Serikali ifikirie kufanya somo la Rasilimali Watu (HR) kuwa lazima vyuo vikuu

fredito13

JF-Expert Member
Sep 3, 2012
213
145
Wakuu,

Nina miaka karibia 10 ya utumishi kwenye sekta binafsi. Nimefanya kwenye makampuni na NGO's kadhaa hapa nchini na kikubwa ambacho ninakiona ni Watanzania kutojua haki zetu maofisini na sheria za kazi!

Kwa kiasi kikubwa, sisi Watanzania ambao tunaajiriwa sekta binafsi, wengi ni wahanga wa kukosa elimu ya wajibu na haki zetu kama wafanyakazi!

Wawekezaji wengi wanawatumia ndugu zetu wa Kitanzania kupora haki zetu za msingi katika ajira. Kwa sababu ya ufahamu mdogo, wengi huwa tunaishia kuwa wanyonge na kukubali matakwa ya waajiri hata pale tunapoumia! Mikataba mingi huandaliwa na upande mmoja na wengine husaini bila kujua kilichoandikwa (isipokua mshahara na JD tu). Mara nyingi waajiri wanavunja mikataba yetu na kutuendesha wanavyotaka, lakini kwa sababu ya uelewa mdogo na hofu ya kukosa ajira basi tunakwenda tu.

Kuna watu wako kwenye ajira mwaka wa 2 mfululizo lakini bado wanaambiwa wao ni vibarua. Kuna watu hawapati michango yao ya Pensheni (NSSF), kuna watu wanalipwa mshahara tarehe anayoamua mwajiri na kuna wenzetu wanakubali mpaka 'kuwambwa' makofi na mabosi kwa sababu ya ajira.

Ifike wakati sasa serikali kupitia TCU, Wizara ya Elimu na taasisi zingine zinazohusika wafikirie kuifanya kozi ya Rasilimali watu (Human Resources) kuwa ni ya lazima kwa wanafunzi wote wa vyuo vikuu, hasa mwaka wa mwisho wa masomo yao. Kama tumeweza kuwa na Computer Course ya lazima kwa kila mwaka wa kwanza chuoni, tuifanye HR lazima kwa wanaoandaliwa kuingia soko la ajira.

Kwa kuwepo course hii, Watanzania wengi wataifahamu sheria ya Kazi na Mahusiano kazini ambayo hutoa mwongozo wa haki na wajibu wa mwajiri na mwajiriwa. Sheria hii itatusaidia kupunguza manyanyaso ofisini ambayo yanatekelezwa na waajiri kupitia 'Watanzania wenzetu'. Pia, itatusaidia kujenga uwezo wa kusimamia na kusimamiwa pasipo kupimana nguvu maofisini!

Kuna mengi yanakosekana kwenye mfumo wetu wa elimu. Lakini hili rahisi linawezekana na litatusaidia hata kwenye mapato ya serikali!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ifike wakati sasa serikali kupitia TCU, Wizara ya Elimu na taasisi zingine zinazohusika wafikirie kuifanya kozi ya Rasilimali watu (Human Resources) kuwa ni ya lazima kwa wanafunzi wote wa vyuo vikuu, hasa mwaka wa mwisho wa masomo yao. Kama tumeweza kuwa na Computer Course ya lazima kwa kila mwaka wa kwanza chuoni, tuifanye HR lazima kwa wanaoandaliwa kuingia soko la ajira.
Sioni mantiki ya ushauri wako. Tuna watu wanasomea HR, Public Administration, Labour Lwas ndani ya sheria sasa kama hawa wanashindwa kazi zao basi tutafute njia nyingine ya kuwafanya wawe waadilifu na wenye maadili ya kazi yao. Tunajua pia wengi wa watanzania wana athirika kwa kuto kujua sheria lakini huwezi kusema kila mwanafunzi wa chuo afundishwe sheria. Mfano wako wa komputa sio sawa. Katika dunia ya sasa technolojia ya tehama haikwepeki na inarahisisha mambo mengi bila kujali uko taaluma gani-hivyo ni jukumu la kila chuo kuona ya kua wahitimu wake si mbumbu wa tehama (computer applications). Hata hivyo kuna vyuo vingi duniani kujifunza computer kunashauriwa lakini hakuko ndani ya mtaala bali vyuo vinahakikisha kila mwenye unitaji anapata nafasi ya kujifunza.
Sio kila kitu cha muhimu lazima kifundishwe kwa wanafunzi wote bali wenye uhitaji wanaweza kutayarishiwa mafunzo maalum nje ya mitaala bila kuwa waangalifu basi muda wa masomo utajaa masomo kama haya: HR (ushauri wako), Ukimwi, Mafuriko, Climate change, Corruption etc ambayo ingawapo yanatoa elimu nzuri lakini ili yafundishwe yanachukua muda kutoka kwenye mitaala/program watu wanazosomea.
 
Kozi ya hr, sio ya muhimu, kitu muhimu kabisa kuliko vyote ni somo la Labour law Lifanywe ni la lazima for instance graduate anapo hitimu anapaswa kujuwa sheria hizi mfano employment and labour relation act (na amendments zote), Labour institutions act, public service act, public service regulations 2009, standing orders, employment and labour relations code of good practice, social security laws eg Nssf act, psssf act, ukizijuwa hizo sheria Vizuri sana nilizo zitaja unakuwa una elewa!
Additionally siku hizi kuna development imekuwa kwa kasi taasisI wanaajiri mawakili /lawyers kufanya kazi za hr, nahisi ni kwa sababu wengi wao hawajifunzi Vizuri labor laws Ndiyo maana wanapewa mawakili kazi zao
 
Back
Top Bottom