
- Serikali ikaribishe wananchi wake kununua hisa kwenye kampuni ya reli, hisa hizi ziuzwe kwa bei ndogo kabisa ili kuwawezesha watanzania wengi zaidi kushiriki, hamasa iwekwe kwa wananchi wengi zaidi kuchangia ili kuliwezesha taifa kuwa na uwezo wa kushindana kibiashara na mataifa mengine kwa kupunguza gharama za usafirishaji/uzalishaji
Naamini njia hii ni rahisi na ikitekelezwa ipasavyo itawezesha kupatikana pesa nyingi na kwa haraka bila kuliweka taifa rehani.
Mimi kwa hili niko na tayari elfu kumi zipo tayari, fanyeni haraka mkuu.
Mkuu wazo lako ni zuri sana
Lakini nadhani kama serikali ikipata muwekezaji wa maana kutoka nje au ndani mwenye uwezo wa kuitengeneza vizuri reli ya kati basi tutafika mbali.
Mkuu,
DRC kwa sasa anajenga barabara toka Sumbawanga hadi Kasanga ziwa Tanganyika,hii inamaana kwamba atakiwa anatoa mizigo Dar kupitia Mbeya-Sumbawanga then anapeleka katika bandari yake anayojenga hapo kasanga ili avushe kiurahisi kwenda DRC.
Sasa reli ya kati imeishia Mpanda mkoani Katavi,hii ina maana tukivuta reli toka Mpanda hadi Kasanga tutamkamua jamaa kwani atatumia reli Dar-tabora-mpanda-kasanga,then tutamkamua na njia ya barabara Dar-mbeya-sumbawanga-kasanga.
Wazo zuri. Financing reli yote yenye urefu takribani km 2,000 (kumbuka reli inazunguka sana) tunaweza hitaji kama tillioni 15 hivi (Railway Finance). It is say 4 years project...
Tunaweza kugawana hivi:
- 40% -Government (each year 10%)
- 20% - International institutions/countries (EU, IMF, nchi zingine wapenda maendeleo)
- 15% - Organizations and companies in the country (mining, communication, banking, institutions, business entities etc)
- 25%- wananchi wote kwa hiari yao
Harambee ya nini? wakati wana kila kitu.
Mie ningewashauri ya kwamba,
-Nzega resolute mining wape wawakezaji wachimbe miaka 10, harafu hao wawekezaji wajenge bandari kubwa za kutosha Tanga, Mtwara na Dar.
-Nyamongo mining wape wawakezaji wachimbe miaka 10, watengeneze electrical power source kwa maji/uranium utoshe kuendesha mahitaji yetu yote mhimu na usalie kuwauzia jirani kama watahitaji.
-Biharamulo mining wape wawekezaji wachimbe miaka 10, wakujengee viwanja vya ndege vya kimataifa mwanza, dar,kigoma na mbeya.
-Gas mtwara wape miaka 20, wajenge reli na train za kasi zinazotumia umeme, kutoka mtwara hadi mipakani kote huko kusini. kutoka dar mpaka mipakani mwa burundi,rwanda na congo, kutoka Tanga mpaka mpakani mwa kenya na ziwa victria.
Ukiamaliza hapo shusha bei ya mizigo za bandari kwa bei nusu ya wengine wote washindani, kwenye bandari na aiport. Ondoa ukiritimba wote, mbona hapo utanifaika sana na unaendelea kwa kasi sana na resource zako zinakuwa zimekulipa vyema ahata wakizimalizamo, utakuwa umebaki na sustainable market.
Mwakyembe hana maamuzi binafsi, mpaka apige simu Bagamoyo ndio achukuwe hatua rejea sakata la bodi ya tpa vs mngt ya tpa na sasa maamuzi ya sumatraKwa michango niliyoiona hapa kuhusu hii thread inaonesha kumbe wengi wetu ni wazalendo.....kwanini Mwakyembe asichukue proposal hii?
Mkuu this is an excellent idea. Maana hata kodi hatupati kwa hizo rasilimali zetu. Tungeingia nao mikataba ya aina hii kweli nchi ingefika mbali sana kimaendeleo.
Mkuu hii makitu ya wawekezaji tuachane nayo, nchi itajengwa na wananchi wenyewe. Shirika letu la reli liwe public Company ambapo wananchi wote wawe na uwezo wa kuwekeza na wahimizwe kuwekeza kama njia ya kuisaidia nchi yao.
Hao jamaa unawaacha wanaenda mpaka wanafika mwisho, wakifika mwisho we unaishusha gharama karibu nusu ya Mombasa tuone watafika wapi.
Wazo zuri. Financing reli yote yenye urefu takribani km 2,000 (kumbuka reli inazunguka sana) tunaweza hitaji kama tillioni 15 hivi (Railway Finance). It is say 4 years project...
Tunaweza kugawana hivi:
- 40% -Government (each year 10%)
- 20% - International institutions/countries (EU, IMF, nchi zingine wapenda maendeleo)
- 15% - Organizations and companies in the country (mining, communication, banking, institutions, business entities etc)
- 25%- wananchi wote kwa hiari yao
mawazo mazuri kama haya ndo tunayoyataka hapa jf. Kwa namna hii tunaweza kuendelea kama yatafanyiwa kazi.